Usaliti wa njia ya mtandao

Gorgeousmimi

JF-Expert Member
Jun 21, 2010
9,296
7,683
Hey hey good people,

Leo ningependa tujadiliane kuhusu usaliti kwa njia ya mtandao na kanuni zipi ambazo zinaweza kutumika kuashiria usaliti kwa njia hio.

Kama tunavyotambua usaliti upo katika mafungu tofauti na uzito tofauti.Je huu usaliti kwa njia ya mitandao ya aina mbalimbali kama Facebook,Viber,Whatsapp,Twiter,Instagram au hata hapa Jamiiforums tunaupa uzito gani?

Nikiongelea usaliti wa aina hii namaanisha ile kuongea na mtu ambae huna mahusiano nae yoyote kuhusu masuala ambayo yanaweza kuleta hamasa tofauti,kumpa mtu huyo uhuru wa kuwasiliana na wewe,kuongea nae maongezi ya kimahaba,kuitana majina ya kimapenzi,kuanika hisia zako kwa mtu huyo n.k

Viashiria vipi vinaweza kutumika ili kudhihirishia kama huu usaliti umepiga hatua mbele,iwapo mwenza wako anapoteza hisia juu yako au mawasiliano yamenoga mpaka mwenza wako anakudharau na kuupa kipaumbele usaliti huu?Au kama wasaliti hawa wana miadi ya kuonana?

Kwa nadharia tu,watu wanaotenda usaliti wa aina hii wana madhumuni ya kupata manufaa gani?Je kuna sababu zinazoweza kupelekea wahusika hawa kutenda usaliti kwa njia hii?Mfano kutafuta vile vitu ambavyo anavikosa kwenye mahusiano yao,kwahio wanatafuta kipoozeo? Au ni tabia na hulka tu?

Tujadiliane.

Wasalaam G
 
Hey hey good people,

Leo ningependa tujadiliane kuhusu usaliti kwa njia ya mtandao na kanuni zipi ambazo zinaweza kutumika kuashiria usaliti kwa njia hio.

Kama tunavyotambua usaliti upo katika mafungu tofauti na uzito tofauti.Je huu usaliti kwa njia ya mitandao ya aina mbalimbali kama Facebook,Viber,Whatsapp,Twiter,Instagram au hata hapa Jamiiforums tunaupa uzito gani?

Nikiongelea usaliti wa aina hii namaanisha ile kuongea na mtu ambae huna mahusiano nae yoyote kuhusu masuala ambayo yanaweza kuleta hamasa tofauti,kumpa mtu huyo uhuru wa kuwasiliana na wewe,kuongea nae maongezi ya kimahaba,kuitana majina ya kimapenzi,kuanika hisia zako kwa mtu huyo n.k

Viashiria vipi vinaweza kutumika ili kudhihirishia kama huu usaliti umepiga hatua mbele,iwapo mwenza wako anapoteza hisia juu yako au mawasiliano yamenoga mpaka mwenza wako anakudharau na kuupa kipaumbele usaliti huu?Au kama wasaliti hawa wana miadi ya kuonana?

Kwa nadharia tu,watu wanaotenda usaliti wa aina hii wana madhumuni ya kupata manufaa gani?Je kuna sababu zinazoweza kupelekea wahusika hawa kutenda usaliti kwa njia hii?Mfano kutafuta vile vitu ambavyo anavikosa kwenye mahusiano yao,kwahio wanatafuta kipoozeo? Au ni tabia na hulka tu?

Tujadiliane.

Wasalaam G

Kwanza kabisa napenda niseme kuwa usaliti katika mahusiano kwa njia ya mtandao upo na kadiri siku zinavyozidi kwenda ndivyo jinsi usaliti huu kwa kutumia mitandao unavyozidi kuongezeka.

Watu wengi wanaofanya usaliti kwa njia ya mtandao, hufanya usaliti huo kwa sababu mbali mbali. Wengine ni kwa sababu ya kutaka faraja kutokana na matatizo yanayomkumba katika uhusiano wake, wengine ni kwa sababu ya kutafuta kitu fulani ambacho ananakikosa kwa mpenzi wake ambacho anadhani atakipata kwa huyo ambaye anafanya naye usaliti. Lakini wengi wao hufanya usaliti kwa sababu ya kutokuwa na msimamo, tamaa ya uzinzi na kutaka kuanzisha uhusiano na kila mwanamke au mwanauem anayemvutia machoni pake.

Mwanzoni uhusiano huu huanza kama mzaha tu, lakini kadiri mawasiliano yao yanavyozidi kuimarika ndivyo ukaribu wao unavyozidi kuongezeka na hatimaye kujikuta wamekuwa wapenzi kabisaaa.

