Unafiki wa imani:Bora hata wanyama wasio na dini wala kumjua mungu kuliko sisi wanadamu

Salary Slip

Platinum Member
Apr 3, 2012
49,324
152,136
Binadamu ni kiumbe mnafiki sana katika mambo mengi ila unafiki wa kiwango cha juu uko katika imani zetu za kidini na pengine katika siasa.Hata hivyo, leo hii nitaongelea zaidi unafiki katika imani zetu.

Wanadamu wa leo wengi wetu tunasali kama fashion tu na zaidi tunasali kwa mazoea lakini miyoni mwetu hatuna mungu bali ni wanafiki wakubwa ingawa wapo wachache wanaoheshimu imani zao.

Wakristo na Makanisa:Mtu yuko kanisani Ibada inaendelea yeye yuko busy na simu.Ibada inaendelea yeye akili haipo kanisani anawaza yake anangoja tu muda wa ibada uishe arudi zake nyumbani ilimradi tu naye leo ameonekana kuwa amefika kanisani!

Watu,wake kwa waume,baada ya ibada ndio wanapata nafasi ya kupeana namba za simu,kupanga appointment wakafanye yao.Mtu anatoka kusali akifika nyumbani kwake anakwenda kumnyanyasa mwanae wa kambo au yatima.Hawa ndio waumini wa leo ambao ukigusa imani yake atatamani akukate na shoka lakini matendo yake ni bora hata ya mpagani au mnyama.

Siku hizi makanisani michango imetamalaki na hata sadaka zimepoteza maana.Mtu anahubiri hukuu watu wanatoka mbele mmoja mmoja na kukambidhi mchungaji hela eti hii ndio sadaka au huku eti ndio kumtolea mungu!

Yanoyohubiriwa makanisani mwetu siku hizi sijui hata kama baadhi yako katika kitabu kitakatifu cha Biblia.Siku hizi kila mtu ni Mchungaji na kila mtu anajiita Nabii!Hakuna biashara inayolipa kama kuanzisha huduma za kiroho!

Baadhi ya waimba kwaya wamegeuza makanisa wanayofanyia mazoezi ya kwaya kama meeting place za kupanga appointment zao na kufanya wanayoyajua wao.

Kwa kifupi huyu ndio mkiristo wa leo ambae ukigusa imani yake iwe hapa mtandaoni au kwingineko atatokwa na povu utadhani anataka kukata roho lakini matendo yake bora hata ya ibilisi!

Waislamu na Misiki:Hawa nao wana yao ikiwemo kuzingatia swala tano.Utamkuta mtu anazingatia swala tano lakini matendo yake bora hata ya mpagani.

Mtu yuko busy na swala tano lakini mtu huyo ni mchoyo,mbinafsi,mpiga majungu,mshirikina na wakati mwingine hata kutupia wengine majini na mapepo!

Hawa waheshimiwa ikifika kipindi cha Ramadhani wanajitahidi kweli kuzingatia wanayopaswa kuyafanya lakini ngoja mfungo uishe utadhani ndio wameruhusiwa kufanya yao.

Swali ambalo huwa najiuliza ni hivi wao kuzingatia maagizo ya mwenyezi mungu ni wakati tu wa kipindi cha Mwezi Mtukufu au ni wakati wote wa maisha yao?

Hawa waheshimiwa wakati mwingine hutumia hata imani ya dini yao kudhuru wengine wakiaminiwa wako sahihi kufanya hivyo katika mazingira fulani.Kwa mfano kujilipua, n.k.Kuna mahali Mungu ameturuhusu kutoa uhai wa wengine kwa kutumia jina lake?!

Yako mengi sana ambayo binadamu huyu anaejifanya kuumia sana pale imani yake inapoguswa lakini kumbe ni binadamu huyu huyu ambae matendo yake ni mabaya na maovu kupindukia.

Kwa mfano, hapa JF ikiletwa mada ikawa na element za udini,basi watu watajifanya kutetea imani zao na kujionyesha wanaumizwa sana pale imani yake inapoguswa lakini ni binadamu huyu huyu anaetenda mambo mabaya na maovu kinyume kabisa na imani yake pasipo hata kushituka.

Hapa hapa JF,kama ilivyo huku mutaani,kuna watu kutukana na kukejeli kwa sio tatizo ila ni hao hao wanaojidai wao ni wacha mungu na wako kutetea imani yao ili hali matendo na dhamira zao ni za hovyo kabisa!

