Ujambazi unaoendelea nchini, tunakosea wapi?

Daniel Mjema

Member
Jul 23, 2007
77
84
Ndugu zangu,

Jana usiku kulitokea ujambazi huko Tanga ambako watu wanne waliuawa. Juzi saa 8:00 usiku wa kuamkia jana majambazi wakiwa na silaha walipanga mawe eneo la Mgagao wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro na kuwapora madereva na abiria wa malory. Ukitizama mfululizo wa matukio ya ujambazi nchini utakubaliana na mimi mambo muhimu yafuatayo:-

1. Bado usalama wa Taifa hawawajibiki ipasavyo maeneo yao ili kukusanya taarifa za uhalifu na wahalifu wanaotishia usalama wa nchi. Zamani walikuwa hawafahamiki, walijichanganya na wananchi kukusanya taarifa. Leo baadhi ya maofisa usalama wa taifa(sio wote) wanaona hadi ufahari kujitambulisha au kutambuliwa na jamii

2. Jeshi la Polisi linapaswa kusukwa upya ili liendane na mabadiliko ya sayansi na tekinolojia ambapo wahalifu hasa majambazi, wanatumia akili nyingi kupanga matukio. Jeshi la polisi lifuatilie nyendo za polisi wake waliofukuzwa baada ya kutiwa hatiani na mahakama zao za kijeshi. Wachunguzwe wanafanya shughuli gani maana hadi miaka ya 80,polisi akifukuzwa alikuwa akirejeshwa hadi kijijini kwao na kumkabidhi kwa uongozi wa kijiji. Leo hii tuko nao uraiani lakini hawajulikani wanafanya kazi gani kujiingizia kipato. Wako ambao ni wema lkn wapo ambao ulikosekana tu ushahidi wa kuwatia hatiani katika mahakama za kiraia japo kwenye mahakama ya kijeshi walitiwa hatiani. Kitengo cha Intelijensia cha polisi kiimarishwe ili kukusanya taarifa sahihi za wahalifu na uhalifu wasijikite kutafuta tu taarifa za kiintelijensia pale kunapokuwa na mivutano ya kisiasa kuhusu maandamano na mikutano ya vyama vya siasa hasa hasa upinzani. Jeshi la polisi litambuliwe linakabiliwa na changamoto kubwa ya uhalifu wa kimakundi hasa uhalifu unaojikita kwenye mwavuli wa dini.

3. Mhimili wa mahakama nao utimize wajibu wao katika kutenda haki. Wasiwe wanatafuta visingizio vya dosari za kiufundi ili tu kumwachia mtu aliyepatikana na hatia ya wizi wa kutumia silaha. Jaji au Majaji wa mahakama za rufaa watazame ushahidi wa jumla kama una uzito kiasi gani badala ya baadhi yao kutafuta vidosari vidogo vidogo vya utaratibu wa uendeshaji wa kesi lower courts ili tu kuhalalisha kuwaachia watuhumiwa sugu wa ujambazi. Wajue wahalifu hawa iko siku watabisha hodi kwenye nyumba zao hata kama sio kwa Jaji au Hakimu aliyemwachia lkn hata kwa coleague. Uzoefu unathibitisha kuwa wengi waliofungwa miaka 30 kwa ujambazi wa kutumia silaha wanapoachiwa hurudi kujihusisha na uhalifu tena kama mwanzo alifungwa kwa kutumia kisu anaporudi hupanda daraja na kutumia bunduki au bastola.

4. Kuna haja ya kukiingiza cheo cha Balozi wa Nyumba kumi kumi kuwa chro rasmi cha kiserikali. Mtakumbuka baada ya sheria ya mfumo wa vyama vingi hawa walibakia kuwa viongozi wa CCM ambao huchaguliwa na mkutano mkuu wa Shina la CCM. Tutafute njia bora ya kupatikana kwao, kama ni kutumia utaratibu ule ule wa kumchagua mwenyekiti wa mtaa au wa kitongoji ni sawa ili awe na uhalali wa kuwa kiongozi wa kiserikali wa kusimamia nyumba hizi kumi. Ili mgeni yeyote katika hizo nyumba kumi lazima aandikishwe kwa balozi wa eneo husika ametokea wapi, amekuja kwa shughuli gani, mwenyeji wake ni nani na liwe sharti la lazima kuja na uthibitisho wa barua kutoka katika nyumba zile kumi anapotokea. Hii itasaidia kuwatambua watu wanaoletwa na kuhifadhiwa katika mitaa yetu halafu usiku wanakwenda kufanya uhalifu

