Ukifanya kipimo cha HSG unaweza kupata ujauzito?

Mama Sabrina

JF-Expert Member
Jul 30, 2016
16,622
27,561
Kwa wanawake/wadada mliowahi kufanya hiki kipimo cha HSG je mlifanikiwa kupata ujauzito, je kuna njia ya kupima tofauti na kipimo hiki maana kinauma sana usiku siku hiyo sikulala mpaka niliumwa homa na baada ya siku mbili nikaingia period.

Inashauriwa ukipima HSG ile ukipona tu yale maumivu ufanye ngono ili mimba iingie, sasa mimi mpenzi alikuwa mbali kiasi kwamba nilipofanyiwa nilikaa tu, mpaka leo sijawahi fanikiwa, tujuzane na kushauriana hapa ni hospitali gani nzuri, au dokta gani mzuri wa wanawake tu, nadhani hii pia itakuwa inasaidia na wengine maana uzazi kwa wengine ni mgumu sana.

Kilichofanya nikafanye hiki kipimo nilikuwa naumwa sana tumbo wakati wa hedhi, kuumwa kiuno na mbavu, lakini nilivyopima niligundulika mirija ya uzazi ina shida imevimba na ikapelekea nikawa sipati siku zangu, nilipofanyiwa kipimo hicho, hayo maumivu yaliisha kabisa maana nilichomwa sindano na dawa nikapewa, tatizo ni naona maumivu ya kuumwa wakati wa hedhi yanarudi tena yaani kiuno kinauma kama sio changu jamani.

Hebu tupeane ushauri najua wengi pia hili tatizo mnalo, najua pia kuna wataalamu humu watasaidia kutoa ushauri mzuri ili siku zijazo tulete mrejesho humu, chochote unachojua kiweke hapa maana haya maumivu ya hedhi sio mazuri kabisa pia tuelekezane sehemu nzuri zenye tiba nafuu sio kupimwa tu laki 2, dawa laki 4.

Karibuni.

ONYO: Waharibu uzi hapa hamtakiwi kabisa, usilete mada tofauti na hii.
 
inashauriwa ukipima HSG ile ukipona tu yale maumivu ufanye ngono ili mimba iingie,,sasa mim mpenzi alikuwa mbali kiasi kwamba nilipofanyiwa nilikaa tu,,mpaka leo sijawah fanikiwa,,
Sasa ni kwa nini ulifanya hicho kipimo wakati mpenzi wako yuko mbali si mngeshauriana kabla na yeye angetulia bila ngono kwa muda wa wiki moja ili sperm zake ziwe nyingi..
 
Miaka ya nyuma nilikua na hilo tatizo nilikua nikiingia period naumwa hadi nalazwa..
Kuna doctor akaniambia suluhisho la hayo maumivu ni utakapo beba mimba. .
By that time sikumuelewa sana sababu nilikua chuo ntabebaje mimba.
Nilivyokuja kubeba mimba ndipo nilipo muelewa hadi leo yale maumivu ni historia

Kwa hiyo my dear concentrate kwenye kutafuta mimba huenda ikawa
Siluhisho na kwako pia..
 
Kwanza ni vyema ungeanza kwa kupima Ultra sound ili wajue pia kuanzia, ikionekana Tatizo kwny Mirija yako ndio ukapime hicho kipimo na faida kubwa ya hicho kipimo ni kuzibua Mirija Kama imeziba kutokana na Uvimbe huo, Hakuna namna ya kutatua Tatizo zaid ya kuizibua, hata ukizibuka mmoja tu inatosha kujaza Duniani kwa kadri uwezavyo!
 
Dalili Ulizo taja hapo ni kama mtu ana MYOMA (FIBROIDS) na hii inawashika watu wengi sanaaa (wakike) nakushauri Fanya Ultrasound ndio itakayo kwambia shida ni nini then kama itakuwa Ni myoma watakupeleka CT scan hapo ndio itaamua kama unaweza kutibiwa au lah
 
Kwa wanawake/wadada mliowahi kufanya hiki kipimo cha HSG je mlifanikiwa kupata ujauzito, je kuna njia ya kupima tofauti na kipimo hiki maana kinauma sana usiku siku hiyo sikulala mpaka niliumwa homa na baada ya siku mbili nikaingia period.

Inashauriwa ukipima HSG ile ukipona tu yale maumivu ufanye ngono ili mimba iingie, sasa mimi mpenzi alikuwa mbali kiasi kwamba nilipofanyiwa nilikaa tu, mpaka leo sijawahi fanikiwa, tujuzane na kushauriana hapa ni hospitali gani nzuri, au dokta gani mzuri wa wanawake tu, nadhani hii pia itakuwa inasaidia na wengine maana uzazi kwa wengine ni mgumu sana.

