Uhaini wa Mtwara ulipangwa


Ntunga: Umenena mambo ya msingi kwa yeyote mwenye upeo na nia ya kuelewa.
Serikali yetu kwa sasa imekuwa na tabia ya kuwa na majibu mepesi kwenye maswali magumu, viongozi wetu wa serikali wamekuwa wavivu wa kufikiri na kutafuta suruhu ya hoja zilizo nzito kama hili suala la Mtwara sasa, bila kufikiri kwa umakini wanakurupuka na kuanza kulihusisha suala hili na siasa na hasa wakikinyooshea kidole CDM, mimi nasema huu ni uvivu wa kufikiri na kutoa majibu mepesi kwenye maswali magumu.
Mwl Nyerere aliweza kuiongoza na kuiunganisha nchi hii kwa sababu hakuwa mvivu wa kufikiri na hakuwa na majibu mepesi kwa maswali magumu, mkikumbuka vita ya Uganda (Amin) wakati wa Mwl. wanachi waliweza kuwa mstali wa mbele kupambana na Nduli Id Amin, watu walijitolea kwa hali na mali zao, enzi za Mwl aliposema siasa ni kilimo watu walikwenda mashambani, wananchi walifurahia kusikiliza hotuba za Mwl radioni nyakati zile watu walikuwa na shahuku ya kujua leo Mwl ataongea nini.
Mambo haya hayakuja tu hivi hivi, Mwl alikuwa na tabia ya kuwa pamoja na wanachi kwenye shida zao, alikuwa tayari kuwaelekeza wananchi kupenda kufanya kazi (kujitegemea), aliwaeleza wananchi wachukie aina yoyote ya udharimu, unyonyaji, wizi, rushwa, ufisadi na kila aina ya jambo lolote lisilo sawa. Mwl alipenda wananchi waelimike wawe na uelewa wa mambo.
Mwl hakuwaonea aibu wale wote watumishi wa serikali waliotumia madaraka yao vibaya (kujinufaisha)
Azimio la Arusha lilikuwa na maana yake, Mwl kafa akilililia, hakuwahi kujua ni kwa nini viongozi wetu walilifuta
Kwa kufanya hivyo wananchi waliipenda nchi/serikali yao na chama chao.

Tukubali tusikubali, CDM kwa sasa ndo wenye uwezo wa kuwajenga Watanzania, Watanzania wa leo kwenye mikutano ya CDM tumeona kwa roho nyeupe kabisa, kwa utashi, pamoja na ugumu wa hali kifedha, lakini wamekuwa wakichangia hizo hizo kidogo kidogo kujenga CHAMA (M4C), wengine wamekuwa wakibeza suala hili, ila lina maana kubwa sana kwa wananchi.

Leo hii kwa serikali hii haya yote hayapo tena (hivi utawaelezaje wananchi kilimo kwanza wakati wewe hulimi, unaiba tu fedha za umma) na viongozi wa serikali yetu hawana namna tena ya kuyatafakari haya (wamekuwa wavivu wa kufikiri), wamebakiwa kutoa majibu mepesi kwenye maswali magumu. Kila linalotokea wanadai ni siasa (suala la kuchinja wanasema ni siasa CDM, viongozi wa dini kushambuliwa wanasema siasa CDM, waandishi wa habari kushambuliwa wanasema siasa CDM, shambulio la Arusha wanasema siasa CDM, kila kitu ni CDM, hata leo hii tamko la serikali Bungeni (Nchimbi) kwa wenye kuelewa wameelewa kuwa alikuwa analenga CDM, haya ni majibu mepesi kwenye maswali magumu)
Kwani ufuaji wa hiyo Gesi ukifanyika hukohuko Mtwara kuna tatizo gani??????? Wanamtwara wanataka kwao huko ambapo Serikali imepaacha siku nyingi kimaendeleo nao wapate hivyo vyanzo vya ajira, mambo yajengwe huko huko. Wanamtwara hawajasema gesi iwanufaishe wao tu, hapana wanataka mambo yajengwe huko kwao, pawe na maendeleo.
Hivi kwa nini kila kitu iwe ni Dar tu??????? (au basi serikali iwe wazi tu tabia hizi za 10% kwenye mikataba ndo inawaletea shida, kwamba kuna kampuni ambayo tayari wameshakula 10% ya mkataba wa ujenzi wa Bomba Mtwara - Dar hivyo wanaona noma kuvunja mkataba huo, lakini kwa nini waingie makubaliano ya kusafirisha gesi kutoka Mtwara - Dar bila kwanza kuwashirikisha Wanamtwara????, hii ni tabia iliyojengeke ya kutowashirikisha wananchi kwenye maamuzi, ni jambo baya mno na gharama yake ni kubwa)
Serikali yetu ifikie sehemu iache kuwa wavivu wa kufikiri.