5. Sisi kama raia hatujatimiza wajibu wetu kikamilifu kwa kufichua mipango ya uhalifu na wahalifu. Wala tusijitetee. Wahalifu hawa tunaishi nao na ni ndugu, jamaa na marafiki zetu. Pilikapilika za uhalifu zinaweza kuonekana katika mitaa yetu. Tuzitilie mashaka pilikapilika hizi hasa zinapohusisha wageni mitaani kwetu. Tusiguswe kufichua uhalifu tu pale tunapoguswa moja kwa moja kwa ndugu au jamaa kuuawa au kuporwa na hata kujeruhiwa. Tusisubiri kwa sababu uhai huwezi kuununua dukani.

Watanzania tukiamua, tunaweza kuupunguza uhalifu

Siku njema
 
Uhalifu ni uhalifu tu ndugu yangu whether ufanywe na Mtanzania au raia wa kigeni katika ardhi ya Tanzania. Ninachojaribu kusema lipo tatizo mahali fulani. Hebu tufanye tumeamini tukio la Tanga ni foreigners (japo binafsi siamini), hivi mgeni anaweza kutekeleza uhalifu hapa nchini bila kuwa na Mtanzania? Mipango hii inafanyika kwenye majumba yetu na pilikapilika hizi wengi wetu tunaziona lkn hatuchukui hatua mpaka pale tunapoguswa na tukio la uhalifu. Lazima sisi kama raia tufanye kitu tusiviachie vyombo vya usalama peke yao.
 
Ndugu zangu,

Jana usiku kulitokea ujambazi huko Tanga ambako watu wanne waliuawa. Juzi saa 8:00 usiku wa kuamkia jana majambazi wakiwa na silaha walipanga mawe eneo la Mgagao wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro na kuwapora madereva na abiria wa malory. Ukitizama mfululizo wa matukio ya ujambazi nchini utakubaliana na mimi mambo muhimu yafuatayo:-

1. Bado usalama wa Taifa hawawajibiki ipasavyo maeneo yao ili kukusanya taarifa za uhalifu na wahalifu wanaotishia usalama wa nchi. Zamani walikuwa hawafahamiki, walijichanganya na wananchi kukusanya taarifa. Leo baadhi ya maofisa usalama wa taifa(sio wote) wanaona hadi ufahari kujitambulisha au kutambuliwa na jamii

2. Jeshi la Polisi linapaswa kusukwa upya ili liendane na mabadiliko ya sayansi na tekinolojia ambapo wahalifu hasa majambazi, wanatumia akili nyingi kupanga matukio. Jeshi la polisi lifuatilie nyendo za polisi wake waliofukuzwa baada ya kutiwa hatiani na mahakama zao za kijeshi. Wachunguzwe wanafanya shughuli gani maana hadi miaka ya 80,polisi akifukuzwa alikuwa akirejeshwa hadi kijijini kwao na kumkabidhi kwa uongozi wa kijiji. Leo hii tuko nao uraiani lakini hawajulikani wanafanya kazi gani kujiingizia kipato. Wako ambao ni wema lkn wapo ambao ulikosekana tu ushahidi wa kuwatia hatiani katika mahakama za kiraia japo kwenye mahakama ya kijeshi walitiwa hatiani. Kitengo cha Intelijensia cha polisi kiimarishwe ili kukusanya taarifa sahihi za wahalifu na uhalifu wasijikite kutafuta tu taarifa za kiintelijensia pale kunapokuwa na mivutano ya kisiasa kuhusu maandamano na mikutano ya vyama vya siasa hasa hasa upinzani. Jeshi la polisi litambuliwe linakabiliwa na changamoto kubwa ya uhalifu wa kimakundi hasa uhalifu unaojikita kwenye mwavuli wa dini.

3. Mhimili wa mahakama nao utimize wajibu wao katika kutenda haki. Wasiwe wanatafuta visingizio vya dosari za kiufundi ili tu kumwachia mtu aliyepatikana na hatia ya wizi wa kutumia silaha. Jaji au Majaji wa mahakama za rufaa watazame ushahidi wa jumla kama una uzito kiasi gani badala ya baadhi yao kutafuta vidosari vidogo vidogo vya utaratibu wa uendeshaji wa kesi lower courts ili tu kuhalalisha kuwaachia watuhumiwa sugu wa ujambazi. Wajue wahalifu hawa iko siku watabisha hodi kwenye nyumba zao hata kama sio kwa Jaji au Hakimu aliyemwachia lkn hata kwa coleague. Uzoefu unathibitisha kuwa wengi waliofungwa miaka 30 kwa ujambazi wa kutumia silaha wanapoachiwa hurudi kujihusisha na uhalifu tena kama mwanzo alifungwa kwa kutumia kisu anaporudi hupanda daraja na kutumia bunduki au bastola.

4. Kuna haja ya kukiingiza cheo cha Balozi wa Nyumba kumi kumi kuwa chro rasmi cha kiserikali. Mtakumbuka baada ya sheria ya mfumo wa vyama vingi hawa walibakia kuwa viongozi wa CCM ambao huchaguliwa na mkutano mkuu wa Shina la CCM. Tutafute njia bora ya kupatikana kwao, kama ni kutumia utaratibu ule ule wa kumchagua mwenyekiti wa mtaa au wa kitongoji ni sawa ili awe na uhalali wa kuwa kiongozi wa kiserikali wa kusimamia nyumba hizi kumi. Ili mgeni yeyote katika hizo nyumba kumi lazima aandikishwe kwa balozi wa eneo husika ametokea wapi, amekuja kwa shughuli gani, mwenyeji wake ni nani na liwe sharti la lazima kuja na uthibitisho wa barua kutoka katika nyumba zile kumi anapotokea. Hii itasaidia kuwatambua watu wanaoletwa na kuhifadhiwa katika mitaa yetu halafu usiku wanakwenda kufanya uhalifu

5. Sisi kama raia hatujatimiza wajibu wetu kikamilifu kwa kufichua mipango ya uhalifu na wahalifu. Wala tusijitetee. Wahalifu hawa tunaishi nao na ni ndugu, jamaa na marafiki zetu. Pilikapilika za uhalifu zinaweza kuonekana katika mitaa yetu. Tuzitilie mashaka pilikapilika hizi hasa zinapohusisha wageni mitaani kwetu. Tusiguswe kufichua uhalifu tu pale tunapoguswa moja kwa moja kwa ndugu au jamaa kuuawa au kuporwa na hata kujeruhiwa. Tusisubiri kwa sababu uhai huwezi kuununua dukani.

Watanzania tukiamua, tunaweza kuupunguza uhalifu

Siku njema
HIVI UNAJUA KAZI ZA HAWA.
upload_2016-4-21_16-3-33.jpeg

MAJAMBAZI YAKIUA POLISI-HAZUNGUMZI.
ILA UA JAMBAZI ATATOA TAMKO REFU.
Human Rights
 
Nakubaliana na wewe. Kituo cha haki za binadamu kinapaswa kutazama pande zote za shilingi kama kinataka kionekane kinatenda haki. Raia wakiuawa na majambazi pia wanapaswa kupaza sauti zao ili kuibana serikali kuchukua hatua kwa vile hakuna mtu mwenye uhalali wa kutoa roho ya mtu. Lkn wakipaza sauti pale tu ambapo mtuhumiwa ameuawa na polisi wataonekana wana agenda fulani tu. Jukumu la kuhakikisha haki za binadamu zinaheshimiwa ni letu sote
 
Jambazi ni wa kuua tu .
Hao polisi wanasema tusichukue sheria mkononi ndiyo wanawapa bichwa
 
