Unywaji wa kahawa unaweza kukukinga na magonjwa ya moyo

Dr Mathew Togolani Mndeme

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
201
809
tk
 

Attachments

  • Khawa.jpg
    Khawa.jpg
    82.1 KB · Views: 685
Wapo wanaosema kahawa Inamadhara, Wengine Kahawa ni safi.
Research zinazopingana na hayo unazungumziaje
 
  • Thanks
Reactions: BAK
mkuu .kidogo nikuulize nnchi nyingi zinatngeneza kahawa.kwa hivyo kuna makabila mengi ya kahawa.je kahawa ipi liyo pendekezwa kunywa?
 
Swali zuri kaka na ni kweli wengi wetu tumekua tukiamini au kuaminishwa kuwa unywaji wa kahawa una madhara. Hata hivyo kauli hizi zimekua za kukaririshwa zaidi kama imani bila scientific explanations. Binafsi sijakutana na utafiti mzuri unaoelezea madhara hivyo sitaweza kutoa maoni kama unavyonitaka. Kama unafahamu utafiti wa kisayansi unaoongelea madhara ya unywaji kahawa tafadhali nishirikishe
1500's headline: Coffee leads to illegal sex
1600's headline: Coffee cures alcoholism but causes impotence
1700's headline: Coffee helps you work longer
1800's headline: Coffee will make you go blind. Have a cup of hot wheat-bran drink instead
1916 headline: Coffee stunts your growth
1927 headline: Coffee will give you bad grades, kids
1970's and '80's headline: Coffee is as serious as a heart attack
Millennium headline: Coffee goes meta
2001 headline: Coffee increases risk of urinary tract cancer
2007 headline: Coffee decreases risk of liver cancer
2011 headline: Coffee reduces risk of stroke and prostate cancer
2012 headline: Coffee lowers risk of heart failure
2015 headline: Coffee is practically a health food

Mwalimu Mdeme Unazungumziaje hii Trend ya Utafiti katika Vipindi mbalimbali. Ingawa CNN walipokuwa wanaandika Habari hii waliishia kwa kusema Hawajui kesho Kitaibuka nini tena kuhusu Coffee na wenda kuna uwezekano wa kuwepo maoni tofauti hapo baadae.

Unazungumziaje Role ya CAFFEINE ambayo watu wanasema ni Addictive. Na wanasema kwa kiwango flani inasaidia kiafya (400mg ya Caffeine kulingana na US Department of agriculture). Huoni kwa sababu ni addictive hakuna mpaka wa kumzuia mnywaji kunywa zaidi na akapata dose kubwa ya CAFFEINE.

msaada zaidi.
 
Swali zuri kaka. Ni kweli tumekua tukiamiambiwa hivyo na kuaminishwa kuhusu madhara ya kahawa ingawa hatukua tunapata maelezo ya kisayansi ya kutosha (katika mazingira yetu ya kitanzania) na hivyo kuonekana kama ni jambo la kuaminishwa zaidi kuliko kuwa ni fact.

Ila ukisoma hii makala tuliyoandika utaona kwamba ulikuwepo ushahidi wa kisayansi ulioonesha kuna madhara kwenye unywaji wa kahawa tena uliofanywa na watu wengi. Lakini kama kawaida ya tafiti za kisayansi, huwa haziweki nukta zinapopata majibu fulani bali utafiti mmoja hushawishi tafiti nyingine zaidi kufanywa na ndio mana utaona tumesema kwamba kulikua na mknganyiko miongoni mwa wanasayansi. Tafiti za kisayansi sio static bali hukua na hubadilika kutokana na sababu nyingi kubwa ukiwa ni kuongezeaka kwa maarifa, kugunduliwa kwa methodolojia mpya na vifaa vya kufanyia utafiti, na mabadiliko mengine. Hivyoo ni sahihi kabisa kupata matokeo yanayokinzana kadiri muda unavyoendelea. Mwisho wa siku utafiti utaonesha kipi ni cha kweli zaidi kati ya majibu tofautitofauti yaliyotolewa an hicho huo ndio huwa ushahidi mpya wa kisayansi.