Suala la Mtwara ni jepesi sana ila Serikali imeamua kulikuza na sasa limekuwa kubwa sana.

Serikali ijenge mtambo wa kufua hiyo gesi hukohuko Mtwara, na mengine yote yaanzie huko na kuelekezwa kwingineko.

Kwa lazima kila kitu kiwe ni Dar tu???????
 

hivi wao ni watu zaidi kuliko kibanda, mwangosi na ulimboka? acheni unafiki.
 
Umetoa elimu ya kutosha mkuu.
"Those who make peaceful revolution impossible will make violent revolution inevitable". John F. Kennedy.
 
Yaani hujui kuwa ccm na viongozi wake ndo wanaoingia mikata isiyo na tija kwa wananchi?,wala rushwa?,wasiyoumia na ugumu wa maisha kwa watanzania?kwani hujui kuwa wao ndiyo wanaolazimisha kujenga bomba la gesi kutoka mtwara kwenda dar?,kwani hujui kuwa wao ndiyo wanasafirisha twiga pembe za ndovu kwenda nchi za nje?kwani hujui kuwa wao ndiyo wanaowakumbatia wala rushwa?kwani hujui kuwa wao ndiyo wanaotoa miongozo juu ya wananchi kubambikiziwa kesi ili kuwakomoa?
 
...Kuna maswali mengi sana ambayo watanzania na wanamtwa wanajiuliza na kujiuliza .. hakuna sababu ya kubahatisha.. wana mtwara wanaona kama vile hawaoni... madai halisi serikali inayajua ... cha msingi wasipuuzwe... wala wasionekane kama wehu au hawajui walifanyalo... kwa sasa watanzania walio wengi wana upeo wa mawazo.. wanajua kupambanua.. wanaelewa, na wanadadisi... narudia kusema madai ya wanamtwara serikali inayafahamu....Mungu aepushilie mbali hatari zaidi..
 

Mkuu watu hawapendi kuyasikia haya japo ndo ukweli. Nape ukimuuliza haya atakwambia ulete ushahidi, si kwamba hajui kwamba yapo na yanafanyika ila atakataa tu, kuwa ni uzushi.
Hawatufai tena hawa.
 
Inahitajika kukaa na wananchi na kusema nao kwa kina,, shida ya politicians ni kujaribu kuleta suluhu kisiasa badala ya kiuhalisia na inawezekana wananchi wa mtwara wanaona wamepigwa changa la macho Ktk ahadi za uchaguzi ndio wanakuwa mad. Kuhusisha na upinzani kisiasa ni kuhafifisha uwezo wa wananchi kufikiri na kuchambua mambo kwa kina yanayohusu maisha yao. Hilo ni kosa kubwa katika zama za ukweli, uwazi na maarifa kuongezeka hasa ya mawasiliano
 

Mkuu hapo kwenye red for your information hicho kitengo haki-deal na mambo hayo, kitengo hiki kwa sasa kina-deal na mambo ya ndani zaidi (Dr. Ulimboka, Kibanda nk)

Hapo kwenye blue, huwa ni kwenye masuala yanayohusiana na mikutano ya CDM tu na si vinginevyo.
Inakuwaje unataka kulaumu watu kwa kazi zisizo zao???????
 
