UKAWA wawatia kiwewe CCM

UKAWA wawatia kiwewe CCM

Nafikiri hatuna viongozi wenye utashi, weledi, uwezo na patriotism ya kuweza kutupitia Katiba mpya yenye dhana ya kujenga a good society ndani ya Chama tawala na ndani ya upinzani.

Tukubali tumechemsha na tusitishe zoezi Hadi tujipange upya! Tutapoteza pesa bure.

Si walioko madarakani, si wapinzani na si wananchi wanaweza kusema kwa nini tunataka Katiba mpya, na kwa nini lazima iwe sasa.

Siasa za kubezana, mchakato ulio na mapungufu makubwa na ubinafsi kamwe havitatupa Katiba mpya itakayoleta ustawi wa taifa Letu tukufu.

Ujasiri unahitajika kwa upande wa Uongozi kukubali hili zoezi halina tija kwa wakati Huu. Kuzomeana hakutatupa matokeo tuliotarajia. We lost the game!! Sad
 
Ukawa ni wehu tu hawana cha maana hata kidogo kwao vurugu ndiyo cha msingi zaidi.
 
Yaani wabunge wa ccm ndio leo wanastuka kwamba bila UKAWA hakuna katiba mpya wakati walikuwa wanatukana? Au wameshaona wananchi wengi wapo upande wa rasimu ya Kina Jaji Warioba ambayo UKAWA wanaishikilia ijadiliwe.

Taifa letu linahitaji sana uponyaji
 
Kila jambo na wakati wake hili la katiba limeonyesha dalili ila wkt wake bado,ni vizuri huu mjadala mzito uendelee na bunge lihairishwe hadi tutakapopata muafaka wa kitaifa.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Ukawa ni wehu tu hawana cha maana hata kidogo kwao vurugu ndiyo cha msingi zaidi.
Kwenye hoja kama hizi uwezo wenu vijana wa Lumumba ni mdogo na upuuzi huu mnaoleta humu na ushabiki wa kipumbavu ndio umelifikisha taifa hapa leo. Inaonekana nyinyi ni wafaidika wa mifumo mibovu ambayo mmebaki nyinyi mnaishi vizuri wakati ndugu zenu wamebaki kuwaomba mkae na watoto wao au muwaombee vibarua huko mijini. Kumbe tulitakiwa tuzike tofauti za kisiasa tutengeneze katiba bora ambayo itakupa uhakika wa maisha bila kutegemea hela za kifasadi. Katiba hiyo itakupa wewe na watanzania wengine uhakika wa maisha wewe ni vizazi vyako bila kujali utakuwa hai ama la, chama chako kitakuwa madarakani ama la. Wewe umebaki na hoja za kitoto bila kujua kwamba huna kazi ya maana zaidi ya kukaa hapo ofisini ukiishia kupigania ubovu ambao hauna faida kwako na familia yako kwa muda mrefu.
 
jana Mwingulu anashtuka na kusema ati walikosea kuleta mapezi ya vyama kwenye mchakato wa katiba mapya ...................ingawa NADHANI ILIKUWA NI WOGA WA KUZOMEWA
 
Wehu kwa lipi? Toa hoja. Naona wewe utakuwa ndiyo mwehu kama utakuwa unawatukana bila kuainisha bayana makosa ya ukawa ni yapi. PERIOD

Ukawa ni wehu tu hawana cha maana hata kidogo kwao vurugu ndiyo cha msingi zaidi.
 
jana Mwingulu anashtuka na kusema ati walikosea kuleta mapezi ya vyama kwenye mchakato wa katiba mapya ...................ingawa NADHANI ILIKUWA NI WOGA WA KUZOMEWA

Kama alisema hivyo anastahili pongezi! Unajua jambo baya kabisa ni kuwa NEC ilitoa ultimatum kuwa wajumbe wake wakatae S3, na wapendekeze S2, na hilo ndo kosa linalotugharim hadi leo! Naamini hoja ya kubaki na S2 isingetolewa na NEC ingeibuliwa tu kiustaarab ungekuta hamna ubishi unaoendelea. Katika mfumo wa vyama vingi, jambo lolote la Kitaifa, Chama dola kikishatoa msimamo wake tu basi ujue hisia zitajitokeza kupinga. Jambo hili lilitakiwa likajadiliwe kwanza BMK, badala yake msimamo ukatoka chamani unategemea nini?
 
Hawa ni mapandikizi ambao wako brainwashed. Mwulize hapa anawatukana ukawa kwa kosa lipi. Abainishe, hawezi. Mwulize rasimu ya katiba ina mapungufu yapi yanayomfanya yeye aikataea, hakuna anachojua. Mwambie katiba ya saa ina strengths gani anazoona zitapotea kwenye katiba mpya. Hajui. Mwulize anajua nini kwenye katiba iliyopo, mgogoro.


Hawa ndio wale 75% wanaosogezwa na serikali kwa ajili ya kuficha aibu. Sasa wanajiona wanauwezo na nguvu kwa sababu hawana wanalolielewa la kitaalamu zaidi ya mikumbo ya makundi. Hawana fikra za kujitegemea. Hawajui hata siasa mbovu, na ushabiki wa kijinga unaathari gani katika maisha yake binafsi. Kwanza hajui maana ya elimu wala umuhimu wa mipango ya kitaalamu.

Usishangae wanatake rasimu ya ccm ipelekwe kupigiwa kura kwa wananchi, huku wakijua watashinda kwa rushwa, uzandiki, wizi wa kura na kwa mtaji wa ujinga na umaskini wa wa Tanzania. Watanzania sasa ni wajinga kuliko siku za uhuru. Kwa sababu kundi la 75% linadhani linaelimu na hivyo kujipa ujasiri wa kuvuruga hata masuala ya kitaalamu. Wakati wa Nyerere wasio na shule walijua umuhimu na mipaka yao. Lakin pia walikuwa na matumani kuliko wahuni walioasisiwa na ccm watu wasio na uelewa, wala matumaini. Hivyo wanaishi ili mradi kunakucha.

Tuanhtaji serikali nyingine kabisa ili ijenge Tanzania kwa upya. Hatuwezi kuwa na watu wenye mitazamo ya level hii mstari wa mbele halafu tutegemee taifa huru na lenye maendeleo.


Kwenye hoja kama hizi uwezo wenu vijana wa Lumumba ni mdogo na upuuzi huu mnaoleta humu na ushabiki wa kipumbavu ndio umelifikisha taifa hapa leo. Inaonekana nyinyi ni wafaidika wa mifumo mibovu ambayo mmebaki nyinyi mnaishi vizuri wakati ndugu zenu wamebaki kuwaomba mkae na watoto wao au muwaombee vibarua huko mijini. Kumbe tulitakiwa tuzike tofauti za kisiasa tutengeneze katiba bora ambayo itakupa uhakika wa maisha bila kutegemea hela za kifasadi. Katiba hiyo itakupa wewe na watanzania wengine uhakika wa maisha wewe ni vizazi vyako bila kujali utakuwa hai ama la, chama chako kitakuwa madarakani ama la. Wewe umebaki na hoja za kitoto bila kujua kwamba huna kazi ya maana zaidi ya kukaa hapo ofisini ukiishia kupigania ubovu ambao hauna faida kwako na familia yako kwa muda mrefu.
 
Back
Top Bottom