Uhamisho kwa watumishi wa umma

mputamaseko

JF-Expert Member
Apr 1, 2013
1,401
949

kumekuwa na kucheleweshwa kwa stahiki mbalimbali za watumishi wa umma tokea awamu hii hiingie madarakani kutokana na sababu mbalimbali , moja wapo wa haki zinazocheleweshwa ni hii ya uhamisho kwa watumishi wa umma kutoka kituo kimoja kwenda kituo kingine. Naomba kupitia uzi huu wadau mbalimbali wanao guswa tuutumie kuikumbusha serikali yetu kuwa kuna familia nyingi za watumishi ambao wanaonana mara mbili au tatu tu kwa mwaka, hii inasababisha msongo wa mawazo na inaweza kusababisha migogoro mikubwa sana ndani ya familia na jamii zetu. Naomba ifikie hatua viongozi wetu watambue kuwa wamechaguliwa kutumikia watu, muda mwingine wajivike uhusika wa watu wanao waongoza! Naomba serikali iruhusu uhamisho ili wafanyakazi waungane na familia zao popote pale walipo nchini.
Karibuni sana wadau tuchangie kistaarabu na kwa lugha ambayo sio ya kukwaza kikundi ama mtu yeyote. Wasalaam
 
Serikali inaongoza kuvunja ndoa zetu ,mkewangu kaomba kuhama toka 2015 taratibu zote zilishapita tunangoja kibali toka Dodoma.

Hatujui lini kitatoka maana yeye anabadilishana na mfanyakazi mwenziye
 
Kwa wale wanaobadilishana vituo nahisi changamoto nafuu ila kwa wale ambao wanaomba kuhamia sehemu fulani nasikia tetesi mpaka wahakiki idadi ya nguvu kazi na mahitaji.
Kuna mtu alikuwa anahamia mjini kumfuata mwenzi wake akajibiwa kuwa mwenye nyumba. Kasema hiyo kada wamejazana mjin kuliko mahitaji hata vijijini watu wapo kwa nn huyo mwenzi asimfuate kijijini?
Nikamshauri aende physical na viambatanisho waone uzito wa jambo ila hii ni tetesi kutokana na mhusika kujibiwa hivyo binafsi sijui kwa nini
 
Wote wanamuogopa le grand pere,atakaetoa tamko kuhusu uhamisho ataungana na bossi wa waya zilizopita majumbani na barabarani pamoja na mwana wa malechela,mnadhani nani anataka njia ya chooni iote nyasi?
 

kumekuwa na kucheleweshwa kwa stahiki mbalimbali za watumishi wa umma tokea awamu hii hiingie madarakani kutokana na sababu mbalimbali , moja wapo wa haki zinazocheleweshwa ni hii ya uhamisho kwa watumishi wa umma kutoka kituo kimoja kwenda kituo kingine. Naomba kupitia uzi huu wadau mbalimbali wanao guswa tuutumie kuikumbusha serikali yetu kuwa kuna familia nyingi za watumishi ambao wanaonana mara mbili au tatu tu kwa mwaka, hii inasababisha msongo wa mawazo na inaweza kusababisha migogoro mikubwa sana ndani ya familia na jamii zetu. Naomba ifikie hatua viongozi wetu watambue kuwa wamechaguliwa kutumikia watu, muda mwingine wajivike uhusika wa watu wanao waongoza! Naomba serikali iruhusu uhamisho ili wafanyakazi waungane na familia zao popote pale walipo nchini.
Karibuni sana wadau tuchangie kistaarabu na kwa lugha ambayo sio ya kukwaza kikundi ama mtu yeyote. Wasalaam
Kuna jamaa zangu wako Wizara ya Kilimo,Mifugo na Uvuvi walihamishwa vituo mwaka jana. Waliripoti vituo vipya ,hadi leo ni mwezi wa nane hata thumuni hawajalipwa. Cha ajabu zilikuwa hamisho za kawaida,iweje wasilipwe hadi leo? Au zimeliwa? Na kama Wizara yao ilikuwa haina pesa,kwa nini wawahamishe na kuleta usumbufu kwa familia zao? Mmoja wa hao,alipelekwa kituo na Mkoa kama Km 1400 kutoka kituo cha awali. Kaniomba nimshauri ,anataka kuacha kazi,ila nimempa wazo amwone Waziri husika amwelezee.
 
Kambi popote, Tanzania yote ni yetu sote, tuache kukimbilia mijini ilhali Vijijin huduma zinaendelea kuwa duni. Tuwahudumie Watanzania bila kujali wapo mijini ama Vijijin. Sifurahishwi na Uhamisho usiozingatia Uwiano wa Rasilimaliwatu. Watu wanaoenda Kigoma, Sumbawanga, Rorya, Mpanda, Mtwara, Lindi nk waende tu. Lkn hamisho nyingi watu wanaenda Dsm, Dom, Arusha na Mwanza. Tuache kuleta starehe kwenye Utumishi wa Umma. Tufanyekazi popote. Over
 
Kambi popote, Tanzania yote ni yetu sote, tuache kukimbilia mijini ilhali Vijijin huduma zinaendelea kuwa duni. Tuwahudumie Watanzania bila kujali wapo mijini ama Vijijin. Sifurahishwi na Uhamisho usiozingatia Uwiano wa Rasilimaliwatu. Watu wanaoenda Kigoma, Sumbawanga, Rorya, Mpanda, Mtwara, Lindi nk waende tu. Lkn hamisho nyingi watu wanaenda Dsm, Dom, Arusha na Mwanza. Tuache kuleta starehe kwenye Utumishi wa Umma. Tufanyekazi popote. Over

Da kuna watu mnatia hasira sana basi tu! Hivi we jamaa unafahamu adha ya kuishi na mwenza wako mbali??? Maisha yenyewe yako wapi, yaani nilipe nyumba, umeme, maji, chakula nk. na mke wangu hivyohivyo?! Kama issue ni hiyo kwa nini wasijitokeze wakatoa utaratibu mpya tuujue?? Halafu mtu unishawishi eti kiongozi fulani anahudumia bila kufuata vyama…… mbona walioteuliwa wanakula raha na wenza wao??
 
Mungu wangu nisaidie Rais wangu aingilie kati ili swala la uhamisho.

Rais wangu mpendwa tafaadhali baba yangu ingilia kati baba, niwe pamoja na mke wangu.

Chuo miaka mitatu, mimi ndio nimemsomesha. Kamaliza chuo kapangiwa sehemu tofauti na mimi nilipo. Sasa ni miaka sita baba nipo mbali na mke wangu.

Naomba usimamie baba Rais wangu uhamisho ufanyike, nakuhaidi baada ya mwaka ntatoa ajira kwa vijana 1000. Maana mimi na mke wangu tunamawazo ya kuwa mfano bora kwa vijana wenzetu.

Tusaidie baba yangu tuwe jirani na wenza wetu.
 
Kambi popote, Tanzania yote ni yetu sote, tuache kukimbilia mijini ilhali Vijijin huduma zinaendelea kuwa duni. Tuwahudumie Watanzania bila kujali wapo mijini ama Vijijin. Sifurahishwi na Uhamisho usiozingatia Uwiano wa Rasilimaliwatu. Watu wanaoenda Kigoma, Sumbawanga, Rorya, Mpanda, Mtwara, Lindi nk waende tu. Lkn hamisho nyingi watu wanaenda Dsm, Dom, Arusha na Mwanza. Tuache kuleta starehe kwenye Utumishi wa Umma. Tufanyekazi popote. Over
Soma thread vizuri! Naona comment yako na maudhui ya thread haviendani!
 
Kambi popote, Tanzania yote ni yetu sote, tuache kukimbilia mijini ilhali Vijijin huduma zinaendelea kuwa duni. Tuwahudumie Watanzania bila kujali wapo mijini ama Vijijin. Sifurahishwi na Uhamisho usiozingatia Uwiano wa Rasilimaliwatu. Watu wanaoenda Kigoma, Sumbawanga, Rorya, Mpanda, Mtwara, Lindi nk waende tu. Lkn hamisho nyingi watu wanaenda Dsm, Dom, Arusha na Mwanza. Tuache kuleta starehe kwenye Utumishi wa Umma. Tufanyekazi popote. Over
Sina uhakika kama umemwelewa mleta uzi.
 
Nashukuru sana mleta Uzi huu na wengine wanaumwa magonjwa ambayo yanahitaji kukaa karibu na hospitali Ila hawahamishwi mfano mtu mwenye pumu inakuwa shida sana
 
Hasa kama mume uko Mjini kwahiyo usiombe uhamisho wa mkeo kisa uko mjini jamani hivi mnajua kuishi mbali na mwenza wako na madhala yanayo weza kujitokeza yapo mengi sana Mf: single parent, magonjwa ya zinaa, kuvunjika kwa ndoa kabisa na nk Ombi langu viongozi husika wajaribu kuangalia kwa jicho la tatu malalamiko haya na wayafanyie kazi
 
Hili La Kuwa Mbali Na Familia Limetuathiri Sana Watumishi , Anyway ! Who Care?
Muda mwingine huwa najiuliza viongozi wetu wanajivunia nini kuongoza watu ambao wanachangamoto kibao na wao wanazifumbia macho ilhali ziko ndani ya uwezo wao kuzitatua.
 
Huu mwaka nahisi watu wengi has a watumishi Wa umma wataachana na kazi kwa kuwa hawaruhusiwi kuhama .
 
Back
Top Bottom