UKITAKA KUISHI MJINI ISHINDE NJAA KWANZA PAT 2

mkaamweusi

JF-Expert Member
Feb 19, 2013
614
802
Hakikisha ukisha ishinda njaa isiridhike,kitambi kikakutoka wee yale ni matokeo ya mind set kuona kana kwamba shida zote zimekwisha,em jaribu kucheza na akili au mind set yako usiridhike ovyo,
niliona katika mtandao mmoja wa kijamii msg moja eti bakhresa ana utajiri kadhaa hana kitambi,sijui dangote dola kadhaa hana kitambi,wewe na mshahara wako wa laki sita tumbo hilooo,

Japo kuwa wengine ni maumbile yao tuu yaani miili yao inashukuru mapema sana,kwenye ukoo wao,ila samtaimu kuna uhusiano flani hivi na uvivu vivu flani hivi,kujivunavuna flani hivi*(ego),kuitwa itwa boss hivi, endelea kupaform vizuri zaidi kwenye angle ya kuacha historia,jitumie vya kutosha kipindi cha ujana wako.

usisubiri pale miguu na viungo vinashindwa shurba(uzee) ndio ustuke nooo! em chkua hii life is a performance,not a reharsal,kwamba kila unachofanya make sure kina count kwenye maisha yako,yaani vizazi vijavyo viwe na sababu ya kukutaja kwa mazuri lakini! eeenh kwamba alikuwepo flani,alibadili hiki,au alipata kunena haya au alitenda hivi,njoo hapa nikupe mfano nyerere,mandela na fidel catsro,hata miaka mia moja baada ya kufariki inaweza kupita lakini wataendelea kukumbukwa au kuhusianishwa na matukio flani katika jamii na duniani kwa kile walicho changia pindi wana nguvu zao!

kubadili au kuchangia mabadiliko ya jamii sio lazima uwe kwenye platform ya siasa bali hata ukiwa mwandishi,mfano chinua achebe,ngug wa thio'ng,mchoraji mfano Paul Kuczynski,masoud kipanya,Gado au unaweza kuwa mwanamashairi mfano prince,mpoto mrisho, au muimbaji kama R.Kelly,James Blunt,VNV Nation,alpha blonde bob marley na wengine wengi
yaani platform zipo nyingi tuu,cha msingi ni wapi wewe unaona unatosha,jioni njema wakuu!

ccRaphael Ipyana Facebk,instagrm
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom