UKAWA mkae mguu sawa

Wapinzani wakikubali kushiriki uchaguzi huo wa serikali za mitaa December bila daftari kuboreshwa na tena uchaguzi ukisimamiwa na TAMISEMI ( ofiisi ya waziri mkuu wa CCM), basi wasubiri maumivu makali kama anavyojitapa Nape, they must go extra miles kukataa jambo hilo.

Wanatakiwa wakomalie sana mambo mawili ya kuwasaidia, moja uchaguzi usimamiwe na tume ya uchaguzi ( maana ndio wenye mamlaka na utaalam na chaguzi zote ndani ya nchi), hilo halitoshi hata tume wakisimamia kwa daftari la zamani ni hasara kubwa, so wakomae sana Daftari jipya litumike hata uchaguzi ukisogezwa mbele ni sawa, maana hapa ndio ccm itajipanga na kufanya mambo yao, la sivyo wasikubali kushiriki uchaguzi kwenye mazingira haya or wakubali wao ni wasindikizaji and CCM are leaders.

Naamini usiamini wapinzani wa TZ wasivyi na mbinu mbadala watakuambia tutakomaa nao hivyo hivyo, and that will be end of story na biashara kuishia hapo, upinzni imarara ninmuhimu sana kwa ustawi wa taifa lolote kwaajili ya check and balance
 
Ukitaka usitake ccm ndio mshindi
 

hapa lazima tupigane kufa na kupona..vinginevyo maccm..yatAtupiga chenga ya mwili
 
Nitawashangaa sana hao UKAWA wakishiriki huo uchaguzi kwa daftari lililopo la wapigakura. Sijui watakuwa na matarajio gani!

Tatizo siyo daftrai tatizo ni huko "KUCHORA NEMBO"ya chama unachokipigia kura.Huku ni kumnyima haki mpiga kura na yule mgombea.Na kama UKAWA hawaendi mahakamani kwa hili nitawaona hawako makini.
 
Tatizo siyo daftrai tatizo ni huko "KUCHORA NEMBO"ya chama unachokipigia kura.Huku ni kumnyima haki mpiga kura na yule mgombea.Na kama UKAWA hawaendi mahakamani kwa hili nitawaona hawako makini.

Mkuu mabadiliko tunayoyatamani Hayaanzii UKAWA yanaanzia kwako namimi kwa tafsiri rahis UKAWA niww na mimi MBOWE na LIPUMBA wapo pale km maKAMANDA waongoza vikosi so Unapoona mambo hayaendi km unavyotamani basi unafanya km KUBENEA na BUNGE la KATIBA,,,,!
 

Unachosema ni kweli kabisa.Wajua lakini kwenye hili tunawategemea zaidi wanasheria sisi wa shule za kata,tusupport tu kwenye ajenda kama kufanya promo nk.Sheria wengine imekaa pembeni sana ndugu yangu.
 
Tatizo siyo daftrai tatizo ni huko "KUCHORA NEMBO"ya chama unachokipigia kura.Huku ni kumnyima haki mpiga kura na yule mgombea.Na kama UKAWA hawaendi mahakamani kwa hili nitawaona hawako makini.
Habari ya kuchora nembo umeiibua wapi? Usiamini kila unachokisoma humu JF.
 
Unatumia lipi mkuu

Ufafanuzi
Hujasikia watu wa kila lamina kuwa wajumbe wa CCM wa nyumba kami (mabalozi) wanaorodhesha w wakazi wa maeneoon yao? Kiujumla kazi hiyo inatakiwa ifanywe na serikali za mitaa kwa maeneo husika. Mipaka inatakiwa iainishwe na serikali Kuu. Haya yote hayajafanyika kwa uwazi na kushirikisha wadau.
 
Habari ya kuchora nembo umeiibua wapi? Usiamini kila unachokisoma humu JF.

Source: Jana taarifa ya habari (kati ya star TV au Ch. 10) sikumbuki vizuri channel, ila ameonekana Mh. mbowe akilalamika hayo kwenye Kikao cha Kamati Kuu CDM.

Aliongeza kuwa hii ni mbinu ya kuharibu kura za CDM.

Take: Inawezekana itakuwa ukikosea kuchora nembo tu kura inaharibika hasa kwa wapinzani.
 
hapa lazima tupigane kufa na kupona..vinginevyo maccm..yatAtupiga chenga ya mwili

Watu lazima waelewe inatumia register ya waazi wa mtaa na si daftari la NEC. Tatizo ni viongozi wa mtaa ndo waandiishaji je watawaandiisha wapinzani? Watu wengi watajiuta uchaguzi umepita tu. Wapinzani lazima waanze upita mitaani na magari ya matangazo kuwaeleza watu waande ujiandiisha
 
Nchi inakoelekea siko! ccm wamegundua mwisho wao umefika. Watafanya kila hila lakini watashindwa. Daftari la wapiga kura lazima liboreshwe kwanza, kama alivyosema Lubuva, kabla ya uchaguzi wowote. Huwezi kuwanyima haki ya kupiga kura mamilioni ya vijana waliofikisha umri wa kupiga kura.
 
Wanatakiwa kwenda mahakamani kupinga utaratibu huo kama upo, na kuzuia uchaguzi wa mitaa mpaka mahakama iamue shauri lao. Daftari ni moja tu.
 

Kwa maana wakipn.a imekula kwao!
Huja kosea kabisa,na safari hii wakikosea namna ya kushughulika na hawa jamaa wasimlaumu mtu!.

Uchaguzi wa Serikali ya Mtaa-ni lazima uwe chini ya Tume ya uchaguzi
Daftari la wapiga kura lazima lifanyiwe marekebisho ,kuingiza wapi na kuondoa waliohama au kufariki.

Kura ya Maoni ya Katoba pendekezwa lazima itumie Daftari liliorekebishwa.
Tume ya Uchaguzi iwe na Wajumbe wanaokubalika na Vyama vyote na iwe huru.
Kinyume na hapo ni bora kutokushiriki katika zoezi hilo la Uchaguzi au Kura ya maoni ya Katiba.

Kufanikisha mikakati hiyo utaalamu wa ziada unahitajika,la muhimu kila Kanda ijiandae namna ya utekelezajikulingana na Mazingira.
 
serikali za mitaa hawatumii daftari la NEC

kwa uzoefu wa uchaguz ulopita ni kweli daftari halitumiki lkn kitambulisho kinatumika ambacho no sawa na kutumia daftari..
 
Wanavyopenda juice za Ikulu lazima wakubali tu...

Nyie watu wa maGAMBA cjui mnatumia viungo gani kufikiri yaani nyie muda wote mnafikiria KULA tu,,,ndio maana mnachaguana kwa Sahani ya WALI MAHARAGE sasa watu km nyie mna umuhimu gani kwenye NCH hii
 
Habari ya kuchora nembo umeiibua wapi? Usiamini kila unachokisoma humu JF.

Siyo tu humu JF hata kwenye magazeti nimeliona hili jambo.Na kama halina ukweli basi wahusika wangekanusha haraka sana.Na mhusika mkuu hapa NI WM Pinda!
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…