Binadamu wengi wa leo(sio wote) tunaenda misikitini na makanisani kusali kama fashion tu na zaidi ili tuonkane tunasali lakini miyoni mwetu hatuna mungu na ndio maana utakut mtu anatoka kanisani au msikiti anapita guest au masaa machache baada ya ibada anaenda kusaliti ndoa yake kwasabubu mtu huyu alikwenda kusali kama kutimiza wajibu tu lakini sio kwenda kusali kwa maana halisi ya kusali.

Mimi nasema bora hata wapagani kuliko sisi wenye dini tunaojaribu kumdanganya mungu kumbe tunajidanganya wenyewe.

Angalieni wanasiasa hawa wanaoapa kwa kutumia Biblia au Msahafu mienendo na matendo yao baada ya kuingia madarakani ndio ujue kuwa imani hizi leo hii tumezigeuza kuwa ni fashion tu ambayo kila mtu anajaribu kwenda nayo ili asionekane yuko nyuma(amepitwa na wakati).

Ni bora hawa wanyama wasio mjua mungu kuliko sisi binadamu tuliojaa unafiki mbele ya macho ya mwenyezi mungu.

Kwa mlionikejeli katika ule uzi mwingine wa "wanaosajili Jumuiya na wacheza pool" msomeni na Baba Askofu hapa itawasaidia maana in yale yale tu niliyokuwa nawajibu katika comment zangu huku mkinilaani na kunitolea lugha chafu.

Mokiwa-28Machi2016.png

Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa
Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa, ametaja majipu 10 yaliyoko makanisani na kuwataka Watanzania kujisafisha kwa kuacha mambo yasiyompendeza Mungu, ikiwamo migogoro ndani ya makanisa.


Askofu Mokiwa amesema ndani ya makanisa kuna mawe makubwa aliyoyafananisha na majipu ambayo hata Yesu Kristo anasononeshwa nayo.

Hayo aliyasema jana katika ibada ya Pasaka iliyoadhimishwa kitaifa katika Kanisa la Mtakatifu Albano, Upanga jijini Dar es Salaam.
Askofu Mokiwa alitaja jipu la kwanza kuwa ni uwapo wa mashindano makanisani, huku akisema siku hizi makanisa yanashindana kwa kuangalia kanisa lipi kubwa kuliko lingine na kanisa linamiliki shule ngapi.

Alisema: "Ushindani wa kanisa gani ni kubwa kuliko lingine, kanisa gani lina mali kuliko lingine, askofu anayeongoza kanisa fulani ni kabila fulani, na kanisa gani lina waumini wengi kuliko lingine na kanisa gani lina vituo vingi vya kulelea watoto yatima kuliko lingine.

“Imefika wakati sasa makanisa yajitathmini na kuanza kupunguza kuzungumza mambo ya nje ya kijamii na badala yake waelekezane uovu unaopatikana ndani ya makanisa,” alisema.

Jipu lingine alilitaja kuwa ni maaskofu kupigana vita. Alisema kuna tabia ya askofu mmoja kumchimba askofu mwingine, kupanga mapinduzi dhidi ya askofu mwenzake, pamoja kutukanana.

Alisema kuna tabia ya askofu kuacha eneo lake na kuingia katika eneo la askofu mwingine na kusababisha misuguano.

Jipu lingine alisema ni mapinduzi ndani ya makanisa, kuwa kuna ugumu wa moyo na kusalimiana kwa badhi ya waumini wa makanisa na kwamba waumini siku hizi wanasemana na kusingiziana, hivyo kumekuwapo kwa uongo ndani ya taasisi hizo ambazo dhima yake ni kuleta amani na furaha miongoni mwa waumuni.

Askofu Mokiwa alitaja tatizo lingine kuwa ni chuki baina ya waumini, huku watu wakiwa hawasalimiani na hawapendani, jambo ambalo hata askofu anapojaribu kuwaita na kuwapatanisha, wanakimbia kwa kutoa udhuru.

Alisema jipu lingine ni uwapo wa nguvu ya pesa kanisani au nguvu ya mtu ndani ya kanisa, ambayo inasababisha kuvurugika kwa kanisa.

Askofu Mokiwa alisema: "Kuna watu makanisani wanatumia pesa kwa manufaa yao wenyewe. Mbona hujitolei kusaidia watoto yatima? Mbona hujitolei kuwasaidi kikundi cha uinjilisti kwenda kuhubiri? Watu wa namna hiyo wana lengo la kuvunja amani."
Alitaja jipu lingine kuwa ni wizi na ulaghai na kwamba katika makanisa kuna ulaghai uliokithiri.

