Upinzani unakufa au CCM kinakufa?

Upinzani unakufa au CCM kinakufa?

MAHANJU

JF-Expert Member
Joined
Aug 26, 2014
Posts
5,255
Reaction score
8,027
Hili ni swali ambalo kwa watu wenye akili nyepsi(Simple minds) hulipatia majibu ya haraka haraka bila kufikiri kwa kina, wazungu hunena kwa usemi usemao " Simple minds discuss people" yaani akili nyepesi huishia akizungumza watu, kwa kiswahili huitwa ni majungu!

Kwa watu wenye akili thabiti huongelea matukio( Complex minds discuss events) yaani hapa kwa akili nyepesi unaweza kufikiri kwauda huu mfupi ambao Rais mteule Ndg Mafuli ameingia madarakani kuamua kufumua fumua Yale ambayo miaka yote hua hayapendi ndo kunaweza kuleta sura mpya ya Chama cha mapinduzi, hapa watu walipaswa waangaliie matukio zaidi na sio kuishia kulijadili jina la Magufuli muda wote! Hapa sio kuifufua CCM pekee!

Ikumbukwe kwamba Rais huyu anayo mitihani mikubwa sana ndani na nje ya chama chake kwani anajua siku zote "kikulacho ki-nguoni mwako" Hapa la kutazamwa kubwa ni kwamba wengi wanaomzungumza kwa wema ni wale wamaccm wa ukweli pamoja walio nje ya CCM! hawa ndio friends of Magufuli wa kweli.

Magufuli kukamilisha ahadi zake alizoahidi kwa Wananchi ni lazima akubaliane na baadhi ya mambo ambayo upinzani imekua ukiyalilia siku zote na ambayo kimsingi wale CCM kindaki (CCM maslahi) hawayataki tena kwa bahati mbaya sana CCM kindaki ndaki si watu wadogo hata kidogo!Tena ni wale ambao baadhi yao ameshaanza kuona ngozi na Rangi zao kwenye matukio yake haya ambayo Wananchi wanayashangilia.

Faida kubwa kwa upinzani ni pale Magufuli kapoamua kuwasikilaza zaidi wananchi kwa kujali maslahi ya taifa zaidi kuliko ya kichama, hapa itambidi sasa atekeleze baadhi ya mambo ambayo upinzani umekua ukiyalilia miaka yote na CCM kindaki ndaki hawataki kuyasikia hata kidogo. Mfano hili suala la kuwazuia viongozi wa nchi kusafiri nje ya nchi na kuwazuia wabunge kua wajumbe wa bodi liwaumiza zaidi wamaccm wengi kuliko ilivyotegemewa, haijawahi kutokea ndani ya awamu zote za utawala chini ya CCM akatokea mtu wa kulipigia hili jambo kelele zaidi ya upinzani,hapa Magufuli amewachoma baadhi ya watu.

Upinzani sasa unapata nguvu sasa hata ya kuwaambia wamaccm tena kwa kujiamini ni kwanini haya miaka yote wamekua wakiyafumbia macho? Magufuli atakapozidi kutumbua majipu mengi zaidi ndiko kunapowapa wapinzani nafasi ya kutengeneza hoja nyingi zaidi kuendelea kuibua mazito zaidi ambayo hata kwa hakika Magufuli atawaunga mkono kwa maslahi mapana ya taifa. Hii hali ya kuona Magufuli anaenda pamoja na matakwa ya wapinzani inaweza kuleta migongano na hatimaye migawanyiko mingi ndani ya CCM.


Kwa vyovyote vile endapo Magufuli atasikiliza na kuzingatia zaidi maagizo ya chama chake hataweza kuendana na kasi yake anayoitaka maana atafungwa na minyororo ya chama chake na kuanza kushindwa kutekeleza Yale aliyoyaahi kwa watanzania na hali kurudi kule kule alikotoka Mtangulizi wake! hapa itaanza ninong'ono mingi kama ilivyokua kwa Mtangulizi wake na kuwapa wapinzani nguvu ya kujipanga zaidi.


Pamoja na baadhi ya wapinzani kusifu juhudi za Magufuli sio kwamba wao hawapendi kuongoza laahasha! Katika kipindi ambacho CCM wanatakiwa kujipanga kuliko hata nyuma ni hiki maana kwa haya anayoyafanya Magufuli wapinzani wako makini sana kufuatilia nyendo zake mguu kwa mguu kutafuta madhaifu yake ili baadaye wapate cha kuwaambia Wananchi, pia hiki ni kipindi ambacho CCM wanaweza kubweteka kutokana na Magufuli kuaminiwa na wananchi wakidhani atakua Rais milele.

