KHALFANI 86
Member
- May 16, 2020
- 14
- 24
Kwa haraka haraka ukiangalia vyama vya upinzani vinakwama wapi utawaangushia lawa viongozi wa vyama vyao ,hii sio sahihi kabisa udhaifu unaoendelea kupatikana kwenye vyama hivyo unatokana na wanachama wenyewe wa vyama husika.
Leo hii unawaza kuhusu kutokea chama kingine kikubwa cha upinzani ambacho kitadhihirika uchaguzi mkuu wa 2020 ambacho kitakigaragaza chama kikuu cha upinzani kilichopo sasa ambacho ni CHADEMA ,Na wengi wanajua huu ndio muda wa kudondoka kwa CHADEMA alafu hao hao walioiunga mkono CHADEMA ndio hao hao watakiunga mkono hicho chama ambacho sintokitaja leo ila kwa wakati Mwingine. Anguko hilo ndio Uimara wa CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM), kawaida ya wanachama wa CCM huwa wako makini na mambo yao kuliko wanachama wa vyama vingine vya upinzani hii ndio siri ya UIMARA wa CCM.
Mfano muda huu wanachama wa vyama vya upinzani wote kwa ujumla wako macho kwenye mambo yanayoendelea CCM kuliko vile wanaangalia chama chao alafu baadae wanaanza kulaumiana Mwenyekiti wa milele akishafanya teuzi zake kuweka watu anaopanga wawepo kwenye nafasi anazoamua yeye. Hapo ndipo CCM inazidi kuimarika kutokana na udhaifu unaovikumba vyama vya upinzani katika kukikimbiza chama hiki tawala chama pendwa na chama kikubwa namba moja Africa na cha pili Duniani.
Leo hii unawaza kuhusu kutokea chama kingine kikubwa cha upinzani ambacho kitadhihirika uchaguzi mkuu wa 2020 ambacho kitakigaragaza chama kikuu cha upinzani kilichopo sasa ambacho ni CHADEMA ,Na wengi wanajua huu ndio muda wa kudondoka kwa CHADEMA alafu hao hao walioiunga mkono CHADEMA ndio hao hao watakiunga mkono hicho chama ambacho sintokitaja leo ila kwa wakati Mwingine. Anguko hilo ndio Uimara wa CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM), kawaida ya wanachama wa CCM huwa wako makini na mambo yao kuliko wanachama wa vyama vingine vya upinzani hii ndio siri ya UIMARA wa CCM.
Mfano muda huu wanachama wa vyama vya upinzani wote kwa ujumla wako macho kwenye mambo yanayoendelea CCM kuliko vile wanaangalia chama chao alafu baadae wanaanza kulaumiana Mwenyekiti wa milele akishafanya teuzi zake kuweka watu anaopanga wawepo kwenye nafasi anazoamua yeye. Hapo ndipo CCM inazidi kuimarika kutokana na udhaifu unaovikumba vyama vya upinzani katika kukikimbiza chama hiki tawala chama pendwa na chama kikubwa namba moja Africa na cha pili Duniani.