Jipu lingine alisema kuwa ni uwapo wa roho ya uchochezi kwa baadhi ya waumini makanisani, huku pia akitaja uwapo wa injili za kibiashara kwa baadhi ya makanisa kutumia injili kujiingizia kipato kwa kufanya miujiza.

Askofu Mokiwa alisema jipu lingine ni uwapo wa wivu na uzushi ndani ya makanisa.

“Siku hizi hayo mambo yanaitwa majipu ambayo yanasababisha kanisa kushindwa kuendelea, wakristo wanashindwa kumwona Mungu kwa sababu kuna watu waliotofauti ndani ya makanisa,” alisema Mokiwa.

MAKONDA: ATAKAYEOMBA ULINZI KANISANI KUSWEKWA NDANI
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika ibada hiyo aliliomba kanisa kumsaidia kutimiza wajibu wake kwa kunyoosha mienendo ya waumini wake, huku akitumia nafasi hiyo kusisitiza agizo lake la kuwataka wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhakiki silaha zao ndani ya siku 90.

“Kuanzia Julai Mosi, mwaka huu mimi mwenyewe nitaongoza msako wa kukagua silaha ambazo hazijahakikiwa. Sitakuwa na huruma, wala sitamwangalia mtu usoni,” alisema Makonda.

Makonda alisema kwa sasa jiji la Dar es Salaam haliko salama kutokana uwapo wa silaha ambazo hazieleweki.

Aliwaomba waumini wa Kikristo, ambao jana walikuwa wanaadhimisha Sikukuu ya Pasaka, kujitolea kuchangia maendeleo ya mkoa ikiwa ni pamoja na kumaliza tatizo la madawati.

“Juzi kuna mama mmoja Kimara, ni kiongozi wa kanisa, anasema kuna shughuli kanisani, anaomba ulinzi. Nikamuuliza wa nini, akasema unajua huku kuna rushwa. Nikashangaa kusikia eti kanisani napo kuna rushwa, hadi leo siamini. Sasa nasema yeyote atakayepiga simu kuomba ulinzi wa polisi kanisani namweka ndani,” alisema Makonda.

CHANZO: NIPASHE
 
mungu akupe utulivu, umenena vyema sana. hawa wanadin bana n wazinzi, waongo, wanafik, wachoyo, wachawi, wabinafsi, wapenda majungu, matapeli, wezi, wanawivu na wachonganish kabsa n wachache sana ambao wanasali/kuswali kiukwel. ila hugeuka mbogo din zao zikiguswa wako radhi wakuue
 
Nimesoma kwa makini andiko lako mkuu.
Iko hoja ya msingi, nami naunga mkono kuwa ni kwa sehemu ndogo sana dini na waumini wake tunaenenda kwa mujibu wa maandiko ya imani zetu.
Ila nataka kusahiisha kidogo. Usiseme heri wapagani kuliko waumini wa dini, kusema hivyo ni kutaka kutuaminisha kuwa Mungu si wa mhimu kutafutwa na kuabudiwa.

Kitu unachosahau ni kuwa hakuna dini itakayomsaidia mwanadamu kuishinda dhambi.

Dini ni jitihada za binadamu kumjua Mungu na jinsi ya kumuabudu.
Ki historia dini bado zimeshindwa kutoa suruhisho la mwadamu kuishinda dhambi.

Dini ya kweli ni hii kumpenda Mungu kwa moyo wako wote, akiri zako zote, na kwa nguvu zako zote na ya pili inafanana na hiyo

Mpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.

Changamoto ni kuzitimiza amri hizo ktk mwili huu wenye dhambi na ubinafsi mkubwa.

Na hapa ndo Yesu alidhihilishwa ili kutuokoa na kutupa ushindi kwa njia ya Roho wake wa uzima ili tuweze kumwabudu ktk roho na kweli.

Sasa usichanganye dini na wokovu wa Mungu.

Kumbuka Yesu alidhihirishwa ili awakomboe wadhambi ambao ni mimi na wewe hivyo kwa wale wanaoupokea wokovu na kuifahamu kweli wanapata faida ktk maisha ya sasa na badae ktk uzima wa milele.
Ila wanaozani dini ni fashion hao hatuitaji kuwafariji, ni watoto wa shetani na jehanamu nimahala pao pa milele.

Walioitwa ni wengi bali wateule ni wachache.