Kugundua kama mtu anakusaliti au akusaliti ni mtihani mgumu sana hasa kwa mtu ambaye ni msiri kupitiliza na kwa mtu ambaye anayeweza kuigiza na kuficha hisia zake. Lakini waswahili wanasema, "Penzi ni kikohozi" maana yake upendo hauwezi kujificha. Kwa kusema hayo, naomba niainishe dalili ambazo zinaweza kukusaidia na kusaidia wengine kutambua mpenzi ambaye anasaliti iwe kwa njia ya mtandao au kwa njia nyingine yoyote ile:

Atapunguza Mapenzi Kwako
Katika ulimwwengu huu hakuna binadamu anayeweza kupenda watu wawili au zaidi ya wawili kwa wakati mmoja na akawapa upendo wenye uwiano sawa. Ama atampenda huyu na kumchukia huyu, au atakashikama na huyu na kumdharau yule.

Atapunguza Mawasiliano na Wewe
Mtu ambaye anakusaliti lazima atapunguza kukujali na kuwasiliana na wewe kwa sababu muda mwingi akili yake na mawazo yake yote yapo kwenye kuimarisha uhusiano huo mpya na ndio maana wakati mwingine zinaweza zikapita siku kadhaa asiliwasiliane na wewe bila ya sababu ya msingi na hata ukimuuliza anaweza akakupa sababu zisizokuwa za msingi. Na hii yote ni kwa sababu upendo wake kwako umepungua.

Anakuwa Msiri
Uhusiano wa kusaliti huwa sio uhusiano halali kwa sababu hiyo, lazima uhusiano huo ufanyike kwa siri. Hivyo mtu ambaye anafanya usaliti lazima atakuwa msiri sana kwa mambo yote anayoyafanya kati yake na huyo anayesaliti naye, hiyo ikiwa ni pamoja na mawasiliano yao na dating appointments zao na ndio maana hata wakati mwingine mpenzi ambaye anasaliti anakuwa hakupi uhuru na simu yake, login passwords za social accounts zake etc. Ukiona mpenzi wako amekuwa msiri kuliko kawaida tena bila ya sababu za msingi ujue kuna uwezekano kuwa mpenzi wako anakusaliti.

Atakuwa Mtu wa Kukulaumu
Siku zote mahali penye upendo wa kweli huwa kuna uvumilivu. Lakini upendo huo unapopungua na kutoweka uvumilivu nao hutoweka.

Hivyo mtu ambaye anakusaliti atakuwa mtu wa kukulaumu na kukutamkia maneno yasiyofaa hasa pale unapokosea badala ya kukukosoa na kukurekebisha kwa upendo. Na yote hiyo ni kwa sababu upendo wake kwako umepungua na ndio maana anashindwa kuvumilia mapungufu yako na anashindwa kukuvumia na kukusamehe hasa pale unapokosea.
 
Mleta mada nadhani hujaolewa wewe! wenye ndoa ndiyo sehemu zao za kupunguzia msongo wa mawazo. kungekuwa hakuna haya ma-mitandao wengi wangekuwa makaburimi.
Je kipindi kile ambacho kulikuwa hakuna mitandao,hao wanandoa walikuwa wana punguza misongo ya mawazo wapi?
 
apa niwe msomaji kwanza .. ili napo enda kutoa marufuku niwe na uhakika na nacho kifanya
 
Ni baadhi ya sababu inayonifanya nisishike simu ya bi mkubwa kabisa...Unamwita mtu yes sweet, Honey,My love..Halafu unaniambia ni utani tu huyu mtu tumezoeana tu kwenye mtandao u can't blve wala simjui na yeye hanijui'''Arghhh...
duuh,unajua wife kazini anataniana na wangapi?maana hapo umezungumzia kushika simu yake tu...mimi naona ni kheri wakiwa na utani wa hivyo usiwe na kificho,kukishakua na siri kati ya mawasiliano basi hapo jua huna chako
 
Je unauongeleaje..Ni kitu kibaya?..Katika misingi ipi?
Hahaha daddy unajua binadamu tuna asili ya kitu kimoja "nikifanya mimi ni sawa ila ukifanya wewe ni kosa kubwa". Me naweza nikawa naona sawa coz maybe nachat tu na mtu online, sijaonana naye wala kufanya naye chochote na ni kweli sina mpango naye wowote. Lakini akifanya partner wangu sitoamini kama kila kitu kinaishia online as I do. So hata kama hakuna kitu kitakachotokea physically still hapa kuna "emotional cheating/betrayal". (Mfano hapa jf tuchukulie mawasiliano ya pm, Tuache utani unaoishia jukwaani)