CCM wanachofikiri zaidi kwa sasa ni kua kasi ya Magufuli ndiyo itakayoua upinzani huku wao wakiweka mikono mifukoni, wanasahau kwa sasa ndio kipindi hasa ambacho wapinzani wako field kujiimarisha zaidi kutafuta mwarobaini wa CCM! Inawezekana kabisa kwa sasa anayezungumzwa zaidi ni Magufuli kuliko CCM, wamesahau kua CCM ni taasisi yenye mfumo wake,utendaji ndani ya Chama pia unahitaji mtu kama Magufuli, kama kuna kitu kibaya CCM wanataka kukijaribu ndani ya chama wasimpe Magufuli uenyeketi wa chama taifa! Anatakiwa apewe nafasi ndani ya Chama apewe rungu aibue na madudu mengine huko.

Kwa akili ya mtu anayefikiria kwa kutumia "Complex mind" kwa kuangalia matukio hawezi kusema sasa ni muda wa upinzani unakufa! Ikumbukwe kua kuna viongozi wa upinzani nchini ambao wanapata mafunzo ya kuviendesha vyama kutoka vyama washirika vya nchi ambazo upinzani umekomaa na umeongoza dola mara nyingi, hapa wanafundishwa hata namna ya kumaintain siasa za ushindani hasa pale kunapokua na changamoto kubwa ya ushindani.
 
UPINZANI chali, chali kabisa, Ndembendembe , kifo cha Mende.
 
Upinzani ss haturudi nyuma bali tunalisongesha.. mwenye akili fupi ndo anawaza kuwa tutakufa....
 
Mara ya kwanza walisema ccm imesimamisha wagombea wawili wa urais,yaani magufuli ccm A na lowassa ni ccm B,ila nimegunduwa kwamba kumbe magufuli alikuwa mgombea wa UKAWA aliyenadiwa na ccm,asanteni ccm kwa kumpa promo magu mkidhani ni mwenzenu
 
mara ya kwanza walisema ccm imesimamisha wagombea wawili wa urais,yaani magufuli ccm a na lowassa ni ccm b,ila nimegunduwa kwamba kumbe magufuli alikuwa mgombea wa ukawa aliyenadiwa na ccm,asanteni ccm kwa kumpa promo magu mkidhani ni mwenzenu

mkuu, linaweza kuwa na ukweli hili??
 
Khaa!! Kumbe kuna watu bado wanawaza kuhusu CCM/UKAWA bado?? Tafuteni kazi za kweli mfanye bana mnatia aibu sana..
 
Ccm inafanya rebranding.. Inakuwa mpya ya wananchi haswa wa hali ya chini. Kitendo tu cha wapinzani kuona Magufuli anasimamia maslahi ya wananchi na wananchi kumuona ndio mkombozi wao ni pigo kwa wapinzani. Siku Magufuli akikabidhiwa rasmi uenyekiti wa ccm ndio mtaelewa pale ambapo nchi yote itakimbilia ccm na ukawa kubaki wakiwa wa milele.
 
Tunawashuukuru sana akina Mbowe na wapinzani wengine. Ndio walioleta mabadiliko tunayoyaona sasa. CCM unayoiona na kuisikia sasa ingekuwepo bila harakati za wana CHADEMA na CUF? labda dhana hii ndiyo aliyosema mleta mada hapo juu.....Simple minds.......... hawawezi kuliona hili! CCM imebadilishwa na vyama vya upinzani. Ni vyama vya upinzani ndivyo vimepiga sana kelele za ufisadi, uzembe na kutokuwajibika kwa waliopo madarakani; mambo anayopambana nayo JPM kwa sasa! Hata vyama vya upinzani vinashukuru kupata Rais ambaye yuko katika kambi yao... yaani anatekeleza kwa vitendo hoja na sera zao. Huyu jamaa hatekelezi sera za CCM!
 
Ukawa walipo hamishia kinyesi chumbani!that was the end!
 
CCM ya Nyerere= CCM ya Magufuri. UKAWA yaa Leo = Ukiwa. UKAWA halisi rudisha Slaa,Lipumba na ZZK ondoa ELN,Kingunge na Sumaye. Chama kipya kusanya Change,Tibaijuk,Rostam,ELN,Kingunge,Sumaye na Riz. Tunataka Tz safi.
 
Kiukweli upinzani nchi hii umeleta mageuzi, Makelele ya upinzani juu ya udhaifu mkubwa wa serikali ya chama cha tawala ndio umemfanya JPM kufanya kila jambo ambalo litawanufaisha wanannchi.
 