Ndg usife moyo, endelea mbele katu usirudi nyuma ktk imani.
Atakaevumilia mpaka mwisho ndiye atakae OKOKA.
 
mungu akupe utulivu, umenena vyema sana. hawa wanadin bana n wazinzi, waongo, wanafik, wachoyo, wachawi, wabinafsi, wapenda majungu, matapeli, wezi, wanawivu na wachonganish kabsa n wachache sana ambao wanasali/kuswali kiukwel. ila hugeuka mbogo din zao zikiguswa wako radhi wakuue
Ni wanafiki sana hawa watu!
 
Binadamu ni kiumbe mnafiki sana katika mambo mengi ila unafiki wa kiwango cha juu uko katika imani zetu za kidini na pengine katika siasa.Hata hivyo, leo hii nitaongelea zaidi unafiki katika imani zetu.

Wanadamu wa leo wengi wetu tunasali kama fashion tu na zaidi tunasali kwa mazoea lakini miyoni mwetu hatuna mungu bali ni wanafiki wakubwa ingawa wapo wachache wanaoheshimu imani zao.

Wakristo na Makanisa:Mtu yuko kanisani Ibada inaendelea yeye yuko busy na simu.Ibada inaendelea yeye akili haipo kanisani anawaza yake anangoja tu muda wa ibada uishe arudi zake nyumbani ilimradi tu naye leo ameonekana kuwa amefika kanisani!

Watu,wake kwa waume,baada ya ibada ndio wanapata nafasi ya kupeana namba za simu,kupanga appointment wakafanye yao.Mtu anatoka kusali akifika nyumbani kwake anakwenda kumnyanyasa mwanae wa kambo au yatima.Hawa ndio waumini wa leo ambao ukigusa imani yake atatamani akukate na shoka lakini matendo yake ni bora hata ya mpagani au mnyama.

Siku hizi makanisani michango imetamalaki na hata sadaka zimepoteza maana.Mtu anahubiri hukuu watu wanatoka mbele mmoja mmoja na kukambidhi mchungaji hela eti hii ndio sadaka au huku eti ndio kumtolea mungu!

Yanoyohubiriwa makanisani mwetu siku hizi sijui hata kama baadhi yako katika kitabu kitakatifu cha Biblia.Siku hizi kila mtu ni Mchungaji na kila mtu anajiita Nabii!Hakuna biashara inayolipa kama kuanzisha huduma za kiroho!

Baadhi ya waimba kwaya wamegeuza makanisa wanayofanyia mazoezi ya kwaya kama meeting place za kupanga appointment zao na kufanya wanayoyajua wao.

Kwa kifupi huyu ndio mkiristo wa leo ambae ukigusa imani yake iwe hapa mtandaoni au kwingineko atatokwa na povu utadhani anataka kukata roho lakini matendo yake bora hata ya ibilisi!

Waislamu na Misiki:Hawa nao wana yao ikiwemo kuzingatia swala tano.Utamkuta mtu anazingatia swala tano lakini matendo yake bora hata ya mpagani.

Mtu yuko busy na swala tano lakini mtu huyo ni mchoyo,mbinafsi,mpiga majungu,mshirikina na wakati mwingine hata kutupia wengine majini na mapepo!

Hawa waheshimiwa ikifika kipindi cha Ramadhani wanajitahidi kweli kuzingatia wanayopaswa kuyafanya lakini ngoja mfungo uishe utadhani ndio wameruhusiwa kufanya yao.

Swali ambalo huwa najiuliza ni hivi wao kuzingatia maagizo ya mwenyezi mungu ni wakati tu wa kipindi cha Mwezi Mtukufu au ni wakati wote wa maisha yao?

Hawa waheshimiwa wakati mwingine hutumia hata imani ya dini yao kudhuru wengine wakiaminiwa wako sahihi kufanya hivyo katika mazingira fulani.Kwa mfano kujilipua, n.k.Kuna mahali Mungu ameturuhusu kutoa uhai wa wengine kwa kutumia jina lake?!

Yako mengi sana ambayo binadamu huyu anaejifanya kuumia sana pale imani yake inapoguswa lakini kumbe ni binadamu huyu huyu ambae matendo yake ni mabaya na maovu kupindukia.

Kwa mfano, hapa JF ikiletwa mada ikawa na element za udini,basi watu watajifanya kutetea imani zao na kujionyesha wanaumizwa sana pale imani yake inapoguswa lakini ni binadamu huyu huyu anaetenda mambo mabaya na maovu kinyume kabisa na imani yake pasipo hata kushituka.

