Awali ya yote nitumie fursa hii kumshukuru Mungu muumba wa mbingu na ardhi na vyote vilivyomo, lakini pia namshukuru kwa kuijaalia nchi yetu kuwa na amani na utulivu ambao umefanya taifa letu kuwa na sifa kubwa dunia, lakini pia kwa kukijaalia chama chetu kuwa chama pekee chenye uwezo wa kutatua kero na shida za watanzania lakini pia kuwa tumaini la watanzania katika maisha yao.
Baada ya kutanguliza kusema hayo, nitumie fursa hii pia kutoa pongezi za dhati kwa Mhe John Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na pia kwa wajumbe wote wa Halmashauri kuu ya Taifa NEC, kwa sasa tunaweza kusema kuwa CCM imefanya usajili mpya wa timu ya ushindi kwa miaka 100 ijayo, hatuna mashaka na timu hiyo hata kidogo.
Kama wanachama wa Chama cha Mapinduzi tunajukumu kubwa na zito la kuhakikisha tuna waunga mkono viongozi wetu wapya na kutoa ushirikiano wetu wa dhati kwa ustawi na uimara wa Chama chetu.
Katika hotuba yake Mhe. Jakaya Kikwete katika mkutano mkuu wa Chama juzi alisema, moja ya changmoto kubwa ambayo kwa sasa chama kinapitia ni kuwa na wanachama wavivu wa kutoa ada za uanachama. Hivyo basi yatupaswa tutambue ya kuwa maendeleo ya Chama yanaletwa na sisi wenyewe, lakini pia ili cha kiweze kuganya shughuli zake bila kigugumizi lazima kiwe na msingi imara wa fedha.
Nakosa neno zuri la kusema kwa kumpongeza Mhe Magufuli kwa hatua nzuri na muhimu aliyo ichuku ya kuteua tume kwa nia ya kufanya tathmini ya miradi yote ya chama, hatua hii ni nzuri kwani itakisaidi chama kujua ni kiasi gani chama kinapata kwa mwaka kupitia miradi yake lakini pia kufanya uiano wa mapato hayo na miradi husika.
USHAURI WANGU KWA WANACHAMA.
1. Kutoa ushirikiano kwa tume hii pindi itakapo hitajika kupata taarifa husika juu ya miradi hiyo.
2. Kutoa mapendekezo yao kama wanachama ya namna bora ambayo miradi hiyo inaweza kutumika ikiwa kama sehemu ya kuongeza mapato ndani ya chama kupitia vyanzo vyake iwapo miradi hiyo inatumika chini ya matumizi bora.
3. Kutoa ushauri wao wa kubuni miradi mbadala ya kusaidia ukuaji wa mapato ya chama.
4. Mbali na mapendekezo hayo lakini pia Chama kuangalia namna gani kinaweza kwenda na usasa katika kubuni njia bora ya ukusanyaji wa mapato kwa njia ya ki elektroniki ili kupunguza mianya ya upotevu wa mapato, kuanzia ulipaji wa ada za wanachama hadi mapato ya miradi.
Nirudie kuwa omba ndugu zangu wapendwa wangu na wana ccm wenzangu, sisi ndiyo walinzi na wajenzi wa Chama chetu. Hakuna sababu ya kutofautiana na kuweka makundi kwani sote tunaishi katika nyumba moja. Jukumu letu kubwa la msingi ni kuhakikisha CCM inaendelea kuwa madarakani na kuisaidia serikali katika kutimiza majukumu yake.
Mwisho nirudie tena kumpongeza Mhe Magufuli Rais wetu mpendwa kwa kuamua kuubeba mzigo mzito wa kulitumikia taifa letu na chama chetu kwa maslahi ya taifa letu, na kwa watenfaji wote wa chama na serikali kwa kazi nzuri wanayo ifanya.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI WANA JF.
Baada ya kutanguliza kusema hayo, nitumie fursa hii pia kutoa pongezi za dhati kwa Mhe John Magufuli Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na pia kwa wajumbe wote wa Halmashauri kuu ya Taifa NEC, kwa sasa tunaweza kusema kuwa CCM imefanya usajili mpya wa timu ya ushindi kwa miaka 100 ijayo, hatuna mashaka na timu hiyo hata kidogo.
Kama wanachama wa Chama cha Mapinduzi tunajukumu kubwa na zito la kuhakikisha tuna waunga mkono viongozi wetu wapya na kutoa ushirikiano wetu wa dhati kwa ustawi na uimara wa Chama chetu.
Katika hotuba yake Mhe. Jakaya Kikwete katika mkutano mkuu wa Chama juzi alisema, moja ya changmoto kubwa ambayo kwa sasa chama kinapitia ni kuwa na wanachama wavivu wa kutoa ada za uanachama. Hivyo basi yatupaswa tutambue ya kuwa maendeleo ya Chama yanaletwa na sisi wenyewe, lakini pia ili cha kiweze kuganya shughuli zake bila kigugumizi lazima kiwe na msingi imara wa fedha.
Nakosa neno zuri la kusema kwa kumpongeza Mhe Magufuli kwa hatua nzuri na muhimu aliyo ichuku ya kuteua tume kwa nia ya kufanya tathmini ya miradi yote ya chama, hatua hii ni nzuri kwani itakisaidi chama kujua ni kiasi gani chama kinapata kwa mwaka kupitia miradi yake lakini pia kufanya uiano wa mapato hayo na miradi husika.
USHAURI WANGU KWA WANACHAMA.
1. Kutoa ushirikiano kwa tume hii pindi itakapo hitajika kupata taarifa husika juu ya miradi hiyo.
2. Kutoa mapendekezo yao kama wanachama ya namna bora ambayo miradi hiyo inaweza kutumika ikiwa kama sehemu ya kuongeza mapato ndani ya chama kupitia vyanzo vyake iwapo miradi hiyo inatumika chini ya matumizi bora.
3. Kutoa ushauri wao wa kubuni miradi mbadala ya kusaidia ukuaji wa mapato ya chama.
4. Mbali na mapendekezo hayo lakini pia Chama kuangalia namna gani kinaweza kwenda na usasa katika kubuni njia bora ya ukusanyaji wa mapato kwa njia ya ki elektroniki ili kupunguza mianya ya upotevu wa mapato, kuanzia ulipaji wa ada za wanachama hadi mapato ya miradi.
Nirudie kuwa omba ndugu zangu wapendwa wangu na wana ccm wenzangu, sisi ndiyo walinzi na wajenzi wa Chama chetu. Hakuna sababu ya kutofautiana na kuweka makundi kwani sote tunaishi katika nyumba moja. Jukumu letu kubwa la msingi ni kuhakikisha CCM inaendelea kuwa madarakani na kuisaidia serikali katika kutimiza majukumu yake.
Mwisho nirudie tena kumpongeza Mhe Magufuli Rais wetu mpendwa kwa kuamua kuubeba mzigo mzito wa kulitumikia taifa letu na chama chetu kwa maslahi ya taifa letu, na kwa watenfaji wote wa chama na serikali kwa kazi nzuri wanayo ifanya.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
MUNGU IBARIKI AFRIKA, MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU WABARIKI WANA JF.