Kama utakumbuka, kwa kareni nyingi sana watu waliamini dunia ina umbo flat na baadaye wengine wakaja kuamini ina umbo la duara. Ila kadiri tafiti zilivyoendelea ilijulikana kwamba dunia ina umbo la tufe na ushahidi huo umedumu hadi sasa maana ulipata evidence ya kutosha.
Kwa dunia kuwa flat,Sphere sawa. Sasa hii kitu ambayo inamadhara (chanya au hasi kulingana na Utafiti husika) tunazungumzia mwili wa mwanadamu ambao Unazaliwa mara Moja na Kufa Mara Moja. Huoni ni bora kuachana na vitu ambavyo ni controversial kuliko kuwa na vitu ambayo leo au kesho utafiti unaweza kuibuka juu ya advancement of Technology Tukagundua tena Inamadhara au ni Bora zaidi. Tunapataje ujasiri wa kuingiza kwenye miili yetu vitu ambavyo kumbe hata tusingevitumia kutokana na utata wake bado tusingepoteza kitu maana kuna vitu mbadala maelfu visivyo na utata na vikitumiwa kama vyakula/vinywaji vinaweza visilete utata.
 
Aisee kahawa nazani ina watu na watu binafsi nikinywa Kahawa au Milinda Nyeusi lazima mapigo ya Moyo yaende mbio hata kama nimekunywa ni kwa uchache tu.
 
Asante mwalimu kwa maelezo yako ya kukusanya tafiti za watafiti wengine, nilitegemea ungetuletea tafiti zako binafsi ukatueleza wewe au nyie mmewatafiti wanywaji wangapi, kwa muda gani na matokeo yakawaje. Hata hivyo nitaendelea kunywa kahawa mpaka serikali itakapopiga marufuku kama ile ya viroba.
 
mimi nikinywa kahawa moyo huenda mbio na hata nikienda short call, ni harufu ya kahawa tu....what's wrong with me?
 
MImi nadhani kuwa addictive sio issue ya kahawa tu. Addictive ni tatizo kwa kitu chochote kile na ndio mana ni muhim sana kuwa na KIASI. Kuna watu ni addictive hata wa cvyakula vya kawaida tu (kula ovyo, kula kila saa, kula chakula kingi sana, nk) hapata madhara. Hata Sukari tunayoipenda sana kwenye kila kitu ikiwa addictive ina madhara ya kiafya tena makubwa sana.
Samahani mwalimu Mdeme, Usichoke ukiona maswali mengi ujue nataka kujifunza vitu, maana sisi walalahoi mtaani tunawaamini nyie wataalamu zaidi ya wanasiasa.
Addiction iko proportional na Dopamine Release.
Hapa kwa harakaharaka ili kuweka kachangamoto kidogo nimepitia hii Scientific Source Caffeine gives cocaine an addictive boost kujaribu kujustfy kuwa Hata ukinywa kidogo, Kitendo cha Caffeine kuwepo kinaongeza uwezekano wa kunywa zaidi kuliko kinywaji ambacho hakina. Kuna jamaa namfahamu yuko addicted kiasi kwamba amebandika offisini kwake "NO Coffee No Job".

When animals receive cocaine repeatedly over a period of days, their initial running response will intensify. This early sensitization process can contribute to future addiction. When rats got cocaine and caffeine together, they ran more, and this effect sensitized, meaning that over several days, they ran farther and farther, much more than with cocaine alone. The effect also happened faster. Cocaine sensitization usually takes five days, but with caffeine added in, it took only three. The scientists published their findings May 14 in The American Journal on Addictions.

Hapo juu ni para moja katika hayo maelezo, Inaonyesha CAFFEINE inaboost addiction. Kwa hiyo hoja yangu mkuu ni unaposema Vikombe viwili vitatu vyafaa wakati ndani ya hicho kinywaji kunaelements(Caffeine) ambazo Zitachochea Dopamine Release ili kuongeza uhitaji zaidi.

Naomba maelezo kidogo mkuu. Usione nakomaa sana ila mimi ni miongoni mwa watu wasiotumia kabisa kahawa na huwa naamini niko sahihi, tafiti muhimu kama hizi huwa napenda kuhoji Squarely ili nielimike vya kutosha.
Msingi wa hoja yangu mkuu ni kwamba, sioni kama ni sawa kulinganisha CAFFENETED FOODS/DRINKS na Vyakula visivyokuwa na Caffeine katika Addiction. Chochote kiinaweza kusababisha addiction lakini Chenye (Addiction Booster yaan Caffeine) kitakuchochea zaidi hivyo kujikuta Unatumia kiwango zaidi cha Caffeine ambacho Utarudi palepale kwenye madhara kama kweli yapo.
 
Kaka nashukuru sana kwa maswali haya ya msingi. Hapa niwe mkweli na muwazi kwamba hata mimi unanisaidia kuongeza ufahamu. Pili niweke sawa tu kwamba mimi sio mtaalamu wa lishe, afya, wala medicine hiyo ufahamu wangu wa hii mada uko limited kisayansi kwa kuwa sio maeneo yangu ya ubobezi. Afya ninakutana nayo katika hybridization ya TEHAMA na afya ambazo ndiko nilipo..tena afya kwa upande wa public health zaidi. Kwa kusema hivyo sina ujasiri wa kujibu kila hoja nisije nikapotosha. Ukitazama utafiti huu tuliocomment nature yake ni evidence zaidi kuliko utaalamu wa afya na ndio mana nimeshiriki kuuongelea.

Ila ulichokiongea kuhusu caffeine na cocaine kuwa addictive booster kina ukweli. Ukichunguza vema hata mtoto akinywa kiasi fulani cha sodaya coke utaona kabisa anabadilika na kuwa more active na agressive pia.. na anataka kuendelea kunywa tu bila kujali tumbo linajaa...hahahaa. Nadhani hamu inachochewa na contents.

Lakini labda nikuulize swali, hivi ukiwa hujalamba kabisa asali na ukiwa unelamba, ni wakati gani ushaiwishi wa kulamba unakua nao? Je, ni kabala ya kulamba kabisa au ni baada ya kulamba kwa mara ya kwanza?

Swali langu ni je, addictive booster haiwezi kuwepo pia kwenye aina nyingine ya vyakula kwa mtindo mwingine?

NB: Ngoja nimuombe Dr Ndosi niliyeandika naye ajibu swali lako kitalaamu zaidi maana yeye afya ni uwanja wa nyumbani.
Mkuu nakupata hata mimi sio mtu wa mambo hayo na nimewahi kuwa mwanafunzi wako baadhi ya courses (IS) nadhani.
Nitafurahi kushibishwa maarifa zaidi. Nadhani hata swali uliloniuliza liko nje ya upeo wangu, labda mtaalamu zaidi anaweza kueleza au Dr. Ila changamoto nilizotoa ni katika kuperuzi huku na kule..
 
kiukweli mi nikinywa kahawa mapigo ya moyo ghafla yanabadirika aiseee ila naipenda sana lakini sasa ndo ivo mapigo ya moyo yameipenda zaid
 
Kaka, haya ndio majibu ya Dr. Mwidimi Ndossi kwa ulichouliza:

" Sayansi haina majibu ya ujumla ujumla kihivyo. (Naendelea kiingereza maana Kiswahili kinanishinda. ) the research process addresses a specific question and after collecting relvant data and analysing them, they suggest an explanation for the observation, which will answer the specific question asked.

In our article above, we have described the benefits of coffee in prevention of cardiac diseases – in fact the consensus is 3-4 cups a day and this has been shown in other chronic diseases and some cancers. The observations give the highest level of evidence available and with that amount of data, one can be confident that all the small variations shown in other small studies are now accounted for in these large meta-analyses. This is the power of meta-analyses as opposed to single primary studies.

