Uhamisho na ndoa za watumishi wa umma

Andre02150

JF-Expert Member
Feb 2, 2010
332
129
Naomba msaada kwa wenye kuelewa sheria za kazi zinasemaje pale mtumishi (mwanamke) anapopewa uhamisho na mwajiri wake pasipo kuzingatia ndoa yake.

Hivi karibuni taasisi nyingi za umma ikiwemo TRA zimekuwa zikihamisha wafanyakazi na hivyo kupelekea kutenganisha familia. Kuna wanawake wenye ndoa na watoto wadogo wamejikuta wanahamishwa pasipo kuzingatia ndoa zao. Swali ninalouliza je sheria ya ajira inasemaje juu ya married couple? Nani anatakiwa amfuate mwenzie inapotokea uhamisho? Je mwajiri ana nafasi gani katika ustawi wa familia na jamii kwa ujumla? Hivi mwajiri anapohamisha watumishi na hatimae kutenganisha wanandoa haoni kama ameshindwa kumtendea haki mtumishi wake?

Nafikiri ni wakati muafaka kwa Serikali, taasisi za kijamii kuona umuhimu wa kuliangalia hili suala kwa macho ya ukaribu kwa ajili ya kujenga familia bora.
 
Siyo wote ila wengi wa watumishi inabidi wawe wanatoa taarifa zao sahihi ili kuepuka mambo kama haya... kuna wengine wanasema wana watoto tu ila hawajaoa au kuolewa... sijui wanafichaga nini...
 
Ni mmoja wa wahanga wa hii issue mke wangu yupo Tabora nimeomba uhamisho ahamie mbeya nambiwa atafute mtu wa kubadilishana ,asipopatikana ndio tutaendelea kuishi hivi kweli..nafikiria kufunga safari kwenda TAMISEMI kulallamika juu ya hili...maana psychologically ..naadhirika San..
 
Dah.... mbona kusoma Ulaya mnaenda bana na wanakuja kuwatembelea, sembuse Katavi?
 
Mkuu ajira yako uliajiriwa we we Na uhamisho una hamishwa wewe .Kama Mke in mtumishi nae aliajiriwa yeye Na atahamishwa yeye.Ushauri ukihamishwa wewe kule uendako katafute nafasi ya Kazi ya mkeo kama IPO mkeo aombe uhamisho kuja huko.
 
Tena mkubwa kwakuwa kama mtu aking'ang'ana kukataa uhamisho anaweza kukaa nyunbani bila malipo. Kumbuka mahali kama Dar pako highly congested
Kweli lakini. Kwa nini huwa hawaopt wao (spouses) kuhamishiwa mikoani kumfuata mwenza isipokua wa mikoani wahamishiwe dar?
 
Mkuu nimehamishwa Niko mbeya kwa ss..but ajira yake ilitok Tabora 3years now ,ninachozungumza hapa ameomba uhamisho wanamwambia hadi atafute mtu wa kubadilishana nae..
 
Kuna dawati la jinsia katika taasisi nyingi za uma kama TRA. ndo kazi zao.
 
Hili jambo linapotokea wanandoa wakapata psychological maumivu. Ni busara liwe jambo la kitambo kidogo huku unashughulikia uhamisho na kutafuta shughuli private kwa mwenza kama uhamisho utazingua.
 
Nenda F.15 pg 119 utapata majibu ya hoja yako
 

Attachments

  • Public Service Standing Orders.pdf
    1.8 MB · Views: 133
Ni mmoja wa wahanga wa hii issue mke wangu yupo Tabora nimeomba uhamisho ahamie mbeya nambiwa atafute mtu wa kubadilishana ,asipopatikana ndio tutaendelea kuishi hivi kweli..nafikiria kufunga safari kwenda TAMISEMI kulallamika juu ya hili...maana psychologically ..naadhirika San..
Hii ya kutafuta mtu wa kubadilishana naye siyo rahisi kivile. Jaribu mwenyewe kwenda TAMISEMI. Siyo rahisi mtu kukubali kubadilisha na mtu wa Tabora unless awe ni mwenyeji wa huko huko.
 
Back
Top Bottom