Hili ni swali ambalo kwa watu wenye akili nyepsi(Simple minds) hulipatia majibu ya haraka haraka bila kufikiri kwa kina, wazungu hunena kwa usemi usemao " Simple minds discuss people" yaani akili nyepesi huishia akizungumza watu, kwa kiswahili huitwa ni majungu!

Kwa watu wenye akili thabiti huongelea matukio( Complex minds discuss events) yaani hapa kwa akili nyepesi unaweza kufikiri kwauda huu mfupi ambao Rais mteule Ndg Mafuli ameingia madarakani kuamua kufumua fumua Yale ambayo miaka yote hua hayapendi ndo kunaweza kuleta sura mpya ya Chama cha mapinduzi, hapa watu walipaswa waangaliie matukio zaidi na sio kuishia kulijadili jina la Magufuli muda wote! Hapa sio kuifufua CCM pekee!

Ikumbukwe kwamba Rais huyu anayo mitihani mikubwa sana ndani na nje ya chama chake kwani anajua siku zote "kikulacho ki-nguoni mwako" Hapa la kutazamwa kubwa ni kwamba wengi wanaomzungumza kwa wema ni wale wamaccm wa ukweli pamoja walio nje ya CCM! hawa ndio friends of Magufuli wa kweli.

Magufuli kukamilisha ahadi zake alizoahidi kwa Wananchi ni lazima akubaliane na baadhi ya mambo ambayo upinzani imekua ukiyalilia siku zote na ambayo kimsingi wale CCM kindaki (CCM maslahi) hawayataki tena kwa bahati mbaya sana CCM kindaki ndaki si watu wadogo hata kidogo!Tena ni wale ambao baadhi yao ameshaanza kuona ngozi na Rangi zao kwenye matukio yake haya ambayo Wananchi wanayashangilia.

Faida kubwa kwa upinzani ni pale Magufuli kapoamua kuwasikilaza zaidi wananchi kwa kujali maslahi ya taifa zaidi kuliko ya kichama, hapa itambidi sasa atekeleze baadhi ya mambo ambayo upinzani umekua ukiyalilia miaka yote na CCM kindaki ndaki hawataki kuyasikia hata kidogo. Mfano hili suala la kuwazuia viongozi wa nchi kusafiri nje ya nchi na kuwazuia wabunge kua wajumbe wa bodi liwaumiza zaidi wamaccm wengi kuliko ilivyotegemewa, haijawahi kutokea ndani ya awamu zote za utawala chini ya CCM akatokea mtu wa kulipigia hili jambo kelele zaidi ya upinzani,hapa Magufuli amewachoma baadhi ya watu.

Upinzani sasa unapata nguvu sasa hata ya kuwaambia wamaccm tena kwa kujiamini ni kwanini haya miaka yote wamekua wakiyafumbia macho? Magufuli atakapozidi kutumbua majipu mengi zaidi ndiko kunapowapa wapinzani nafasi ya kutengeneza hoja nyingi zaidi kuendelea kuibua mazito zaidi ambayo hata kwa hakika Magufuli atawaunga mkono kwa maslahi mapana ya taifa. Hii hali ya kuona Magufuli anaenda pamoja na matakwa ya wapinzani inaweza kuleta migongano na hatimaye migawanyiko mingi ndani ya CCM.


Kwa vyovyote vile endapo Magufuli atasikiliza na kuzingatia zaidi maagizo ya chama chake hataweza kuendana na kasi yake anayoitaka maana atafungwa na minyororo ya chama chake na kuanza kushindwa kutekeleza Yale aliyoyaahi kwa watanzania na hali kurudi kule kule alikotoka Mtangulizi wake! hapa itaanza ninong'ono mingi kama ilivyokua kwa Mtangulizi wake na kuwapa wapinzani nguvu ya kujipanga zaidi.


Pamoja na baadhi ya wapinzani kusifu juhudi za Magufuli sio kwamba wao hawapendi kuongoza laahasha! Katika kipindi ambacho CCM wanatakiwa kujipanga kuliko hata nyuma ni hiki maana kwa haya anayoyafanya Magufuli wapinzani wako makini sana kufuatilia nyendo zake mguu kwa mguu kutafuta madhaifu yake ili baadaye wapate cha kuwaambia Wananchi, pia hiki ni kipindi ambacho CCM wanaweza kubweteka kutokana na Magufuli kuaminiwa na wananchi wakidhani atakua Rais milele.

