Hii sala inasaliwa nchi nzima kila siku na hasa hasa jumapili (na takribani watu milioni ishirini). Ukweli utajulikana!
SALA YA KUMUOMBA MUNGU AWAFICHUE WANAOPANGA MAOVU DHIDI YA WAKRISTO (NA RAIA WEMA WENGINE)
Bwana Yesu, Mfalme na Kiongozi wetu, uwe nasi katika safari yetu ya Imani. Sisi tunaosadiki, tunaamini katika ahadi zako. Wewe ulisema: Msifadhaike mioyoni mwenu. Mwamini Mungu niaminini nami pia Anayeniamini atafanya mambo makubwa ninayoyafanya mimi, naam atafanya hata makuu zaidi ..Na chochote mtakachoomba kwa jina langu nitafanya(Yn 14:1,12,13).
Tunakuomba uwafichue wale wote wanaopanga na kutekeleza uovu, ili kufikia malengo yao yasiyo na tija. Ukweli ujulikane. Ee Bwana, inuka ujitetee. Usikifedheheshe kiti cha Ufalme wako. Waliokuinukia walegee. Nasi kondoo wako ututunze. Kama mboni ya jicho lako utulinde. Ee Mungu wa Amani utusikie. Nasi tutalisifu jina lako milele. Amina.