Gorgeousmimi
JF-Expert Member
- Jun 21, 2010
- 9,296
- 7,683
Hey hey good people,
Leo ningependa tujadiliane kuhusu usaliti kwa njia ya mtandao na kanuni zipi ambazo zinaweza kutumika kuashiria usaliti kwa njia hio.
Kama tunavyotambua usaliti upo katika mafungu tofauti na uzito tofauti.Je huu usaliti kwa njia ya mitandao ya aina mbalimbali kama Facebook,Viber,Whatsapp,Twiter,Instagram au hata hapa Jamiiforums tunaupa uzito gani?
Nikiongelea usaliti wa aina hii namaanisha ile kuongea na mtu ambae huna mahusiano nae yoyote kuhusu masuala ambayo yanaweza kuleta hamasa tofauti,kumpa mtu huyo uhuru wa kuwasiliana na wewe,kuongea nae maongezi ya kimahaba,kuitana majina ya kimapenzi,kuanika hisia zako kwa mtu huyo n.k
Viashiria vipi vinaweza kutumika ili kudhihirishia kama huu usaliti umepiga hatua mbele,iwapo mwenza wako anapoteza hisia juu yako au mawasiliano yamenoga mpaka mwenza wako anakudharau na kuupa kipaumbele usaliti huu?Au kama wasaliti hawa wana miadi ya kuonana?
Kwa nadharia tu,watu wanaotenda usaliti wa aina hii wana madhumuni ya kupata manufaa gani?Je kuna sababu zinazoweza kupelekea wahusika hawa kutenda usaliti kwa njia hii?Mfano kutafuta vile vitu ambavyo anavikosa kwenye mahusiano yao,kwahio wanatafuta kipoozeo? Au ni tabia na hulka tu?
Tujadiliane.
Wasalaam G
Leo ningependa tujadiliane kuhusu usaliti kwa njia ya mtandao na kanuni zipi ambazo zinaweza kutumika kuashiria usaliti kwa njia hio.
Kama tunavyotambua usaliti upo katika mafungu tofauti na uzito tofauti.Je huu usaliti kwa njia ya mitandao ya aina mbalimbali kama Facebook,Viber,Whatsapp,Twiter,Instagram au hata hapa Jamiiforums tunaupa uzito gani?
Nikiongelea usaliti wa aina hii namaanisha ile kuongea na mtu ambae huna mahusiano nae yoyote kuhusu masuala ambayo yanaweza kuleta hamasa tofauti,kumpa mtu huyo uhuru wa kuwasiliana na wewe,kuongea nae maongezi ya kimahaba,kuitana majina ya kimapenzi,kuanika hisia zako kwa mtu huyo n.k
Viashiria vipi vinaweza kutumika ili kudhihirishia kama huu usaliti umepiga hatua mbele,iwapo mwenza wako anapoteza hisia juu yako au mawasiliano yamenoga mpaka mwenza wako anakudharau na kuupa kipaumbele usaliti huu?Au kama wasaliti hawa wana miadi ya kuonana?
Kwa nadharia tu,watu wanaotenda usaliti wa aina hii wana madhumuni ya kupata manufaa gani?Je kuna sababu zinazoweza kupelekea wahusika hawa kutenda usaliti kwa njia hii?Mfano kutafuta vile vitu ambavyo anavikosa kwenye mahusiano yao,kwahio wanatafuta kipoozeo? Au ni tabia na hulka tu?
Tujadiliane.
Wasalaam G