nani kasema chadema itasambaratika?Kwa wanachedema,
Umakini zaidi unahitajika kuongoza chama wakati huu mgumu na tete. Mgongano wa mawazo kati ya Zitto, Mbowe na hata kundi la wanachama wapya waliojiunga chama hivi karibuni ni lazima litazamwe kwa makini. Ni demokrasia kugonganisha mawazo lakini ni vizuri tukatumia vizuri kuepusha mianya ya sumu kupenyezwa. Chadema ni tumaini la wengi na Survival yake inategemea jinsi itakavyoweza kupambana na kumeneji tofauti kati ya makundi na chaguzi za ndani. Ikipita kwenye changuzi za ndani salama na kuwa na safu safi kama mwaka huu mipango ya wapinzani wenu itakuwa mashakani.
Mungu aiepushe na migawanjiko inayoweza kuwagonganisha. Chaguzi za ndani ya chadema ni sehemu muhimu kwa watu wenye nia mbaya kuwasambaratisha.
Mungu ibariki Tanzania!
For sure ni hivyo!CHADEMA is only going to get stronger from here on out.
Hata kama kuna wanaojiingiza kwa siri chadema wakiwemo wanafki wa usalama wa taifa (ccm). Amabao wengi wao wamejichokea kimaisha na wanahaha kila mahali kupata habari za umbea kuhusu chadema ili wakivuruge chama hawataweza maana wazalendo wa kweli ni hao ambao tayari tunao na wanahimiza mabadiliko siku zote wababaishaji wasiotulia hawana nafasi IMANI KUBWA IMEONYESHWA NA WANANCHI IHESHIMIWE NA CHADEMA KWA MASILAHI YA TAIFA.
Kama huna kadi ya CHADEMA wewe si mwanachama, sasa utahama vipi wakati hujawahi kuwa? Hata hivyo siyo ujasiri wala busara kuhama mara unapokabiliwa na changamoto. Kama NCCR ni poa kama unavyosema kwa nini usiende huko mara moja. Weka wazi kama wewe ni mkimbizi kutoka CCM.kiukweli wengi tulispaoti chadema but hatuna kadi za chama so ikiyumba tutahamia pangine mbona NCCR hipo poa tu? na siasa safi? so far tunagalia yupi anaeleweka kaka but ccm wameshindwaaa
For sure ni hivyo!
Lakini tahadhari ni muhimu sana kabla ya ajali!...uzoefu unaonyesha kwamba kwa vyama vinavyofanya vizuri kama hiki, huwa pia ni kichaka cha migogoro, kwahiyo tusitegemee mema tu, tuweke precautions na measures za kukabiliana na lolote!
Pamoja na majukumu yao ya kibunge kazi kubwa ya ziada ya wabunge wa CHADEMA (na vyama vingine vya upinzani) iwe kuhakikisha kwamba chama kinaota mizizi katika majimbo yao (na kuidhoofisha CCM) ili kiweze kuteka serikali za mitaa/vijiji katika chaguzi zijazo na kuhakikisha kuwa CCM haiwezi kuyapata tena majimbo yao katika uchaguzi mkuu wa 2015, iwe kwa mizengwe au bila mizengwe. Hii ina maana ya kuwa na muundo imara katika ngazi ya mashina na matawi (au vyovyote vile inavyojulikana ndani ya CHADEMA). CCM ilikuwa inapata kiburi kutokana na hiyo grassroots organisation ambayo sasa imeanza kubomoka. Pendekezo langu lingine ni kuwa Dr. Slaa asitafute nyadhifa zingine kama kukubali kuwa mbunge wa kuteuliwa na JK. Akae nje ya Bunge akijenge chama kwa kuimarisha sehemu ambako chama kina nguvu na kukipenyeza kule ambako kilikuwa akijawa na nguvu. Maaskari wake akina Zitto, Mnyika, Mdee, Mr.II, n.k. nao wapewe majukumu ya kukijenga chama majimboni mwao na hata sehemu zingine mbali na majimbo yao.Unajua CHADEMA ni chama kilichoweza kutoa mwelekeo mpya na tumaini la mabadiliko chanya. CCM walifanikiwa kusambaratisha upinzani ktk miaka ya 2000-2005 kwa kupandikiza mamluki kwenye upinzani na kisha kuwarudisha CCM kwa mbwembwe (Tambwe Hiza,Lamwai na wengine) hivyo kujenga picha kuwa wapinzani ni "wababaishaji" na "waroho" wa madaraka mbele ya wananchi, and that explains low number of opposition MPs in the previous parliament.
Lakini CHADEMA imefanya kazi kubwa kurudisha ima ya wananchi and i must say the future for CHADEMA is pretty shiny cos its demography expands rapidly especially among youth who are many in number, more energetic and can help the party now and in the future.
Cha muhimu ni uongozi kuwa dynamic na kuadopt to the growing numbers and challenges, kujikita katika mizizi na pia kuwekeza sehemu ambazo hakijapata umaarufu sana. Ni muhimu pia kwa chama kuwa bunifu na kujitofautisha na CCM na vyama vingine. The sky is the limit for CHADEMA if they play their cards right!