Hapa hapa JF,kama ilivyo huku mutaani,kuna watu kutukana na kukejeli kwa sio tatizo ila ni hao hao wanaojidai wao ni wacha mungu na wako kutetea imani yao ili hali matendo na dhamira zao ni za hovyo kabisa!

Binadamu wengi wa leo(sio wote) tunaenda misikitini na makanisani kusali kama fashion tu na zaidi ili tuonkane tunasali lakini miyoni mwetu hatuna mungu na ndio maana utakut mtu anatoka kanisani au msikiti anapita guest au masaa machache baada ya ibada anaenda kusaliti ndoa yake kwasabubu mtu huyu alikwenda kusali kama kutimiza wajibu tu lakini sio kwenda kusali kwa maana halisi ya kusali.

Mimi nasema bora hata wapagani kuliko sisi wenye dini tunaojaribu kumdanganya mungu kumbe tunajidanganya wenyewe.

Angalieni wanasiasa hawa wanaoapa kwa kutumia Biblia au Msahafu mienendo na matendo yao baada ya kuingia madarakani ndio ujue kuwa imani hizi leo hii tumezigeuza kuwa ni fashion tu ambayo kila mtu anajaribu kwenda nayo ili asionekane yuko nyuma(amepitwa na wakati).

Ni bora hawa wanyama wasio mjua mungu kuliko sisi binadamu tuliojaa unafiki mbele ya macho ya mwenyezi mungu.
Mungu anawapenda watu wa namna hii. Nabii yeremia aliwaambia ndugu zake ukweli kwamba wakirudi misri watauliwa,watateswa na watoto wao watakuwa watumwa. Wao ndio waliomuomba akamuulize Mungu waende au wasiende lkn jibu lilipokja wakamgeuzia kibao. Watu wa aina yako huchukiwa sana makanisani sio tu na waumini bali na viongozi wote. Hii haibatilishi ukweli wa Mungu na Kutufanya tuone upagani ni Bora. STICK TO PRINCIPLES, Tusikatetamaa eti kwa kuwa watu wamekengeuka. Hii yote ilitabiriwa. Endelea kutuonya nani ajuae Maana Mungu huwaheshimu na Kuwapenda pamoja na kuwalinda watu wa aina yako maana ni wachache.
 
Mungu anawapenda watu wa namna hii. Nabii yeremia aliwaambia ndugu zake ukweli kwamba wakirudi misri watauliwa,watateswa na watoto wao watakuwa watumwa. Wao ndio waliomuomba akamuulize Mungu waende au wasiende lkn jibu lilipokja wakamgeuzia kibao. Watu wa aina yako huchukiwa sana makanisani sio tu na waumini bali na viongozi wote. Hii haibatilishi ukweli wa Mungu na Kutufanya tuone upagani ni Bora. STICK TO PRINCIPLES, Tusikatetamaa eti kwa kuwa watu wamekengeuka. Hii yote ilitabiriwa. Endelea kutuonya nani ajuae Maana Mungu huwaheshimu na Kuwapenda pamoja na kuwalinda watu wa aina yako maana ni wachache.
Ndugu asante sana na ubarikiwe.
 
Binadamu ni kiumbe mnafiki sana katika mambo mengi ila unafiki wa kiwango cha juu uko katika imani zetu za kidini na pengine katika siasa.Hata hivyo, leo hii nitaongelea zaidi unafiki katika imani zetu.

Wanadamu wa leo wengi wetu tunasali kama fashion tu na zaidi tunasali kwa mazoea lakini miyoni mwetu hatuna mungu bali ni wanafiki wakubwa ingawa wapo wachache wanaoheshimu imani zao.

Wakristo na Makanisa:Mtu yuko kanisani Ibada inaendelea yeye yuko busy na simu.Ibada inaendelea yeye akili haipo kanisani anawaza yake anangoja tu muda wa ibada uishe arudi zake nyumbani ilimradi tu naye leo ameonekana kuwa amefika kanisani!

Watu,wake kwa waume,baada ya ibada ndio wanapata nafasi ya kupeana namba za simu,kupanga appointment wakafanye yao.Mtu anatoka kusali akifika nyumbani kwake anakwenda kumnyanyasa mwanae wa kambo au yatima.Hawa ndio waumini wa leo ambao ukigusa imani yake atatamani akukate na shoka lakini matendo yake ni bora hata ya mpagani au mnyama.

