Ukomo wa uongozi

Ukomo wa uongozi

kailakarama

Member
Joined
Aug 30, 2014
Posts
73
Reaction score
30
Wanachama wa Cuf,Cdm,NCCR na NLD wasema na wao karibuni watalipua makao makuu ya vyama vyao.

Kama wananchi wa Burkina Faso walivyolipua bunge kwa sababu ya kupitisha kifungu cha kumruhusu rais wao agombee kwa kipindi cha tano baada ya kuwa madarakani kwa miaka 27.

Na wanachama wa Cdm,Cuf,NCCR na NLD wanasema nao wamewachoka wafalme Mbowe,Lipumba,Mbatia na makaidi.

Nawashauri wasilipue ofisi zao bora waondoke huko na kujiunga na wazalendo wa ACT-Tanzania kwani katiba yetu Sura ya Sita Ibara ya 22 namba 2 vifungu vidogo vya (a),(b) na (c) vinasema ukomo wa uongozi ndani ya chama ni vipindi visivyozidi viwili vya miaka mitano.

Karibuni ACT-Tanzania
Taifa Kwanza leo na kesho.
 
Viongozi wa chadema shinyanga mjini wahamia ACT baada ya kuchoshwa na siasa za uzushi za chadema

Walio hamia ACT ni pamoja na Mwenyekiti wa kata ya kambarage ndugu Samwel dalla katibu muenezi kata Merchiory Tafuta, muhazini kata samuel raphael na kata ya chamaguha ni zacharia Samsoni mjumbe mkutano mkuu wilaya na dada misanya muhasibu wa tawi la kambarage
Pamoja na katibu wa solwa bwana Godwin Makomba a.k.a (shelembi mdogo).
 
Bora umetufafanulia kitu ambacho kilikua ni hisia za wengi kuwa kumbe ACT Tanzania, ni CCM B, na lengo la kuanzishwa kwenu ni kuisaidia CCM, kuviattack vyama vya upinzani ambavyo viko serious kutafuta, kuwakomboa wananchi wanyonge wanaokandamizwa na mfumo wa utawala wa CCM.

Inashangaza umewataja akina Mbowe,Lipumba, Mbatia na Makaidi kuwa wamekaa kwenye nafasi zao kwa muda mrefu.

Hata hivyo ukajifanya 'kusahau' namna Lyatonga Mrema alivyo 'Mfalme' ndani ya chama chake cha TLP!

Vivyo hivyo ukamsahau pia John Cheyo alivyo 'Sultani' kwenye chama chake cha UDP!

Vile vile ukajisahaulisha namna wabunge wa CCM walivyojigeuza 'Wafalme'. kupitia Rasimu ya Chenge na 'swaiba' wake Sitta, baada ya kuiondoa ibara iliyokuwemo kwenye Rasimu ya Tume ya Warioba, iliyobeba maoni ya wananchi ambao walisema ukomo wa kipindi cha ubumge kisizidi vipindi 3, na pale mbunge anapoboronga, wananchi ambao ndiyo Mwajiri wa mbunge, wawe na uwezo wa kumng'oa mbunge huyo aliyeshindwa kudeliver.

Ibara hiyo imenyofolewa, ili wabunge wa CCM wawe 'Wafalme' kwenye nafasi zao za ubunge,hadi hapo kifo kitakapowatenganisha na nafasi zao 'wanazozihusudu' sana za uheshimiwa ubunge!

Ukilinganisha hapo ni wanachama wapi hasa wanaostahili kuandamana hadi makao makuu ya vyama vyao ili kuwang'oa viongozi wao masultani, ni wanachama wa ukawa au wanachama wa magamba na 'coalition' yao ya TLP na UDP?!

Jibu lako la dhahiri kama utaondoa unafiki litakuwa ni wanachama wa magamba pamoja na wanachama 'swaiba' wao wa vyama vya TLP na UDP.
 
Hv ACT kazi yenu ni kupigania wanachama wa upinzani?mbona mko uchi halafu hamjijui?
Kila uchao ugomvi wenu ni dhidi ya upinzani,malengo yenu ni nin?
 
Wanachama wa Cuf,Cdm,NCCR na NLD wasema na wao karibuni watalipua makao makuu ya vyama vyao.

Kama wananchi wa Burkina Faso walivyolipua bunge kwa sababu ya kupitisha kifungu cha kumruhusu rais wao agombee kwa kipindi cha tano baada ya kuwa madarakani kwa miaka 27.

Na wanachama wa Cdm,Cuf,NCCR na NLD wanasema nao wamewachoka wafalme Mbowe,Lipumba,Mbatia na makaidi.

Nawashauri wasilipue ofisi zao bora waondoke huko na kujiunga na wazalendo wa ACT-Tanzania kwani katiba yetu Sura ya Sita Ibara ya 22 namba 2 vifungu vidogo vya (a),(b) na (c) vinasema ukomo wa uongozi ndani ya chama ni vipindi visivyozidi viwili vya miaka mitano.

Karibuni ACT-Tanzania
Taifa Kwanza leo na kesho.

Wewe umekosa kazi.
 
Kama set A(CCM) wana uhusiano na set B(CUF) kule Zanzibar na wakati huo huo huku Bara set B(CUF) anauhusiano na set C(CDM),set D(NCCR) na set E(NLD).
Hivyo basi set C(CDM), set D(NCCR) na set E(NLD) wana uhusiano wa moja kwa moja na set A(CCM)
 
Back
Top Bottom