Ujerumani; North korea ni ya nne kwa uwezo duniani

kimsboy

JF-Expert Member
Oct 17, 2016
9,839
20,285
Idara ya intelejensia nchini Ujerumani imesema kuwa, Korea Kaskazini ina jeshi la nne duniani na mpinzani wa nguvu wa Marekani.
Tovuti Ujerumani ya Astatysta na ambayo inajihusisha na ukusanyaji wa taarifa za kiintelejensia yenye makao yake mjini Hamburg, Ujerumani imeandika kuwa, kutokana na hatua ya Marekani ya kuelekeza meli zake za vita kuelekea katika pwani ya Korea Kaskazini, Pyongyang imeionya Washington kwamba, imejiandaa kwa ajili ya vita yoyote tarajiwa na Marekani.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Korea Kaskazini imeitahadharisha Marekani kwamba Washington inatakiwa ifikirie mara mbilimbili matokeo mabaya ya chokochoko zake hizo. Kuhusiana na hilo Pyongyang imetangaza kuwa, endapo meli hizo zitajaribu kufanya harakati yoyote ya kichokozi, basi Korea Kaskazini itawalenga kwa kuwashambulia marafiki wa Washington katika eneo hilo. Tovuti hiyo ya idara ya intelejensia ya Ujerumani imetathmini uwezo wa jeshi la Korea Kaskazini kwa kutegemea vyanzo vya ripoti za Kituo cha Kistratijia cha Kimataifa na kadhalika gazeti la The New York Times la nchini Marekani na kuandika kuwa, ikiwa mgogoro utaongezeka, Pyongyang inao askari wa kutosha kwa ajili ya operesheni za kukabiliana na waitifaki wa Marekani katika eneo la Peninsula ya Korea.
Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Kistratijia chenye makao yake nchini Marekani kimeandika kuwa, Korea Kaskazini ina jeshi la nne duniani na kwamba uwezo wake katika kukabiliana na majeshi ya ardhini, haufai kupuuzwa. Inafaa kuashiria kuwa, Uchina ndio nchi yenye jeshi la pili duniani kwa kuwa na askari milioni mbili na laki mbili, huku India ikiwa na askari milioni moja na laki nne. Marekani ina jeshi la askari milioni moja na laki tatu, huku Korea Kaskazini ikiwa na jeshi lenye askari milioni moja na laki mbili.
Chanzo; parstoday.sw
 
Naamini CIA ,MOSSAD na MI6 japo hawana uhakika 100%na kinafanyika Pyongyang lakini kwa walichonacho wanaweza kumshauri Trump kuwa maisha ya watu wa eneo la Pacific yana thamani sawa na wamarekani kitendo cha kuBET maisha ya wajapani na wakorea kusini kinaweza kuleta madhara mkubwa sana kwa Upande wa kiuchumi wa nchi ya US na Ulaya kiujumla
 
NK ni Nchi ngumu sana taarifa zake kukaa uchi haina utaratibu wa kusambaza mambo yao kama Nchi nyinginezo hili huwawia watu ugumu wakujua ni nchi ya aina gani na yenye vitu vya aina gani.

Japan, SK zinahofu ya machafuko zaidi hata ya NK maana wanalazimishwa kujifunga kitanzi ambacho hakiwahusu na US ....na kwa akili za Kim kama US atamtibua basi nadhani madhara makubwa yatazikumba nchi hizo ambazo ni washirika wa US.

Najua US inapeleleza kujua undani wa NK na kiburi chake ila sio nchi ya kuingiliwa kirahisi kama wengi wanavyodhani
 
Wachambuzi mmekuwa wengi tatizo. Wako watu humu mnajifanya kuzijua Korea Kaskazin, USA,Russia etc zaidi kuliko hata maraisi au wakuu wa vyombo vya inteligensia vya huko. Acha kubabaisha fanyeni kazi
 