Siku hizi makanisani michango imetamalaki na hata sadaka zimepoteza maana.Mtu anahubiri hukuu watu wanatoka mbele mmoja mmoja na kukambidhi mchungaji hela eti hii ndio sadaka au huku eti ndio kumtolea mungu!

Yanoyohubiriwa makanisani mwetu siku hizi sijui hata kama baadhi yako katika kitabu kitakatifu cha Biblia.Siku hizi kila mtu ni Mchungaji na kila mtu anajiita Nabii!Hakuna biashara inayolipa kama kuanzisha huduma za kiroho!

Baadhi ya waimba kwaya wamegeuza makanisa wanayofanyia mazoezi ya kwaya kama meeting place za kupanga appointment zao na kufanya wanayoyajua wao.

Kwa kifupi huyu ndio mkiristo wa leo ambae ukigusa imani yake iwe hapa mtandaoni au kwingineko atatokwa na povu utadhani anataka kukata roho lakini matendo yake bora hata ya ibilisi!

Waislamu na Misiki:Hawa nao wana yao ikiwemo kuzingatia swala tano.Utamkuta mtu anazingatia swala tano lakini matendo yake bora hata ya mpagani.

Mtu yuko busy na swala tano lakini mtu huyo ni mchoyo,mbinafsi,mpiga majungu,mshirikina na wakati mwingine hata kutupia wengine majini na mapepo!

Hawa waheshimiwa ikifika kipindi cha Ramadhani wanajitahidi kweli kuzingatia wanayopaswa kuyafanya lakini ngoja mfungo uishe utadhani ndio wameruhusiwa kufanya yao.

Swali ambalo huwa najiuliza ni hivi wao kuzingatia maagizo ya mwenyezi mungu ni wakati tu wa kipindi cha Mwezi Mtukufu au ni wakati wote wa maisha yao?

Hawa waheshimiwa wakati mwingine hutumia hata imani ya dini yao kudhuru wengine wakiaminiwa wako sahihi kufanya hivyo katika mazingira fulani.Kwa mfano kujilipua, n.k.Kuna mahali Mungu ameturuhusu kutoa uhai wa wengine kwa kutumia jina lake?!

Yako mengi sana ambayo binadamu huyu anaejifanya kuumia sana pale imani yake inapoguswa lakini kumbe ni binadamu huyu huyu ambae matendo yake ni mabaya na maovu kupindukia.

Kwa mfano, hapa JF ikiletwa mada ikawa na element za udini,basi watu watajifanya kutetea imani zao na kujionyesha wanaumizwa sana pale imani yake inapoguswa lakini ni binadamu huyu huyu anaetenda mambo mabaya na maovu kinyume kabisa na imani yake pasipo hata kushituka.

Hapa hapa JF,kama ilivyo huku mutaani,kuna watu kutukana na kukejeli kwa sio tatizo ila ni hao hao wanaojidai wao ni wacha mungu na wako kutetea imani yao ili hali matendo na dhamira zao ni za hovyo kabisa!

Binadamu wengi wa leo(sio wote) tunaenda misikitini na makanisani kusali kama fashion tu na zaidi ili tuonkane tunasali lakini miyoni mwetu hatuna mungu na ndio maana utakut mtu anatoka kanisani au msikiti anapita guest au masaa machache baada ya ibada anaenda kusaliti ndoa yake kwasabubu mtu huyu alikwenda kusali kama kutimiza wajibu tu lakini sio kwenda kusali kwa maana halisi ya kusali.

Mimi nasema bora hata wapagani kuliko sisi wenye dini tunaojaribu kumdanganya mungu kumbe tunajidanganya wenyewe.

Angalieni wanasiasa hawa wanaoapa kwa kutumia Biblia au Msahafu mienendo na matendo yao baada ya kuingia madarakani ndio ujue kuwa imani hizi leo hii tumezigeuza kuwa ni fashion tu ambayo kila mtu anajaribu kwenda nayo ili asionekane yuko nyuma(amepitwa na wakati).

Ni bora hawa wanyama wasio mjua mungu kuliko sisi binadamu tuliojaa unafiki mbele ya macho ya mwenyezi mungu.

Kwa mlionikejeli katika ule uzi mwingine wa "wanaosajili Jumuiya na wacheza pool" msomeni na Baba Askofu hapa itawasaidia maana in yale yale tu niliyokuwa nawajibu katika comment zangu huku mkinilaani na kunitolea lugha chafu.

