Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,934
Mataifa mengi Duniani, watu walipigana, watu walipoteza uhai na mali, walipoteza wapendwa wao, siyo kwa sababu ya kutaka kupata shule, barabara, hospitali, majumba, magari, umeme, maji n.k; bali kwaajili ya kuupata uhuru wao.
Wala hawakukubali kuyapitia magumu yote hayo ili wabadilishiwe mtu wa kuwanyima uhuru, yaani badala ya mzungu awe mweusi au wa kijani.
Watanzania, wazazi wao baada ya kuhangaikia uhuru. Uhuru huu ilimaanisha kuwa na maamuzi ya waongozwe namna gani, viongozi wapatikane kwa matakwa yao, maisha yao ya kila siku yamriwe na wao wenyewe, wajichagulie wanaowataka kuwaongoza, wapande taratibu za kupata haki zao pale miongoni mwao anapodhulumu, waweke utaratibu wa haki wa kuwatambua na kuwadhibiti wahalifu, n.k.
Kwa bahati mbaya, Watanzania, wamerudi kule kule kwenye ukoloni, tena ukoloni mbaya kuliko hata ule wa mzungu:
1) Mtanzania awe na kosa au hana kosa, polisi ana uwezo wa kumkamata, kumrundika ndani, na kwa kupitia DPP, anaweza kumfungulia mashtaka yoyote anayoyataka yeye, na mtuhumiwa akisota rumande hata miaka, huku polisi wakiendelea kusema uchunguzi unaendelea, bado haujakamilika. HIVI KUNA UKOLONI MBAYA KUUZIDI HUU?
2) Leo hii, mkuu wa Wilaya au Mkoa, anaweza kumwamuru Polisi amkamate raia yeyote kwenye eneo lake la uongozi na kumsweka ndani, hata kama sababu ni kwa sababu ya chuki za kugombania kimada. Utaswekwa ndani, akipenda, baada ya masaa 48, atamwamuru polisi akuachie. HIVI KUNA UKOLONI MBAYA KUUZIDI HUU?
3) Leo hii Rais akitaka anaweza kuwateulia watu wa kuja kuwatawala, mpende msipende, kuanzia mkoani mpaka wilayani (RC, RAS, RPC, DC, DAS, DED, OCD, n.k.). Wawe wana sifa za kuwa viongozi au hawana, iwe mnawataka au hamuwataki, mtataliwa kwa lazima. Hatukumchagua gavana, wala RC, wala DC, wakati wa ukoloni, je, leo tunawachagua? KUNA UKOLONI MBAYA ZAIDI YA HUU?
4) Leo hii, Rais anawateua majaji wote, Mwanashetia mkuu wa Serikali, jaji mkuu, jaji kiongozi, msajili wa mahakama, DPP, IGP, CDF, mkurugenzi wa TISS, n.k. Halafu unadanganywa kuwa eti unaweza kuishtaki serikali ila ili uishtaki, kwanza uombe kibali kwa serikali cha kuishtaki serikali. Na sisi tunaona ni sawa na inawezekana. Hivi kweli sisi tuna akili? Yaani unaenda mahakamani kabisa ukiwa na akili yako, kesi ipo chini ya jaji aliyeteuliwa na unayemshtaki, halafu eti unasubiria haki, hivi kuamini hilo kama linaweza kutokea, ni kwa sababu tumekuwa wajinga, wapumb.avu au wendawazimu? HIVI KUNA UKOLONI UNAOZIDI HUU?
Ukitizama kwa umakini, unaona dhahiri kuwa, Tanzania tulipigania kuwa huru kutoka kwenye ukoloni wa mwingereza ili tuwe kwenye ukoloni na utumwa wa weusi wenzetu, hata kama utakuwa mbaya zaidi kuliko hata ule wa mtu mweupe.
Leo kila kitu, ni Rais. Haulizwi, hashtakiwi, yupo juu ya sheria. Kwenye mazingira haya si afadhali hata gavana wa Kiingereza ambaye alikuwa anaweza kuhojiwa hata na malkia? Tuliutafuta uhuru au kongwa na utumwa wa kwetu wenyewe?
