Mantiki yake ni rahisi tu --- usitumie maji meeeeeeengI! Inadilute viasili na chembechembe mwilini, inaflashi out. Mbona anaeleweka?? Sema maelezo kaweka meeeeengi
Ahsante kwa somo Doctor, lakini mimi nadhani kunywa maji kwa kufuata formula ni sawa kabisa na inaepusha mtu kuzidisha kiwango cha maji,mfano mimi hapa uzito wangu ni 58 kg na kitaalamu wanasema ili kupata kiwango sahihi cha maji ambayo mtu anatakiwa kunywa ni unachukua uzito wako unagawanya kwa 30,hivyo kwa uzito wangu wa 58 kg nitatakiwa kunywa Lita 1.93 kwa siku kiwango ambacho nakiona ni sahihi sana,japo kuna wakati nazidisha unywaji wa maji,lakini pia kuna vitu ambavyo hupelekea kuzidisha kiwango cha maji,mfano mtu ambaye shughuli zake ni za juani ,huyu mtu hata afanye nini lazima kiwango cha utumiaji maji kizidi
Kwa mtu ambaye ana uzito wa kg 100 ukigawanya kwa 30 atambidi anywe Lita 3.3 za maji mbona hiki kiwango ni sahihi kabisa
Mwisho nasisitiza kuwa kunywa maji kwa kufuata kanuni ni vizuri ila kosa in pale mtu anakuambia kuwa kunywa maji mengi bila kukupa kanuni sahihi ya unywaji maji,matokeo yake unakuta mtu mwenye kilo 30 anakunywa maji Lita 5 huyu mtu lazima apate mgonjwa ya figo nk.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.