Mokiwa-28Machi2016.png

Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa
Askofu wa Kanisa la Anglikana, Dayosisi ya Dar es Salaam, Dk. Valentino Mokiwa, ametaja majipu 10 yaliyoko makanisani na kuwataka Watanzania kujisafisha kwa kuacha mambo yasiyompendeza Mungu, ikiwamo migogoro ndani ya makanisa.


Askofu Mokiwa amesema ndani ya makanisa kuna mawe makubwa aliyoyafananisha na majipu ambayo hata Yesu Kristo anasononeshwa nayo.

Hayo aliyasema jana katika ibada ya Pasaka iliyoadhimishwa kitaifa katika Kanisa la Mtakatifu Albano, Upanga jijini Dar es Salaam.
Askofu Mokiwa alitaja jipu la kwanza kuwa ni uwapo wa mashindano makanisani, huku akisema siku hizi makanisa yanashindana kwa kuangalia kanisa lipi kubwa kuliko lingine na kanisa linamiliki shule ngapi.

Alisema: "Ushindani wa kanisa gani ni kubwa kuliko lingine, kanisa gani lina mali kuliko lingine, askofu anayeongoza kanisa fulani ni kabila fulani, na kanisa gani lina waumini wengi kuliko lingine na kanisa gani lina vituo vingi vya kulelea watoto yatima kuliko lingine.

“Imefika wakati sasa makanisa yajitathmini na kuanza kupunguza kuzungumza mambo ya nje ya kijamii na badala yake waelekezane uovu unaopatikana ndani ya makanisa,” alisema.

Jipu lingine alilitaja kuwa ni maaskofu kupigana vita. Alisema kuna tabia ya askofu mmoja kumchimba askofu mwingine, kupanga mapinduzi dhidi ya askofu mwenzake, pamoja kutukanana.

Alisema kuna tabia ya askofu kuacha eneo lake na kuingia katika eneo la askofu mwingine na kusababisha misuguano.

Jipu lingine alisema ni mapinduzi ndani ya makanisa, kuwa kuna ugumu wa moyo na kusalimiana kwa badhi ya waumini wa makanisa na kwamba waumini siku hizi wanasemana na kusingiziana, hivyo kumekuwapo kwa uongo ndani ya taasisi hizo ambazo dhima yake ni kuleta amani na furaha miongoni mwa waumuni.

Askofu Mokiwa alitaja tatizo lingine kuwa ni chuki baina ya waumini, huku watu wakiwa hawasalimiani na hawapendani, jambo ambalo hata askofu anapojaribu kuwaita na kuwapatanisha, wanakimbia kwa kutoa udhuru.

Alisema jipu lingine ni uwapo wa nguvu ya pesa kanisani au nguvu ya mtu ndani ya kanisa, ambayo inasababisha kuvurugika kwa kanisa.

Askofu Mokiwa alisema: "Kuna watu makanisani wanatumia pesa kwa manufaa yao wenyewe. Mbona hujitolei kusaidia watoto yatima? Mbona hujitolei kuwasaidi kikundi cha uinjilisti kwenda kuhubiri? Watu wa namna hiyo wana lengo la kuvunja amani."
Alitaja jipu lingine kuwa ni wizi na ulaghai na kwamba katika makanisa kuna ulaghai uliokithiri.

Jipu lingine alisema kuwa ni uwapo wa roho ya uchochezi kwa baadhi ya waumini makanisani, huku pia akitaja uwapo wa injili za kibiashara kwa baadhi ya makanisa kutumia injili kujiingizia kipato kwa kufanya miujiza.

Askofu Mokiwa alisema jipu lingine ni uwapo wa wivu na uzushi ndani ya makanisa.

“Siku hizi hayo mambo yanaitwa majipu ambayo yanasababisha kanisa kushindwa kuendelea, wakristo wanashindwa kumwona Mungu kwa sababu kuna watu waliotofauti ndani ya makanisa,” alisema Mokiwa.

MAKONDA: ATAKAYEOMBA ULINZI KANISANI KUSWEKWA NDANI
Naye Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda katika ibada hiyo aliliomba kanisa kumsaidia kutimiza wajibu wake kwa kunyoosha mienendo ya waumini wake, huku akitumia nafasi hiyo kusisitiza agizo lake la kuwataka wakazi wa Mkoa wa Dar es Salaam kuhakiki silaha zao ndani ya siku 90.

“Kuanzia Julai Mosi, mwaka huu mimi mwenyewe nitaongoza msako wa kukagua silaha ambazo hazijahakikiwa. Sitakuwa na huruma, wala sitamwangalia mtu usoni,” alisema Makonda.

