Vitu ambavyo vinasababisha Ardhi kumilikiwa na Miungu mingine kihualali
A. Damu
Ardhi inauwezo wa kutunza kumbukumbu, na kila kitu kinachofanyika kwenye Ardhi kinaingia kwenye kumbukumbu , Damu yoyote ya Mwanadamu hisopokuwa Damu ya Yesu inapoingia kwenye Ardhi , inanena kisasi na kisasi ambacho inachotangaza ni kisasi cha mauti na hakuna kitu cha kuondoa Damu kwenye Ardhi isipokuwa Damu yingine kumwagika
Ufunuo wa Yohana 6:10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?
Kisasi cha Damu, kwahiyo kunakomwagika Damu Ardhi inakuwa ni najisi kwa Mungu kunakuwa na adhabu ya laana na shetani anapata uhalali wa kumiliki na kutawala Ardhi Kwa njia ya laana ya Mungu hivyo ili kutoka hapa ni lazima kufanyika toba kwa Mungu
B. Maneno ya laana
Ardhi inatunza maneno ya laana, ulishawai kusikia mtu anakwambia utaona kama utapata mtoto Tena anaweka kihapo kwamba ukipata mtoto labda sio Mimi kijukuu cha flani? Kazi ya Ardhi ni kuandika , kwahiyo maneno kama hayo Yana anadikwa kwenye Ardhi, na Ardhi inakuwa Shahidi juu ya kile kitu kilichosemwa juu yako, ndio maana unashangaa yanakupata kama yalivyosemwa
Yeremia 22:29-30 Ee nchi, nchi, nchi, lisikie neno la BWANA. BWANA asema hivi, Andikeni habari za mtu huyu kwamba hana watoto, kwamba mtu huyu hatafanikiwa siku zake zote; maana hapana mtu katika wazao wake atakayefanikiwa, akiketi katika kiti cha enzi cha Daudi, na kutawala tena katika Yuda.
C. Madhabahu
Ardhi inabeba madhabahu, ulishawai kusikia MTU anapewa ilizi anakwenda kuchimbia kwenye eneo lake? Mahali popote ambapo mwandamu anakutana na Miungu hapo ni eneo la madhabahu
Kumbukumbu la Torati 12:1-2 Hizi ndizo amri na hukumu mtakazotunza kuzifanya katika nchi aliyokupa BWANA, Mungu wa baba zako, uimiliki, siku zote mtakazoishi juu ya nchi.
.
[2]Vunjeni kabisa mahali pote walipokuwa wakiitumikia miungu yao mataifa mtakayoyamiliki, juu ya milima mirefu, na juu ya vilima, na chini ya kila mti wenye majani mabichi;
:
Kumbukumbu la Torati 12:3
[3]nanyi zivunjeni madhabahu zao, zibomoeni nguzo zao, na maashera yao yateketezeni kwa moto, na sanamu za kuchonga za miungu yao zikateni; na jina lao lifutilieni mbali na mahali hapo.
And ye shall overthrow their .
E.Uovu
Ardhi inabeba uovu, kama eneo ambalo unakaa kuna Mambo ya uzinzi na uasherati yanafanyika katika eneo lenu, ujue kuna uovu kwenye eneo
Hosea 1:2 Hapo kwanza BWANA aliponena kwa kinywa cha Hosea, BWANA alimwambia Hosea, Enenda ukatwae mke wa uzinzi, na watoto wa uzinzi; kwa maana nchi hii inafanya uzinzi mwingi, kwa kumwacha .
Kuna maeneo umeskia yaani Mambo ya uzinzi hayajawai kuisha kwanini maeneo mengi ya vyuoni uzinzi unatawala , unaweza ukaenda binti mzuri kabsa na unashangaa Tu unajikuta umeshajiingiza kwenye uzinzi ? Kwa sababu Ardhi imebeba uovu, vitu hivi shetani anatumia kutawala Maisha ya watu.
Tutaendelea