Kilichofanya nikafanye hiki kipimo nilikuwa naumwa sana tumbo wakati wa hedhi, kuumwa kiuno na mbavu, lakini nilivyopima niligundulika mirija ya uzazi ina shida imevimba na ikapelekea nikawa sipati siku zangu, nilipofanyiwa kipimo hicho, hayo maumivu yaliisha kabisa maana nilichomwa sindano na dawa nikapewa, tatizo ni naona maumivu ya kuumwa wakati wa hedhi yanarudi tena yaani kiuno kinauma kama sio changu jamani.

Hebu tupeane ushauri najua wengi pia hili tatizo mnalo, najua pia kuna wataalamu humu watasaidia kutoa ushauri mzuri ili siku zijazo tulete mrejesho humu, chochote unachojua kiweke hapa maana haya maumivu ya hedhi sio mazuri kabisa pia tuelekezane sehemu nzuri zenye tiba nafuu sio kupimwa tu laki 2, dawa laki 4.

Karibuni.

ONYO: Waharibu uzi hapa hamtakiwi kabisa, usilete mada tofauti na hii.
Majibu ya HSG yalisema una tatizo Gani??.... maana HSG itaangalia Uterus Na Fallopian tubes itaangalia kama imevimba kama imeziba au shape ya uterus na vingine ambavyo vinakufanya Fertelization is fanyikee so nataka kujua Majibu ya Kipimo yalisemaje?

Ila baada ya kipimo huwa tunamwambia mgonjwa atajisikia severe belly pain pia heavy bleeding na Vaginal bleeding

Ila tuanzie kwenye Majibu
 
Clinical History yako sijaona indication ya kufanya HSG....ww ni una mwa sana kiuno wakati wa hedhi lakini sijaona indication ya wewe kufanya HSG ....ww ilitakiwa Ultrasound then CT LABDA uwe kwa daktari na hapa umejieleza tofauti
 
Tatizo la ugonjwa wako ni kubeba mimba. Kama mpenzio yuko mbali njoo mie nikubebeshe nikunusuru na maumivu hayo!
 
Majibu ya HSG yalisema una tatizo Gani??.... maana HSG itaangalia Uterus Na Fallopian tubes itaangalia kama imevimba kama imeziba au shape ya uterus na vingine ambavyo vinakufanya Fertelization is fanyikee so nataka kujua Majibu ya Kipimo yalisemaje?

Ila baada ya kipimo huwa tunamwambia mgonjwa atajisikia severe belly pain pia heavy bleeding na Vaginal bleeding

Ila tuanzie kwenye Majibu
Nilisitisha kuona siku zangu zikawa navuka mwezi mmoja ndio naingia ,,kwenda kupima kwenye kioo ndio wakasema nipime hsg waone vyema ,ndio kukuta upande mmoja uligoma dawa kuingia mpaka waliporudia ndio dawa ikaingia ,,aisee nilikuwa naisikia kabisa inavyoingia ile dawa ,,,walikuta mirija yangu imevimba hasa wa upande wa kulia na nilikuwa napata maumivu ya upande wa tumbo,kizazi kilikuwa hakina shida ni mirija,,

Walivyonipa dawa,,nikawa naingia siku zangu bila kuumwa kiuno wala tumbo,,,sasa naona kama hali inajirudia tena baada ya mwaka hali naona imerudi nikiingia mp aisee mpaka nachemka na kiuno kinauma vibaya sasa naogopa isije kuwa ugumba lo
 
Dalili Ulizo taja hapo ni kama mtu ana MYOMA (FIBROIDS) na hii inawashika watu wengi sanaaa (wakike) nakushauri Fanya Ultrasound ndio itakayo kwambia shida ni nini then kama itakuwa Ni myoma watakupeleka CT scan hapo ndio itaamua kama unaweza kutibiwa au lah
Walisema kulikuwa na viuvimbe vidonge upande wa kulia ndio nikawa nachomwa sindano dawa ili vipote,,,baadae nilienda kupima nikaambiwa nishapona eti
 
Nilisitisha kuona siku zangu zikawa navuka mwezi mmoja ndio naingia ,,kwenda kupima kwenye kioo ndio wakasema nipime hsg waone vyema ,ndio kukuta upande mmoja uligoma dawa kuingia mpaka waliporudia ndio dawa ikaingia ,,aisee nilikuwa naisikia kabisa inavyoingia ile dawa ,,,walikuta mirija yangu imevimba hasa wa upande wa kulia na nilikuwa napata maumivu ya upande wa tumbo,kizazi kilikuwa hakina shida ni mirija,,

Walivyonipa dawa,,nikawa naingia siku zangu bila kuumwa kiuno wala tumbo,,,sasa naona kama hali inajirudia tena baada ya mwaka hali naona imerudi nikiingia mp aisee mpaka nachemka na kiuno kinauma vibaya sasa naogopa isije kuwa ugumba lo

PID ( Pelvic Inflammatory disease)

Pole sana
 

Similar Discussions

4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom