"Unikumbushe nikupe hela yako"

"Unikumbushe nikupe hela yako"

haszu

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2017
Posts
1,477
Reaction score
3,541
Amekufata mwenyewe umkopeshe halafu unakutana nae anakwambia hivyo, wewe utamjibu nini ?
 
Waswahili wanasema uungwana vitendo. HUyo ndugu hajawa muungwana kwa hilo. Kumkumbusha ama kutokumkumbusha kutategemea na ukubwa wa deni lenyewe, Kama ni haya madeni yetu ya kishkaji 20k,60k nk Nitakaa kimya akiamua kulipa sawa asipolipa amejifungia milango siku za mbeleni.
 
Mlete huku Morogoro kwenye Lori!
 
Waswahili wanasema uungwana vitendo. HUyo ndugu hajawa muungwana kwa hilo. Kumkumbusha ama kutokumkumbusha kutategemea na ukubwa wa deni lenyewe, Kama ni haya madeni yetu ya kishkaji 20k,60k nk Nitakaa kimya akiamua kulipa sawa asipolipa amejifungia milango siku za mbeleni.
K60? Kishikaji?
 
Amekufata mwenyewe umkopeshe halafu unakutana nae anakwambia hivyo, wewe utamjibu nini ?
Haisee mm nitamkumbusha, then atanipa ela yang pia haitaishia hapo nitamkopa kiasi cha fedha alaf na mm nalipiza mara mbl ya usumbufu
 
"Unikumbushe nikupe hela yako" maana yake anayo hiyo hela tayari. Either ipo kwenye sim (mpesa, tigo pesa nk) or anategemea kuipata muda si mrefu (Siku hiyo hiyo) sasa ni uungwana kumkumbusha wala si dharau.
.
Kuna wakati natoka na hela ya mtu nyumbani ili nikamlipe tukikutana kazini. Najikuta nimerudi nayo ndio nakumbuka heee mbona sijampa. Sasa ili nisisahau nampigia simu namwambia kilichotokea na kumwomba kesho anikumbushe ili niweze mpatia.
 
K60? Kishikaji?
Kwa jamaa zangu wanaoshinda nami kila siku katika magumu na mepesi ni zaidi ya kishkaji hii, Ila ikitokea imekua hali kama mtoa mada alivyotanabaisha basi atakua amejifungia milango siku nyingine. Nami nikikwama pia nitashindwa kumkopa sababu atahisi nataka nijilipe deni langu kupitia malngo wa pili.
 
Ili jambo uweze kulikumbuka lazima uwe na interest nalo. Mf. Ukikutana na mtu kwenye basi ambaye hutegemei kukutana naye tena akakutajia jina lake, huwezi kulikumbuka siku nyingine. Tofauti na ukikutana na boss kwenye semina akakwambia usijali shida yako ya ajira nitaitatua nikirudi ofisini, huwezi kusahau jina lake. Hivyo hivyo mkopo sio jambo la kufurahisha unapolipa so huna interest nalo si rahisi uweke kwenye kumbukumbu zako.
 
Back
Top Bottom