RABIN GHYOOT
Member
- Sep 17, 2014
- 10
- 2
Ukisoma "Tanzania Daima" la jumatatu, tarehe 15th September 2014 ukurasa wa mbele unaona kichwa cha habari "Migomo, maandamano bila ya kikomo nchi nzima", "Mbowe aonya sasa basi, amshukia Sitta."
Pia ukisoma "Tanzania Daima" la jumatano, tarehe 17th September 2014 ukurasa wa tano unaona kichwa cha habari "Maandamano yaiva" humo ndani kuna taarifa na nukuu "Taarifa kutoka Makao makuu ya Chadema na mikoani zinaeleza kuwa maandalizi ya maandamano ya amani na migomo isiyo na kikomo yenye lengo la kushinikiza kusitishwa kwa shughuli za Bunge Maalumu la Katiba inaendelea kukamilika."
Baada ya kusoma hizi taarifa naona CHADEMA wanachanganya vitu viwili tofauti "Migomo" na "Maandamano"
Ingekuwa haya magazeti hayamilikiwi na Mbowe na hawa waandishi hawakuajiriwa na Mbowe ningefikiri ni uzushi.
Kinachoshangaza katika mpango wa Mbowe ni "migomo". Kufanya au kuhamasisha migomo bila ya kuwashirikisha TUCTA ni uvunjifu wa sheria.
Ukiangalia sheria ya kazi na ajira unaona wanaoweza kugoma ni wafanyakazi kupitia vyama vyao, tena baada ya kupiga kura kwa mujibu wa katiba ya chama chao. Pale wengi wamepiga kura ya kuchagua kugome ndio mgomo unafanyika.
Section 80(1)(d) of Employment and Labour Relation Act 2004 inasema:
"employee may engage in lawful strike if the strike is called by trade union, a ballot has been conducted under the union's constitution and majority of those voted were in favour of the strike"
Kwahiyo kuitisha mgomo kwa namna yoyote nyingine ni kuvunja sheria.
Vilevile kuna makundi yanayotowa huduma muhimu yamekatazwa kugoma na sheria za nchi.
Kwa mfano makundi yanayotowa huduma za maji, umeme, afya, zima moto nakadhalika.
Kwahiyo Mbowe anavyo hamasisha kugoma bila ya kufafanua anavunja sheria za nchi.
Kwahiyo waislamu wanapohoji inawezekana vipi Mbowe anavunja sheria lakini anaachiwa huru, wakati Sheikh Ponda alipovunja sheria alitiwa ndani wana hoja ya msingi.
Je ni dhamana gani mtu anapewa ambayo masharti yake yanaruhusu mtu kutoka nje ya nchi? Basi hata Sheikh Ponda angepewa ili akimbie zake mpaka mambo yakipowa.
Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inazungumzia Mkusanyiko kama haki ya msingi ambayo pia inawajibu wake (duty).
Pia ukisoma "Tanzania Daima" la jumatano, tarehe 17th September 2014 ukurasa wa tano unaona kichwa cha habari "Maandamano yaiva" humo ndani kuna taarifa na nukuu "Taarifa kutoka Makao makuu ya Chadema na mikoani zinaeleza kuwa maandalizi ya maandamano ya amani na migomo isiyo na kikomo yenye lengo la kushinikiza kusitishwa kwa shughuli za Bunge Maalumu la Katiba inaendelea kukamilika."
Baada ya kusoma hizi taarifa naona CHADEMA wanachanganya vitu viwili tofauti "Migomo" na "Maandamano"
Ingekuwa haya magazeti hayamilikiwi na Mbowe na hawa waandishi hawakuajiriwa na Mbowe ningefikiri ni uzushi.
Kinachoshangaza katika mpango wa Mbowe ni "migomo". Kufanya au kuhamasisha migomo bila ya kuwashirikisha TUCTA ni uvunjifu wa sheria.
Ukiangalia sheria ya kazi na ajira unaona wanaoweza kugoma ni wafanyakazi kupitia vyama vyao, tena baada ya kupiga kura kwa mujibu wa katiba ya chama chao. Pale wengi wamepiga kura ya kuchagua kugome ndio mgomo unafanyika.
Section 80(1)(d) of Employment and Labour Relation Act 2004 inasema:
"employee may engage in lawful strike if the strike is called by trade union, a ballot has been conducted under the union's constitution and majority of those voted were in favour of the strike"
Kwahiyo kuitisha mgomo kwa namna yoyote nyingine ni kuvunja sheria.
Vilevile kuna makundi yanayotowa huduma muhimu yamekatazwa kugoma na sheria za nchi.
Kwa mfano makundi yanayotowa huduma za maji, umeme, afya, zima moto nakadhalika.
Kwahiyo Mbowe anavyo hamasisha kugoma bila ya kufafanua anavunja sheria za nchi.
Kwahiyo waislamu wanapohoji inawezekana vipi Mbowe anavunja sheria lakini anaachiwa huru, wakati Sheikh Ponda alipovunja sheria alitiwa ndani wana hoja ya msingi.
Je ni dhamana gani mtu anapewa ambayo masharti yake yanaruhusu mtu kutoka nje ya nchi? Basi hata Sheikh Ponda angepewa ili akimbie zake mpaka mambo yakipowa.
Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania inazungumzia Mkusanyiko kama haki ya msingi ambayo pia inawajibu wake (duty).