Nampongeza IGP na jeshi la polisi kwa ujumla kwa kuona umuhimu wa kuimarisha ulinzi kwenye vituo vyetu. pamoja na kuimarishwa huko kwa kuongeza idadi ya askari walinzi wa vituo, kuweka askari wenye silaha, na kuweka standby bodaboda lakini bado kuna changamoto chache ambazo mkuu unapaswa kuzielewa.
Boresha ulinzi na rekebisha mpasuko unaoendelea baina ya wananchi na jeshi lako.
- Askari kuendelea kuishi kwa mazoea ya kawaida
- Kama ukiwa makini unaweza kuona kuwa bado kuna baadhi ya askari wanafanya mazoea mabaya kama watumishi wengine wa umma wa Tanzania. pamoja na kuwa kwenye state of high alert bado kuna askari wenye silaha unawakuta wanashughulika na kusoma magazeti, wanashughulishwa na simu zao au wapo wanapiga soga either wao kwa wao au na watu wengine waliovaa kiraia. nadhani kwenye state ya sasa, ni risk kwa askari mlinzi akiwa kazini kuwa na multiple tasks maana itampunguzia umakini.
- Uwepo shughuli nyingine za kijamii zisizo rasmi kwenye vituo
- Pamoja na kuweka vizuizi kwenye maeneo ya vituo vya polisi ili kutoruhusu watu wasikatize, lakini bado kwenye vituo vingi vya polisi kuna shughuli nyingi zinazozua mikusanyiko isiyo rasmi ambayo pia inatoa access kwa watu wasiokuwa askari kufika karibu na ofisi. watu wa breakdowns wamewekeza kwenye vituo na wanashinda hapo, lakini pia wapo baadhi ya wafanyabiashara wa vyakula, magazeti na bidhaa nyingine au huduma nyingine ndogondogo wanakuwa maeneo karibu sana na vituo, angalau kwa sasa, wasitishe huduma hadi hapo hali ikiwa shwali.
- Mlundikano wa magari na bodaboda
- mkusanyiko mkubwa wa magari na bodaboda zilizofikishwa vituoni kutokana na matukio mbalimbali vinawaweka polisi kwenye wakati mgumu wa ku-manage eneo lenu, hata likitokea tatizo (ambush) hata nyinyi wenyewe mnalazimishwa ku-escape kupitia maeneo machache sana.
- Askari wa usalama barabarani kutoshiriki operation
- siwezi kusema najua ni kwa jinsi gani askari wetu wamejipanga, ila kwa sasa, hawa askari wa barabarani wanapaswa nao waache kuabudu kuandika fine tu, nao check point zao zingejita Zaidi kwenye kuchunguza watu tunaokuwa ndani ya magari kuliko kulitazama gari/bodaboda. waharifu wangeogopa Zaidi kama wangejua kuwa sasa hata wao watahojiwa wakiwa kwenye vyombo vyao.
- ubabe dhidi ya wananchi
- mnahitaji sana support ya raia so tushirikiane badala ya kufanya ubabe
Boresha ulinzi na rekebisha mpasuko unaoendelea baina ya wananchi na jeshi lako.