Ugonjwa wa Tetekuwanga (Chicken Pox): Maambukizi, dalili, madhara na tiba

Gigo

JF-Expert Member
Aug 6, 2006
456
46
Kuna jamaa yangu ameugua ugonjwa wa tete kuwanga.Na yeye ni zaidi Ya miaka 14 sasa naona ameshamuambukiza kaka yake mwenye umri wa zaidi ya miaka 24. Nimepata wasiwasi huenda anayefuatia kuugua ni mimi,lakini nilishawahi kuugua kabla.

Je, naweza kuugua tena kwa mara ya pili?

Je, nini kinga na tiba ya ugonjwa wa tetekuwanga?

2. mama fulani anauliza..
Habari za mida hii wakuu! ndugu zangu naugua tetekuwanga kwa siku ya pili leo nimeenda hospital nimepewa dawa ya vidonge ambayo ni AMPICLOX na ya kuogea POTASIUM PEMANGANET zinanisaidia kiasi fulani maana muasho umepungua japo vipele vinaongezeka.

Sasa tatizo ninasikia zinaambukiza haraka sana na mimi nina mtoto wa miezi sita nanyonyesha.

Je, naweza kujikingaje ili nisiambukize wengine hasa huyu mtoto wangu mdogo maana nina homa kali sana naogopa sana yakimpata mtoto.


=========
Maoni na ushauri wa wadau




Tetekuwanga kwa Watoto


Ikiwa aikloviri itaanzishwa kwa masaa ya mwanzo wa vipele itapunguza dalili lakini haina athari kwa kiwango cha kutatiza. Kwa sasa basi, matumizi ya asikloviri haipendekezwi kwa watu wenye kingaimara (yaani, watu wenye siha bora wasio na upungufu wa kinga kwa sasa au wanaotumia tiba za udhibitikinga).


Matibabu ya tetekuwanga kwa watoto hulenga dalili wakati ambapo mfumo wa kinga hukabiliana na virusi. Huku watoto wadogo zaidi ya miaka 12 wakikata kucha na kuziweka safi ni sehemu muhimu ya matibabu kwa

vile wao huwa hatarini zaidi ya kukuna malengelenge yao. Watoto walio na umri wa chini ya miaka 12 lakini kuzidi mwezi mmoja hawafai kupata dawa za kuzuia virusi iwapo hawaugui ugonjwa wowote mwingine ambao unaweza kuwaweka katika hatari ya kupatwa na matatizo.


Ili kuepuka kuishiwa na maji mwilini ,unywaji wa kiasi kikubwa cha maji unashauriwa hasa iwapo mtoto atapatwa na homa. Homa au maumivu ya kichwa yanaweza kupunguzwa kwa dawa za kupunguza maumivu

kama vile parasetamoli au ibuprofeni. Watoto ambao ni wakubwa kuzidi mwaka mmoja wanaweza kupewa vidonge vya antihistamini au dawa za maji ambazo kusaidia wakati ambapo mtoto hawezi kupata usingizi kwa sababu ya kuwashwa.


Asikloviri au kingaglobulini kwa jumla huagizwa kwa watoto walio katika hatari ya kukumbwa na matatizo yatokanayo na tetekuwanga . Wao hupokea matibabu sawa na iliyotajwa hapo juu kuongezea na dawa dhidi

ya virusi. Kategoria za watoto wanaoonekana kuwa katika hatari ya kupatwa na matatizo ni pamoja na watoto wachanga wa chini ya umri wa mwezi mmoja, walio na mfumo wa kinga hafifu, wale ambao hutumia steroidi au

dawa za kudhibiti kinga au watoto walio na magonjwa sugu ya moyo, mapafuna ngozi. Aidha, watu wazima na vijana huchukluliwa kuwa katika hatari ya kupata matatizo na kwa kawaida hupewa dawa ya kuzuia virusi.


Aspirini haikubaliki sana kwa watoto wadogo wa chini ya miaka 16 kwa vile imekuwa ikihusiana na uwezekano wa hali mbaya na hatari ijulikanayo kama dalili za Reye.
 
Chicken pox, is a highly contagious viral infection.

Chicken pox is acquired by direct contact with infected blister fluid or by inhalation of respiratory droplets.

In addition to affecting the skin, chicken pox can also cause lesions on the mucous membranes in the eyes, mouth, and ******.

Mara nyingi huwa ni kwa watoto under 14, japokuwa kama hujawahi kuugua utotoni chance ya kuugua ukubwani is high.
 
Kwani wewe ni mara ya kwanza kuwa exposed na chicken pox? kama hujawahi kuwa exposed wala kuugua, yes may be, lakini pia inategemea na immunity yako.

Severity ya disease pia ni individual, wengine wanaweza kuugua sana na wengine just one rash n.k

Surua na tetekuwanga zote ni viral diseases.
 