Kwahiyo mulitaka wakiandamana waharibu na kupoga mali za wapinzani?

Hivi kweli mtu mzimq na akili yako unajiuliza kwa nini CCM? Yani Miaka 50 ya kuwatia umesikini hamuikumbuki?
 
hata kuiongoza familia y\huwezi wewe kama haya ndio mawazo yako.imepangwa na nani na umesikia wanamtwara for the past 2days walikuwa wanasubiri huyo sospeter aseme neno hapo ndipo walipojianda akili zakushikiwa
Nini wewe ungetarajia haswa ukiwakilisha mawazo yako na matarajio ya. watu wa kusini angesema Muhongo.
 
Kama na haya ya Mtwara bado tu tunamtafuta wa kumbebesha mzigo basi hakika katika CCM na Serikali yote basi hakuna watu wanaoweza kufikiri na kutenda inavyopaswa!!.. Na hili linatusikitisha sana wananchi na zaidi sana inatutia hofu mno na hakuna mwenye uhakika na usalama wake sasa!.

Binafsi mimi nashangaa sana mpaka sasa Rais hajafanya lolote linaloweza kuweka mambo sawa. Nilichokiona na kukisikia jana ni hotuba zilezile za Rais ambazo badala ya kutuliza mambo huamusha maswali yasiyo na majibu!!. Pili alipaswa kwenda Mtwara yeye mwenyewe mara moja na kutuliza mambo.

Mimi naamini Rais angefanya hivi, watu wa Mtwara watamsikiliza pamoja na udhaifu wake na watatulia. Na wakishatulia hapo ndipo wanaweza kuwaeleza watu ni nini mipango ya serikali A to Z..

Hebu CCM onesheni uongozi na uongozi si kulazimisha mnatotaka ninyi yafanyike tu. Shirikesheni watu katika maamuzi yenu, kila kitu kifanyike kwa ukweli na uwazi. Kwa kweli muda wa kuwahadaa watu na ahadi za uongo hauna nafasi tena katika zama hizi ambazo ufahamu wa watu juu ya mambo mbalimbali umeongezeka maradufu. Ni kujidanganya sana kutumia mbinu za uongozi wakale katika kutekeleza mipango na sera zetu.

Binafsi naona kabisa kuwa kama mfumo huu wa uendeshaji wa mambo yetu hautabadilika kuna hatari ya yaliyotokea Mtwara kutokea katika maeneo mengi ya nchi yetu siku za usoni!!!...
 
Serikali ya ccm taften chanzo cha tatzo, msikimbilie kulaum vyama vya upinzan, wananch wanachoma nyumban zenu kwasababu mmewasaliti na kuwasababishia maisha magumu. kama mtakimbilia kukilaum cdm ndo mtazd kujimalza kabisa wananch wamewachoka kbalini
 
kuna watu hum jf wanaandika tu kwasababu wamesajiliwa,hv mtu haoni umuhimu wa madai ya wanamtwara?hata kama hujasoma kuna mambo ambayo hayahitaji elimu hata ya chekechea kuyaelewa,tuache unafiki
 
kama wtz tutaendelea kumtafuta mbu wa malaria badala ya kinga ya malaria hatutaweza kutatua migogoro ya kijamii. Tatizo la mtwara si la jana lakini linatatuliwa kisiasa badala ya kutafuta suluhu ya kweli.
Naishauri serikali iendeshe midahalo huru kwa wananchi nchi nzima ili isikie wanasema nini halafu ndiyo ilaumu chama au kundi fulani. Naamini yanayotokea mtwara ni matokeo ya uchungu wa wananchi wa siku nyingi kiasi kwamba sasa umemwagikia; kikombe kimejaa hakuna namna zaidi ya kutafuta kuyapunguza ili yasiendelee kumwagika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…