The fact kwamba partner wangu anawasiliana na mtu mwingine regularly (anapata muda wa kumuwaza girl mwingine apart from me) inaweza kuharibu mahusiano kabisa , na kadri wanavyocontact wanaform a certain bond na ndo wanazidi kufahamiana kila siku. Imagine unaamka asubuhi afu cha kwanza Unawaza kum-pm rubii, huku atoto hata hujamtafuta teh. It kills trust pale partner wako atakapofuma conversation zenu, coz hata kama Ukimwambia kuwa huna mpango na huyo mtu na hamjawahi kuonana maybe, obviously mwenzako hatokuamini. Pata picha tunavyokuwaga na confidence za kujiachia nyuma ya keyboard, unafunguka+ maneno matamu tamu mwee as unajua baby hajui wala hanioni. Ile feeling tu ya kujua baby angu ana mtu mwingine anamuwaza na wanaongea hivi na vile inaumiza eti (kizuri nakula peke angu"). Afu lazima ujue unamuibia mpenzi wako muda wake coz itabidi muda mwingine usimtafute uchat na bae wako wa online Teh, so attention ina-divert kidogo

What matters ni nyie partners kuwekeana limit ya matumizi yenu ya Internet. Kama hamuumizwi na hizo flirtings ni sawa, but kama zinawaumiza then you both know what to do
 
duuh,unajua wife kazini anataniana na wangapi?maana hapo umezungumzia kushika simu yake tu...mimi naona ni kheri wakiwa na utani wa hivyo usiwe na kificho,kukishakua na siri kati ya mawasiliano basi hapo jua huna chako
Hakuna cha heri hapo cha msingi mtu ukiwa kwenye mahusiano ama ndoa usikaribishe mazoea yanayovuka mipaka full stop..Utania huo huo wa makazini unakuta hadi mtu anampiga mke wa mtu kibao cha makalio na mdada anakenua tu eti ni utani..Really? Imagine husband ametokea hapo kwa bahati mbaya na kushuhudia hiyo scene...Na hata wale ma-traffic walikamatwa wakidendeka unajua walisema si wapenzi ila walikuwa kwenye utani na mazoea ya kazi tu...
 
duuh,unajua wife kazini anataniana na wangapi?maana hapo umezungumzia kushika simu yake tu...mimi naona ni kheri wakiwa na utani wa hivyo usiwe na kificho,kukishakua na siri kati ya mawasiliano basi hapo jua huna chako

Hata kwa utani iwe wa wazi au wa siri binafsi naona sio sahihi kwa sababu kama kweli watu hao wapo kwenye uhusiano wanaweza kutumia kigezo cha utani kama kuhalalisha, kuficha na kudumisha uhusiano wao.
 
Hata kwa utani iwe wa wazi au wa siri binafsi naona sio sahihi kwa sababu kama kweli watu hao wapo kwenye wanaweza kutumia kigezo cha utani kama kuhalalisha, kuficha na kudumisha uhusiano wao.
...bob,em kasamaraiz ile 'saiklopidia' uloandika juu...inawezekana kuna nondo nimeziruka!
....samahani lakini
 
Hahaha daddy unajua binadamu tuna asili ya kitu kimoja "nikifanya mimi ni sawa ila ukifanya wewe ni kosa kubwa". Me naweza nikawa naona sawa coz maybe nachat tu na mtu online, sijaonana naye wala kufanya naye chochote na ni kweli sina mpango naye wowote. Lakini akifanya partner wangu sitoamini kama kila kitu kinaishia online as I do. So hata kama hakuna kitu kitakachotokea physically still hapa kuna "emotional cheating/betrayal". (Mfano hapa jf tuchukulie mawasiliano ya pm, Tuache utani unaoishia jukwaani)

The fact kwamba partner wangu anawasiliana na mtu mwingine regularly (anapata muda wa kumuwaza girl mwingine apart from me) inaweza kuharibu mahusiano kabisa , na kadri wanavyocontact wanaform a certain bond na ndo wanazidi kufahamiana kila siku. Imagine unaamka asubuhi afu cha kwanza Unawaza kum-pm rubii, huku atoto hata hujamtafuta teh. It kills trust pale partner wako atakapofuma conversation zenu, coz hata kama Ukimwambia kuwa huna mpango na huyo mtu na hamjawahi kuonana maybe, obviously mwenzako hatokuamini. Pata picha tunavyokuwaga na confidence za kujiachia nyuma ya keyboard, unafunguka+ maneno matamu tamu mwee as unajua baby hajui wala hanioni. Ile feeling tu ya kujua baby angu ana mtu mwingine anamuwaza na wanaongea hivi na vile inaumiza eti (kizuri nakula peke angu"). Afu lazima ujue unamuibia mpenzi wako muda wake coz itabidi muda mwingine usimtafute uchat na bae wako wa online Teh, so attention ina-divert kidogo

What matters ni nyie partners kuwekeana limit ya matumizi yenu ya Internet. Kama hamuumizwi na hizo flirtings ni sawa, but kama zinawaumiza then you both know what to do
Yaani umenielewa vyema kabisa.Sasa usaliti wa aina hii unaweza kuvumilika mami?
 
Back
Top Bottom