You should remember that coffee is a normal human beverage but not a normal food for rats. So whereas in humans we are explaining the benefits of coffee, for rats, a cup of coffee or tea may be a strong drug. Rats don’t drink coffee for breakfast! Therefore those small studies conducted in rats in highly artificial conditions do not have any power to explain or being extrapolated to what happens to human beings living in the real world.

We have explained the relationship between coffee and cardiovascular diseases, meaning that habitual drinking of coffee is cardio-protective. Coffee drinking that is excessive i.e. over and above normal drinking do not carry those benefits. Actually benefits gained start to be lost between 5-10 cups per day. The evidence shows to have cardiac problems with coffee you have to start drinking over 10 cups per day! That could happen in case of addiction or just for someone who has just had many meetings in the day J. Addiction is a disease and one can be addicted to many things even reading sms on your phone and I think an addiction is another huge subject needing a discussion thread of its own.

Despite the benefits explained above, we did not mean that coffee is good for everything. For example, coffee may not be good for drinking in the evening when you want to have a good night sleep (most people are affected, though not all).

The mistake that many people do when they talk about coffee, they think coffee=caffeine. Coffee is food and it has more ingredients than just caffeine and if you speak to food scientists they will tell you all that is contained in coffee. All we are saying and educating the public here is that coffee is not bad for your health, especially when it comes to your cardiovascular health, coffee is cardio-protective.

"
Asante kwa mwangaza mkuu.
Ila nimetatizwa na hitimisho la Dr maana maelezo ya ndani yanazungumzia Limited amount of Coffee, pia yameenda mbali kabisa kueleza hadi ni wakati gani inaweza kuwa na effects kwa mtumiaji japo sio wote(kunywa jioni). Ingekuwa vizuri kama hitimisho nalo lingekuwa specific sio general kama All we are saying and educating the public here is that coffee is not bad for your health, especially when it comes to your cardiovascular health, coffee is cardio-protective.

Kwa hapa nashukuru mkuu, kwa maelezo mazuri sana, na Pongezi nyingine zimuendee Dr. Nitajaribu kupitia zaidi hizo link kweye bandiko pale juu na kama kutakuwa na hitaji lolote la maelezo sitasita kuhitaji ufafanuzi kutoka kwenu mkuu maana nyie ndio uwanja wenu wa Tafiti, na bila tafiti hakuna maendeleo.
Shukrani...
 
Kwa nini utegemee kusikia utafiti niliofanya mimi mwenye kwenye hili? Ndio ingekufanya ukubali kilichosemwa au unamaanisha nini? Jua tu kwamba, any academic/scientific enterprise is subjected to and finds its ways within " a body of knowledge": which is a some sort of scientific understanding universally agreed within a given field of specialization. Scientists have one thing in common which might be different from politics or something else: they respect any scientific work as long as it proves to remain objective, systematic, and specific to its subject matter. Kama kila mwanasayansi anatakiwa arudie utafiti yeye mwenyewe ndio awe na "voice" ya kuongelea matokeo yake, huoni kama hiyo itageuka kua chaos?

BTW: In academic world, the best practice is to present your knowledge and/or arguments by dialogistically engaging in a conversation that involves the suggestions/views of others. Kama una uelewa wa kutosha kuhusu tafiti, utaelewa kwamba, as of per the existing knowledge, there is no a sound and scientifically convincing evidence than a meta-analysis study. One should have a very strong and rational counterargument to question its finding, hence the need of an alternative scientific undertaking. Na hiki ndicho kilichoko kwenye study ya kina Choi

MM

Mwalimu sisi wengi tunajifunza kupitia worldwideweb, I expect when I google about coffee analysis then your name will be among those scientists so that I can refer it to someone else, naamini upo hapa JF kutuelimisha kuhusu ugunduzi wako kwa mfano kama ni analysis tu you can google it and you will find plenty of material to study, I need your research and analysis which have been presented in colleges and universities so that I can be proud of my Tanzanian brother and scientist:

Coffee and cancer risk: A meta-analysis of prospective observational studies
 
Back
Top Bottom