Helo, mie nimesoma agronomy nenda kapambane vizuri ugumuwake ni kama civil engineering vile, kwahyo msuli unahitajika, tulikuwa 26 tu na msichana 1 tu tulipoanza bt wengi walianza kudisco kama mvua tukamaliza 14 akiwepo na huyo msichana ngangali. Ukifika unakutana na physcal chemistry inafundishwa na Elisante, Nkoma, Tungaraza hawa ni wataalamu wa kula vichwa vizembe vinavyofikiri kuchaguliwa chuo ni ufahari baada ya kupiga kitabu, pia utakutana na Maro mtaalam wa soil rocks hii ni kama geology ya COET vile, pia Dr. Kaaya, Kilasala, hao ni waliobobea katika soil chemistry, soil fertility, na kuna practical za kufa mtu kwenye maabara za udongo, jiandae hii ukiendekeza FB, Whatsapp, Viber chat na mengine basi unadisco hata kabla ya miaka 3. Pepa kila jumapili kuanzia saa tano baada ya ibada zinafanyikia pae freedom square, professor atasimama juu ya dawati akikisimamia usiangalizie, pepa ya majibu unapewa ikiwa na mihuri, ukienda toilet jua mgambo wapo wanakusindikiza hello SUA hakuna ulelemama wala cheating wale jamaa hawana huruma Once you are caught gilt you shall be expelled out soon.