UKAWA badilisheni mfumo wa siasa zenu-Ni wakati wa kubadilika

General Mangi

JF-Expert Member
Dec 21, 2013
15,300
23,023
Wanabodi salaam

Kama tunavyoona kasi ya rais Magufuli na jinsi alivyoiteka audience katika nchi.

Kila nikitazama vyama vya upinzani hasa vilivyo katika umoja wao, UKAWA bado naona hawajui wafanye nini kwasasa.

Jinachonichanganya zaidi, Ukawa hufanya maamuzi ambayo wanashindwa kujua hatma ya maamuzi yao pale itakapo shindikana.

Kwa mfano, wameshindwa kabisa kwa umoja wao kulisimamia suala la zanzibar, wamekuwa wakitoa matamko ambayo hayana impacts yoyote kwa wafuasi wao. Ukawa kwa umoja wao wameshindwa kabisa kuwaaunganisha wafuasi wao kuamini kile wao wanaona ni sahihi.

Tukio jingine ni lile la bungeni kuhusu TBC kuonyesha matangazo live. Ukawa walitoka nje kupinga maamuzi hayo, alafu tunawaona kesho yake wapo bungeni kushiriki vikao vya bunge na kuachana na msimamo wao.
Nashindwa kuelewa wakati wanafanya maamuzi haya huwa hawajiulizi fate ya maamuzi yao itakuwa nini.

Ukawa kwa umoja wao anashindwa kuwa wabunifu wakufanya wananchi waaunge mkono.

Inashangaza Chadema kutumia rasilimali nyingi kuzunguka na helkopta nchi nzima wakati walikuwa na uwezo wakufubgua redio yao na gazeti lao na kuwafikia watanzania kila siku,kitu ambacho si tu kujitangaza, pia kupata mapato ya kukijenga chama zaidi.

Tunaweza kuwabeza CCM na vyombo vyao vya habari, lkn tukumbuke kuwa vyombo hivyo huvitangaza chama chao.

Chadema kinajua kuwa vijana wengi hata kwenye mitandao wanawaunga mkono, lakini cha kushangaza wameshindwa kutumia fursa hiyo kujiendelezaa.

Ushauri.

2. Sasa ni wakati wa kubadilika kulingana na siasa zinavyokwenda. Ni wakati wa kuweka maslai yenu pembeni na kujenga umoja, chama kamili, chama kikubwa cha upinzani, tena mushirikishe na ACT -wazalendo.

2. Mje na itikadi inayopendwa na watanzania, mfumo gani mtakao tumia kuongoza nchi.

3. Anzisheni media yenu ambayo itawafikia watanzania kujitangaza zaidi. Muunganiko wa vyama vyenu vya upinzani bungeni na kuunda chama kimoja sidhani kama mtashindwa kuwa na redio na gazeti lenu.

4. Angalieni jinsi ya kuwaunganisha watanzania wawaunge mkono pale mnapoona mnachokisimamia kinafaa kwa jamii. Inashangaza kila jambo bovu hapa nchini linafanyika lkn wananchi hawaoneshi hisia zozote kupinga ubovu huo, hapa inaonesha vyama vya upinzani mmeshindwa kuwaunganisha watantania.

5.Onesheni mifano ya kupambana na ufisadi katika majimbo yenu, kila mbunge aishi jimboni kwake na wananchi wake kutatua kero za wananchi.

Hitimisho.

Ndugu wana JF, linapokuja suala la kukosoa upinzani pale ambapo unaona si sawa, ni vema kila mtu akaunga mkono. Kama wana Ukawa mnavyopenda kuikosoa serikali ya ccm, basi na ninyi mkubali kukosolewaa.

Ifike hatua pale ambapo, Mbowe, Lissu, Lowassa, Seif, Mbatia, Zitto anakosea, tumwambie ukweli kwamba unakosea, unaharibu.
Lakini hili suala la kuwatetea kwa kila jambo linawafanya vipofu, wanabweteka zaidi.

Bado ninaimani na upinzani katika nchi yetu, lakini nataka upinzani makini na wenye nguvu ya ushawishi.

Asanteni.
 