Idara ya intelejensia nchini Ujerumani imesema kuwa, Korea Kaskazini ina jeshi la nne duniani na mpinzani wa nguvu wa Marekani.
Tovuti Ujerumani ya Astatysta na ambayo inajihusisha na ukusanyaji wa taarifa za kiintelejensia yenye makao yake mjini Hamburg, Ujerumani imeandika kuwa, kutokana na hatua ya Marekani ya kuelekeza meli zake za vita kuelekea katika pwani ya Korea Kaskazini, Pyongyang imeionya Washington kwamba, imejiandaa kwa ajili ya vita yoyote tarajiwa na Marekani.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Korea Kaskazini imeitahadharisha Marekani kwamba Washington inatakiwa ifikirie mara mbilimbili matokeo mabaya ya chokochoko zake hizo. Kuhusiana na hilo Pyongyang imetangaza kuwa, endapo meli hizo zitajaribu kufanya harakati yoyote ya kichokozi, basi Korea Kaskazini itawalenga kwa kuwashambulia marafiki wa Washington katika eneo hilo. Tovuti hiyo ya idara ya intelejensia ya Ujerumani imetathmini uwezo wa jeshi la Korea Kaskazini kwa kutegemea vyanzo vya ripoti za Kituo cha Kistratijia cha Kimataifa na kadhalika gazeti la The New York Times la nchini Marekani na kuandika kuwa, ikiwa mgogoro utaongezeka, Pyongyang inao askari wa kutosha kwa ajili ya operesheni za kukabiliana na waitifaki wa Marekani katika eneo la Peninsula ya Korea.
Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Kistratijia chenye makao yake nchini Marekani kimeandika kuwa, Korea Kaskazini ina jeshi la nne duniani na kwamba uwezo wake katika kukabiliana na majeshi ya ardhini, haufai kupuuzwa. Inafaa kuashiria kuwa, Uchina ndio nchi yenye jeshi la pili duniani kwa kuwa na askari milioni mbili na laki mbili, huku India ikiwa na askari milioni moja na laki nne. Marekani ina jeshi la askari milioni moja na laki tatu, huku Korea Kaskazini ikiwa na jeshi lenye askari milioni moja na laki mbili.
Chanzo; parstoday.sw
Hiv ndio vitu vya kuandika humu safi sana mkuuu
 
Idara ya intelejensia nchini Ujerumani imesema kuwa, Korea Kaskazini ina jeshi la nne duniani na mpinzani wa nguvu wa Marekani.
Tovuti Ujerumani ya Astatysta na ambayo inajihusisha na ukusanyaji wa taarifa za kiintelejensia yenye makao yake mjini Hamburg, Ujerumani imeandika kuwa, kutokana na hatua ya Marekani ya kuelekeza meli zake za vita kuelekea katika pwani ya Korea Kaskazini, Pyongyang imeionya Washington kwamba, imejiandaa kwa ajili ya vita yoyote tarajiwa na Marekani.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Korea Kaskazini imeitahadharisha Marekani kwamba Washington inatakiwa ifikirie mara mbilimbili matokeo mabaya ya chokochoko zake hizo. Kuhusiana na hilo Pyongyang imetangaza kuwa, endapo meli hizo zitajaribu kufanya harakati yoyote ya kichokozi, basi Korea Kaskazini itawalenga kwa kuwashambulia marafiki wa Washington katika eneo hilo. Tovuti hiyo ya idara ya intelejensia ya Ujerumani imetathmini uwezo wa jeshi la Korea Kaskazini kwa kutegemea vyanzo vya ripoti za Kituo cha Kistratijia cha Kimataifa na kadhalika gazeti la The New York Times la nchini Marekani na kuandika kuwa, ikiwa mgogoro utaongezeka, Pyongyang inao askari wa kutosha kwa ajili ya operesheni za kukabiliana na waitifaki wa Marekani katika eneo la Peninsula ya Korea.
Kituo cha Kimataifa cha Utafiti wa Kistratijia chenye makao yake nchini Marekani kimeandika kuwa, Korea Kaskazini ina jeshi la nne duniani na kwamba uwezo wake katika kukabiliana na majeshi ya ardhini, haufai kupuuzwa. Inafaa kuashiria kuwa, Uchina ndio nchi yenye jeshi la pili duniani kwa kuwa na askari milioni mbili na laki mbili, huku India ikiwa na askari milioni moja na laki nne. Marekani ina jeshi la askari milioni moja na laki tatu, huku Korea Kaskazini ikiwa na jeshi lenye askari milioni moja na laki mbili.
Chanzo; parstoday.sw
Ya kwanza ni IPI? Na Tanzania ni ya ngap?
 
Back
Top Bottom