Upinzani au UKAWA dhidi ya chama tawala

Upinzani au UKAWA dhidi ya chama tawala

Deliver

Member
Joined
Apr 17, 2014
Posts
61
Reaction score
17
Habarini wana jamvi nimekua mfuatiliaji sana wa mada za humu ndani mada nyingi ni kuuponda uongozi uliopo si vibaya kila kitu kina faida na hasara hata wewe pale nyumbani kwako kuna mambo kadhaa ambayo umekosea mengine umefanya vizuri.

Nirudi kwenye mada yangu au swali langu ukikaa ukatafakari hivi upinzani ukipewa nchi wana kikosi gan cha kutuongoza sababu nyadhifa nyingi zipo kisiasa wataweza kuitawala nchi kwa ufanisi?

Maana kwa kuona kwangu nchi nyingi upinzani ulipo kiangusha chama tawala ni kutokana na kumeguka kwa chama tawala upinzani ukapata watu makini waliotoka chama tawala ila kwa Tanzania bado chama tawala hakijameguka hivyo kwa fikira zangu ndogo naona upinzani Tanzania bado kwa sababu zifuatazo:

Kwanza viongozi wengi wa upinzani wana njaa wasitudanganye wakipata nchi hawatabadilisha chochote bali watajiweka sawa kwanza kiuchumi.

Pili hawana timu makini ya kutuongoza wote naona wababe,Elimu za kawaida na maneno mengi yasio na maana sana hata ukiwasikiliza.

Tatu hawana uzoefu wa kuongoza nchi maana hamna kiongozi wao aliewahi kua hata waziri utaongozaje nchi haujawahi kuingia baraza la mawaziri inamaana ukiingia ikulu inabidi ujifunza kwanza.

Rai yangu kuona upinzani unakazana kuongeza wabunge ila uraisi bado.
 
Nyerere alipokabidhiwa nchi 1961 uzoefu name team ya kuongoza nchi Vilitoka wapi. Nchi haiongozi na wanasiasa tu Bali wataalam ndio went .Hakuna chuo cha kusomea uwaziri wala urais.. kit kitaenda vizuri.Tanzania Vila ya CCM @ kit kinawezekana.
 
Tumia ubongo wako zaidi ya hapo! Nyerere alipoanza alikuwa na timu kubwa yenye uzoefu mkubwa kiasi gani? Nchi haikuwa na wasomi wala wataalamu wa fani karibu zote lakini alitawala miaka yote ile na kuinua nchi ki vile. Angalia UKAWA kwa makini. Unaweza kupata mawaziri wote wenye sifa zote na kubaki. Wataalamu wasio wanasiasa wapo na mabadiliko ya kisiasa hayawahusu. Mfumo wa kisiasa uliopo sio wa kukarabati bali ni kuufumua na kusuka upya. Ni wakati wa Upinzani kupewa nafasi ya kufanya kazi hiyo.
 
mleta thread nakupinga hapo uliposema kwa ufahamu wako mdogo ,,, issue ni kwamba hata huo mdogo huana kabsa
 
Wanajamvi msishangae bado madhara ya division 5 lazima yaonekane
 
Nyerere alipokabidhiwa nchi 1961 uzoefu name team ya kuongoza nchi Vilitoka wapi. Nchi haiongozi na wanasiasa tu Bali wataalam ndio went .Hakuna chuo cha kusomea uwaziri wala urais.. kit kitaenda vizuri.Tanzania Vila ya CCM @ kit kinawezekana.

Hahaha! Nyerere hakuanzia U-rais moja kwa moja. Alipitia level ya Uwaziri Mkuu Kiranja wa walio wengi (2 September 1960- 1May 1961) na Waziri Mkuu kamili (1 May 1961-22 January 1962) akiwa chini ya Malkia Elizabeth II ambaye aliwakilishwa na Gavana Sir Richard Gordon Turnball ambaye alikuwa Gavana wa kumi na wa mwisho Tanganyika ( 1958-1961) japo aliendelea mpaka 1962 kwa nafasi ya Gavana Mkuu (Governor-General of Tanganyika).

Hii inaonyesha Nyerere alipata uzoefu kabla hajawa Rais wa Tanganyika mnamo tarehe 9 December 1962. Uongozi wa juu hasa wa mabadiliko makubwa haya, haupingiki kupata uzoefu ama kuwa na mzoefu kundini! Tofauti na hapo, nchi inaweza kuyumba kutokana na kiongozi kuyumbishwa.
 
Back
Top Bottom