Kwa taarifa yako upinzani hautakaa ufe cose hata hao waliowaweka watawala madarakani hawatakubali hilo, kama siyo nguvu ya upinzani usingeyaona haya,fikiria miaka mitano mafuta hayapimwi mita zimechakachuliwa ,utitiri wa vituo vya mafuta umeanzia kibaha hadi chalinze,kisa yanapita throuw way
 
kosoa hoja iliyopo mezani mkuu, sio vijembe visivyo na maana
Nchi hii hakuna wapinzani kuna wachumia tumbo tu; kelele za nini waacheni walioshinda waendeshe serikali yao na kuhudumia watu nyie kawatafuteni kondoo elfu saba elfu (milioni 7) ambao hawakupiga kura muwashawishi kuwa wanachama wenu: makelele na ngumi havitawapeni ushindi katu bali umaarufu wa bei ndogo
 
UKAWA walifanya kosa kubwa sana kumsimamisha Lowassa na kukipokea kikundi cha mafisadi toka ccm. Ni kosa litalowasumbua kwa muda mrefu sana na linaenda kuiua kabisa chadema.
 
Endeleeni kumjadili lowassa wakati ukawa wakiikaba serikali kodi zikusanywe ipasavyo.
 
Sijawahi kuona ukawa wakiikaba serikali bali wanalilia kuuza sura kwenye tv ambao ni upuuzi wa kimataifa.
Kama hawaikabi kwanini kuzuia Bunge live???Kama Magufuli anataka kusaidiwa kwanini afunge midomo watu???
 
Kama kusoma hujui hata picha uoni ndugu,ccm ikikumbuka upinzani waliopata hata wasira angekuwa bungeni asingelala tena Mungu bariki ukawa ccm wasipate usingizi ili wasimamie maslahi ya nchi bila kujimilikisa wenyewe
 
Nchi hii hakuna wapinzani kuna wachumia tumbo tu; kelele za nini waacheni walioshinda waendeshe serikali yao na kuhudumia watu nyie kawatafuteni kondoo elfu saba ambao hawakupiga kura muwashawishi kuwa wanachama wenu: makelele na ngumi havitawapeni ushindi katu bali umaarufu wa bei ndogo


Basi haina haja ya kupiga kura nakupoteza muda mwingi kuwasikiliza wanasiasa ipitishwe na ijulikane wazi kwamba Tanzania hakuna mfumo wa vyama vingi. Pia ifahamike kwamba suala la uchaguzi ni jipu kubwa sana. Hawa wahisani wanao toa pesa zao kwa shughuli za uchaguzi tukumbuke kwamba haziendi bure wanakuja nyonya rasilimali zetu kwa kigezo chakusaidia shughuli za uchaguzi.
 
Mleta mada nafikiri utakuwa umepatwa na mihemuko tu ya kisiasa. Bado sijaona mantiki ya hoja yako.
 
Kama hawaikabi kwanini kuzuia Bunge live???Kama Magufuli anataka kusaidiwa kwanini afunge midomo watu???
Bunge alionyeshwi live na tbc sababu ya kubana matumizi pesa zisaidie taifa.


Magufuli ajawai kufunga mtu mdomo ila kama kuna wajinga wanataka kupata sifa za kishamba lazima washughulikiwe.
 
Nilimsoma kwanza Kitila kama hivi....
Wakaja waungwana wengine kama hivi.....sasa ni wewe Ibilisi

Ila sasa naona mapokeo ya wakereketwa ni vile vile. Naanza kuwaamini wale wasemao kuwa kabla ya kukuangamiza Mwenyezi Mungu hutuma waja wake kwanza kukupa fursa ya angalizo na kujirekebisha na baada ya ukaidi yeye hukuongezea upofu na ukiziwi....asilani huwezi kuona wala kusikia lolote lakini ndio hivyo unakuwa unaelekea shimoni. Time will tell!!!!
 
Bunge alionyeshwi live na tbc sababu ya kubana matumizi pesa zisaidie taifa.


Magufuli ajawai kufunga mtu mdomo ila kama kuna wajinga wanataka kupata sifa za kishamba lazima washughulikiwe.

Hata TBC wangeweza kuonyesha kama wangeSTRETCH akili zao zaidi.Hivi imeshindikana kupata wafadhli wa kufadhili MATANGAZO kibiashara??Na MATANGAZO je???Hivi wameshidnwa kuuzia vituo vingine habari ili pasiwepo na hiyo hasara???

SIkatai inawezekana ni gharama lakini imeshindikana kufanya matangazo ya BUNGE kugenerate income ya kituo???Tatizo miubongo ya wakurugenzi na wanasiasa wetu imelela kabisa.Hivi Nape alishindwa kuwaagiza TBC kuyafanya matangazo hayo yawe ya kibiashara???

Tumelala tunasubiri wazungu waje kutamsha.
 
Wapinzani hawana la kuongea wamebaki wanasubiri kick wapate pa kuuzia sura
 
Back
Top Bottom