CCM wanachofikiri zaidi kwa sasa ni kua kasi ya Magufuli ndiyo itakayoua upinzani huku wao wakiweka mikono mifukoni, wanasahau kwa sasa ndio kipindi hasa ambacho wapinzani wako field kujiimarisha zaidi kutafuta mwarobaini wa CCM! Inawezekana kabisa kwa sasa anayezungumzwa zaidi ni Magufuli kuliko CCM, wamesahau kua CCM ni taasisi yenye mfumo wake,utendaji ndani ya Chama pia unahitaji mtu kama Magufuli, kama kuna kitu kibaya CCM wanataka kukijaribu ndani ya chama wasimpe Magufuli uenyeketi wa chama taifa! Anatakiwa apewe nafasi ndani ya Chama apewe rungu aibue na madudu mengine huko.

Kwa akili ya mtu anayefikiria kwa kutumia "Complex mind" kwa kuangalia matukio hawezi kusema sasa ni muda wa upinzani unakufa! Ikumbukwe kua kuna viongozi wa upinzani nchini ambao wanapata mafunzo ya kuviendesha vyama kutoka vyama washirika vya nchi ambazo upinzani umekomaa na umeongoza dola mara nyingi, hapa wanafundishwa hata namna ya kumaintain siasa za ushindani hasa pale kunapokua na changamoto kubwa ya ushindani.

Inakufa ccm
 
CCM ya Nyerere= CCM ya Magufuri. UKAWA yaa Leo = Ukiwa. UKAWA halisi rudisha Slaa,Lipumba na ZZK ondoa ELN,Kingunge na Sumaye. Chama kipya kusanya Change,Tibaijuk,Rostam,ELN,Kingunge,Sumaye na Riz. Tunataka Tz safi.

Wewe ni kilaza mkuu
 
Ccm inafanya rebranding.. Inakuwa mpya ya wananchi haswa wa hali ya chini. Kitendo tu cha wapinzani kuona Magufuli anasimamia maslahi ya wananchi na wananchi kumuona ndio mkombozi wao ni pigo kwa wapinzani. Siku Magufuli akikabidhiwa rasmi uenyekiti wa ccm ndio mtaelewa pale ambapo nchi yote itakimbilia ccm na ukawa kubaki wakiwa wa milele.

Utasubiri sana kwa hilo kutokea.
Mimi pro-UKAWA na nafurahia sana majipu kutumbuliwa.
Hata hivyo nikiwa hai 2020, kura ZANGU huyo MAKUFULI atazisikia tu UKAWA.
 
Ninaamini Magufuli akikaza buti ccm itakufa.Kwa sababu hakuna aliye msafi. Hakuna ambaye ni salama mpaka sasa. Naikumbuka vita ya sokoine (RIP)na wahujumu uchumi,ilikuwa ni nchi nzima wahujumu waliwekwa ndani lakini.........
 
Sijui akili yangu ila naona kama reform ya wachina namna walivyojirekebisha na mambo yakaendelea sasa wanaosema maigizo wacha tusubiri ila kwa maoni yangu ccm itaimarika watakao umia ni wale mapapa yaliozoea kwiba yaani ni mabunifu ya namna ya kwiba na kukifanya chama kichokwe na raia.
 
Siwaelewi! Mnafurahia au mnasikitika? Kwani alipokuwa akipita akinadi M4C "Magufuli For Change" mlijua ni mabadiliko ya kuvaa mashati? Msipojitahidi kuwa na Ajenda mbadala mtaishia kudandia tu kama Kawaida yenu.
 
Ninaamini Magufuli akikaza buti ccm itakufa.Kwa sababu hakuna aliye msafi. Hakuna ambaye ni salama mpaka sasa. Naikumbuka vita ya sokoine (RIP)na wahujumu uchumi,ilikuwa ni nchi nzima wahujumu waliwekwa ndani lakini.........
 
Duh, kazi kweli kweli. ILA Ni ukweli uliowazi kabisa kwamba pamoja na kwamba Magufuli WA CCM yupo ikulu lakini anafanya kazi 100% kwa kufuata sera za Ukawa. Ukawa tuna kila sababu ya kutembea kifua mbele kwa sababu sisi ndo washindi.
Mbali ya Hilo, bila kitimtim cha timu nzims ya kamanda Mbowe CCM wasingekuwa na Magufuri kama rais.
Nathubutu kusema upinzani umaimaarika wakati CCM kikipoteza mwelekeo.
 
Mara ya kwanza walisema ccm imesimamisha wagombea wawili wa urais,yaani magufuli ccm A na lowassa ni ccm B,ila nimegunduwa kwamba kumbe magufuli alikuwa mgombea wa UKAWA aliyenadiwa na ccm,asanteni ccm kwa kumpa promo magu mkidhani ni mwenzenu

Kwahiyo ukawa mlikataa kuutambua ushindi wa mwana ukawa mwenzenu.....!!!!!
 
Back
Top Bottom