Wala hawakukubali kuyapitia magumu yote hayo ili wabadilishiwe mtu wa kuwanyima uhuru, yaani badala ya mzungu awe mweusi au wa kijani.
Watanzania, wazazi wao baada ya kuhangaikia uhuru. Uhuru huu ilimaanisha kuwa na maamuzi ya waongozwe namna gani, viongozi wapatikane kwa matakwa yao, maisha yao ya kila siku yamriwe na wao wenyewe, wajichagulie wanaowataka kuwaongoza, wapande taratibu za kupata haki zao pale miongoni mwao anapodhulumu, waweke utaratibu wa haki wa kuwatambua na kuwadhibiti wahalifu, n.k.
Kwa bahati mbaya, Watanzania, wamerudi kule kule kwenye ukoloni, tena ukoloni mbaya kuliko hata ule wa mzungu:
1) Mtanzania awe na kosa au hana kosa, polisi ana uwezo wa kumkamata, kumrundika ndani, na kwa kupitia DPP, anaweza kumfungulia mashtaka yoyote anayoyataka yeye, na mtuhumiwa akisota rumande hata miaka, huku polisi wakiendelea kusema uchunguzi unaendelea, bado haujakamilika. HIVI KUNA UKOLONI MBAYA KUUZIDI HUU?
2) Leo hii, mkuu wa Wilaya au Mkoa, anaweza kumwamuru Polisi amkamate raia yeyote kwenye eneo lake la uongozi na kumsweka ndani, hata kama sababu ni kwa sababu ya chuki za kugombania kimada. Utaswekwa ndani, akipenda, baada ya masaa 48, atamwamuru polisi akuachie. HIVI KUNA UKOLONI MBAYA KUUZIDI HUU?
3) Leo hii Rais akitaka anaweza kuwateulia watu wa kuja kuwatawala, mpende msipende, kuanzia mkoani mpaka wilayani (RC, RAS, RPC, DC, DAS, DED, OCD, n.k.). Wawe wana sifa za kuwa viongozi au hawana, iwe mnawataka au hamuwataki, mtataliwa kwa lazima. Hatukumchagua gavana, wala RC, wala DC, wakati wa ukoloni, je, leo tunawachagua? KUNA UKOLONI MBAYA ZAIDI YA HUU?
4) Leo hii, Rais anawateua majaji wote, Mwanashetia mkuu wa Serikali, jaji mkuu, jaji kiongozi, msajili wa mahakama, DPP, IGP, CDF, mkurugenzi wa TISS, n.k. Halafu unadanganywa kuwa eti unaweza kuishtaki serikali ila ili uishtaki, kwanza uombe kibali kwa serikali cha kuishtaki serikali. Na sisi tunaona ni sawa na inawezekana. Hivi kweli sisi tuna akili? Yaani unaenda mahakamani kabisa ukiwa na akili yako, kesi ipo chini ya jaji aliyeteuliwa na unayemshtaki, halafu eti unasubiria haki, hivi kuamini hilo kama linaweza kutokea, ni kwa sababu tumekuwa wajinga, wapumb.avu au wendawazimu? HIVI KUNA UKOLONI UNAOZIDI HUU?
Ukitizama kwa umakini, unaona dhahiri kuwa, Tanzania tulipigania kuwa huru kutoka kwenye ukoloni wa mwingereza ili tuwe kwenye ukoloni na utumwa wa weusi wenzetu, hata kama utakuwa mbaya zaidi kuliko hata ule wa mtu mweupe.
Leo kila kitu, ni Rais. Haulizwi, hashtakiwi, yupo juu ya sheria. Kwenye mazingira haya si afadhali hata gavana wa Kiingereza ambaye alikuwa anaweza kuhojiwa hata na malkia? Tuliutafuta uhuru au kongwa na utumwa wa kwetu wenyewe?
wakiwa na furaha kibao tofauti na huko walikopita kwa so called ndugu zao na kadhia walizokutana nazo