Kuna case moja hapa mtaani kwetu wezi walitusumbua miezi sita mfululizo. Tulitoa taarifa polisi lkn hatua zikawa hazichukuliwi. Siku moja saa 8:00 usiku wa manane mmoja wa majirani akawa anawahi kwenda kufungua maji kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji mpunga. Akakutana na watu watano wamebeba vitu mbalimbali kuanzia TV, Radio,Mito ya makochi na vitu vingine vya watu. Alipopiga kelele za wezi wakamgeukia wanataka kumuua maana walikuwa na mapanga. Yeye alikuwa na jembe. Akapambana nao akamkata mmoja ambaye alikuwa amebeba TV akaanguka chini. Walr wenzake walifanikiwa kumjeruhi kwa panga mkononi. Kutokana na kelele za yule bwana na kwa vile tulitikiswa sana na wezi, watu wengi walijitokeza kutoa msaada. Wale wezi wakakimbia wakimwacha mwenzao. Wananchi hawakumchelewesha. Walimtia kiberiti huku prmbeni kukiwa na TV yake hadi akabaki majivu. Cha ajabu polisi baadae walikuja kumkamata yule bwana aliyejieruhiwa na wale majambazi kwamba ndiye aliua yule jambazi wakati aliuawa na kundi la watu wenye hasira. Tulijiuliza sana, hivi polisi walitaka yule raia mwema ndio auawe? Hatukuwaelewa kabisa. Ni kweli kujichukulia sheria mkononi ni kosa la jinai lkn polisi wanapaswa kupima mazingira ya tukio lenyewe. Mtu alichomwa saa 8:00 usiku na kundi la wananchi utajuaje nani alikuja usiku ule kutoa msaada? Scenerio kama hizi kwa kweli huwavunja moyo raia wema
 
Hakuna mahali duniani hakuna uhalifu..Vatican kwenyewe kuna mauaji,wizi nk ndo iwe bongo.Papa John Paul wa I aliuawa ndani ya kuta za Vatican.Yesu mwenyewe alisulubiwa Enzi hizo na wakora kama Baraba,Cain alimkill Abel,the list is endless.uhalifu ni part ya human nature huwezi ufuta kabisa
 
Pointi yako ya 5 naipinga kabisa. Ukitaka kuishi kwa hofu maisha yako yote nenda polisi kawaambie kuwa unamjua jambazi fulani. Siku zako zitahesabika. Polisi hawa wetu wamejaa njaa tupu mpaka wanadiriki kuomba chakula kwetu (Mahotelini).
Wabadilishe na kulifumua kabisa kabisa hilo jeshi tangu mkuu mpaka yule instructor pale ccp. Hawafai. Zamani mtu akitaka kuingia jeshi la polisi alishushuliwa hadi kijijini na ukoo anaotoka. Kama kulikuwa na dalili za wizi kwao, hapati. Leo, kuingia ni pesa yako tu. Kujulikana kwa kiongozi yeyote wa polisi unaingia tu.
Sitaki kusema lakini ni kulifumua tu hilo jeshi kwanza, tuwaandae wengine au kuwachambua hao walioko mpaka turidhike nao. Intelijensia ya polisi isiwe tu kwa upinzani, wajipime weyewe kwanza.
 
Ugumu wa maisha pia usisahaulike kama kigezo cha kupambana na uhalifu umaskini pamoja na umaskini unachangia sana kushawishi watu kirahisi kufanya uhalifu kuliko kwa watu wenye kipato.
 
Majambazi ni JIPU kubwa - mheshimiwa liangalie na litumbue wananchi watii sharia hatuna raha
 
Pointi yako ya 5 naipinga kabisa. Ukitaka kuishi kwa hofu maisha yako yote nenda polisi kawaambie kuwa unamjua jambazi fulani. Siku zako zitahesabika. Polisi hawa wetu wamejaa njaa tupu mpaka wanadiriki kuomba chakula kwetu (Mahotelini).
Wabadilishe na kulifumua kabisa kabisa hilo jeshi tangu mkuu mpaka yule instructor pale ccp. Hawafai. Zamani mtu akitaka kuingia jeshi la polisi alishushuliwa hadi kijijini na ukoo anaotoka. Kama kulikuwa na dalili za wizi kwao, hapati. Leo, kuingia ni pesa yako tu. Kujulikana kwa kiongozi yeyote wa polisi unaingia tu.
Sitaki kusema lakini ni kulifumua tu hilo jeshi kwanza, tuwaandae wengine au kuwachambua hao walioko mpaka turidhike nao. Intelijensia ya polisi isiwe tu kwa upinzani, wajipime weyewe kwanza.
Si kila polisi unampa siri(intelligence), mpe polisi unayemfahamu vzr hizo taarifa na hakika utafurahia kazi nzuri
 
Usalama wa Taifa ni kama hawapo kabisa, matukio ya kiuhalifu(ujambazi, wizi, ubakaji, mauaji n.k) yanajulikana baada ya kutokea , hali iliyopelekea Polisi kuanzisha kitengo chao cha intelligence ambacho kiasi kikubwa kinajitahidi sana
 
Back
Top Bottom