Makonda alisema kwa sasa jiji la Dar es Salaam haliko salama kutokana uwapo wa silaha ambazo hazieleweki.

Aliwaomba waumini wa Kikristo, ambao jana walikuwa wanaadhimisha Sikukuu ya Pasaka, kujitolea kuchangia maendeleo ya mkoa ikiwa ni pamoja na kumaliza tatizo la madawati.

“Juzi kuna mama mmoja Kimara, ni kiongozi wa kanisa, anasema kuna shughuli kanisani, anaomba ulinzi. Nikamuuliza wa nini, akasema unajua huku kuna rushwa. Nikashangaa kusikia eti kanisani napo kuna rushwa, hadi leo siamini. Sasa nasema yeyote atakayepiga simu kuomba ulinzi wa polisi kanisani namweka ndani,” alisema Makonda.

CHANZO: NIPASHE
evansGREATDeal njoo umsome na Askofu maana Mimi niliongea upuuzi ila huyu Askofu kawasifia
 
evansGREATDeal njoo umsome na Askofu maana Mimi niliongea upuuzi ila huyu Askofu kawasifia
mkuu ukizungumzia kuwa mtu yupo kanisani anachati hayo ni mahusiano binafsi na MUNGU
:Mtu yuko kanisani Ibada inaendelea yeye yuko busy na simu.Ibada inaendelea yeye akili haipo kanisani anawaza yake anangoja tu muda wa ibada uishe arudi zake nyumbani ilimradi tu naye leo ameonekana kuwa amefika kanisani!

shida ni moja je kanisa husika mchungaji/viongoz misimamo yao ikoje???
kama mchungaji/viongoz hawajasimama vizur ktk misingi mizuri bas waumini watakuwa wahovyo na mambo ya ajabui,
washirika ni watu wanaenda kanisani kusali na kuishi kuishi ktk misingi ya neno la MUNGU iwapasayo,.......ni sawa na bible inasema
kumbukumbu la torati,...kuwa wanawake wasvae mavaz yampasayo mwanamume(suruali)ila baadhi ya makanisa wanaruhusu.,.....hii ni wachungaji baadh misimamo yao sio thabiti....kanisani kwetu ukiingia simu lazima uzime kuepusha vurugu na kutoa tension ya watu wengine simu itapoita,na suruali marufuku......

so mkuu swala la kuchati mtu akiwa church ni viongoz wa baadhi ya makanisa kuwa hawasimami ktk nafas zao................................
tunaendelea mkuu
 
evansGREATDeal njoo umsome na Askofu maana Mimi niliongea upuuzi ila huyu Askofu kawasifia
Siku hizi makanisani michango imetamalaki na hata sadaka zimepoteza maana.Mtu anahubiri hukuu watu wanatoka mbele mmoja mmoja na kukambidhi mchungaji hela eti hii ndio sadaka au huku eti ndio kumtolea mungu!

mkuu ni sahihi.......
ila bible inasema kuwa watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa......
Yesu alisema kuwa ukitoa sadaka hata mkono wako wa kushoto usijue umeshika kias gani........
so watu kwenda kumpa mchungaji pesa madhabuhuni na huku pesa ikiwa juujuu ili mtu ajionyeshe...
hii kibiblioa haipo.........
watu hawana maandiko mkuu thats why watu wanapoteaa.....nahii huja kwasababu watu hawana maarifa hawasomi bible/neno la MUNGU....ndomana watu wanadanganywa hovyo2..........
wakristo wa sikuhizi mtu tangu aokoke hajawi kusoma neno...unategemea mtu huyu atasimama???
never......Neno la MUNGU na lijae kwa wingi ndani yenu
ukisoma neno la MUNGU unajua misingi ya kuishi na MUNGU ikoje na kupotoshwa utakusikia2 au kuona kwa watu wengine wakipotoshwa....
Yesu alituambia kuwa hawa manabii wa uongo watakuja2......ila tutawatambua kwa matunda yao.......
so hao wanaodanganywa inamaana hawana neno la MUNGU ndomana wanapotoshwa.....
NB;sio manabii wote ni wa uongo ndomana tutawatambua kwa matunda yao
 
Juzi uli nikera kwasababu uli fananisha nawa cheza pool.lakinileo ume uleta ujumbe murwa kabisaaa! niukweli kwamba tuna cheza kamari na mungu lakini hatu shituki yakwamba mungu yeye katuli wala hatujibu.
 
Back
Top Bottom