Wakuu naomba kufahamu kati ya calamine lotion na elyvate betamethazone valerate ointment,ipi nzuri kwa mgonjwa wa tetekuwanga?ipi inapönyesha haraka?inachukua muda gani kupona?maana hapa mwili unawasha
 
Wakuu naomba kufahamu kati ya calamine lotion na elyvate betamethazone valerate ointment,ipi nzuri kwa mgonjwa wa tetekuwanga?ipi inapönyesha haraka?inachukua muda gani kupona?maana hapa mwili unawasha

Mkuu, kwanza pole kwa kuwashwa na mwili. Lakini napenda kukuuliza maswali machache kabla ya kukufahamisha dawa sahihi ya tatizo lako.
1: Je diagnosis yako 'tetekuwanga' ni sahihi?
2: Umejuaje tatizo lako la kuwashwa mwili ni tetekuwanga?
3: Je, tatizo lako limeanza lini?
4: Mbali na kuwashwa mwili , Je kuna tatizo lingine limejitokeza?
 
1. Ndyo tetekuwanga mkuu.
2. Nimeenda hospitali ndyo Wameniambia hvyo.
3. Siku tatu zilizopita.
4.vipele fulan hv kama malengelenge,ndyo vinawasha.
N.b
hospital jana waliniambia dawa hamna ila nikanunue moja wapo kati ya hzo
 
1. Ndyo tetekuwanga mkuu.
2. Nimeenda hospitali ndyo Wameniambia hvyo.
3. Siku tatu zilizopita.
4.vipele fulan hv kama malengelenge,ndyo vinawasha.
N.b
hospital jana waliniambia dawa hamna ila nikanunue moja wapo kati ya hzo

Chickenpox (tetekuwanga) ni ugonjwa unaosababishwa na virus. Self limiting. Mara nyingi inasumbua watoto. Inapotokea kwa mtu mzima au immunocompromised, Mara nyingi ugonjwa unakuwa mkali (severe). Kwahiyo kutokana na swali lako, tumia Calamine Lotion. Re-apply the lotion 12 hourly . Utapona
 
Shukrani mkubwa,maana nilikuwa napaka zote,ngoja niache h moja
 
Nakubaliana na wewe Mkuu,
Lakini pia unaweza kunywa, antihistamine kama Piriton(R), kupunguza makali ya kuwasha!



 
Mdogo wangu ametokwa na vipele viduchuviduchu yan kama vya joto sio hata maaana vimeabza juz bt leo mwili mzima anawashwa anajikuna amevimba hadi uson, miguun yan mwili mzima analia tuu sa jana alipelekwa dispensary eti wakamwambia kuwa ni dalili za surua vt then wakasema sio na wakampatia dawa ya mebendazole n alerid-d sijuihata if ni sahihi au laah jamn mwenye upeo maana icant stand seeing him anlia nakujikuna hivoo
 
Mkuu hiyo ni alergy kuna kitu atakuwa amekula,mimi mtoto wangu vilimtokea Ijumaa iliopita mara baada ya kula samaki yaani ndani ya masaa mawili vilitokea mwili mzima na vikawa vinamuwasha mpaka akawa analia nika muwahisha hopitali wakampiga sindano ya mkononi,akapewa vidonge vya alergry jina nimesahau,erythromycin,calamine lotion na mimi mwenyewe nikamnunulia piriton ndio ikwa nafuu yake na mpaka juzi akawa amepona kabisa,nijulishe unaishi maeneo ya wapi inawezekana tunaishi eneo moja ili nikuelekeze hiyo hospitali.
 

Nipo hapa airpot dear kuvuka reli dar
 
Huyo mdogo wako ana umri gani? Kwa sababu surua huwapata watoto ila tetekuwanga kama hukuugua utotoni basi hata ukubwani unaweza kupata. Je macho yake ni mekundu?
 
Kama utaweza nenda pale Mbezi mwisho(Morogoro road) kuna Hospitali inaitwa Kipasika otherwise nenda pale ukonga Hospitali ya karibu na recreation centre-Bar ya Magereza jina limenitoka iko barabarani ulizia madereva Tax watakuelekeza.
 
Huyo mdogo wako ana umri gani? Kwa sababu surua huwapata watoto ila tetekuwanga kama hukuugua utotoni basi hata ukubwani unaweza kupata. Je macho yake ni mekundu?

Yupo std 5 n yan kaharibika sidhan kama tetekuwanga coz ni vipele vidogoooooooo sana
 
kama utaweza nenda pale Mbezi mwisho(Morogoro road) kuna Hospitali inaitwa Kipasika otherwise nenda pale ukonga Hospitali ya karibu na recreation centre-Bar ya Magereza jina limenitoka iko barabarani ulizia madereva Tax watakuelekeza.

Iliopo ukonga madafu ile ya kanisani kipenzi? Mana maskin alitaka kusafiri mwenyewe akapumzike likizo hii bt ndo ivo yabid asiende basi ntafanya hivo my dear mana sion any improvement na hizi dawa waliompatia
 
Iliopo ukonga madafu ile ya kanisani kipenzi? Mana maskin alitaka kusafiri mwenyewe akapumzike likizo hii bt ndo ivo yabid asiende basi ntafanya hivo my dear mana sion any improvement na hizi dawa waliompatia

Ndio hiyo,wahi ikiwezekana nenda leo vinatesa sana,nimekuhurumia kwani vilinifanya siku mbili nikae nyumbani bila kwenda kazini nikimliwaza kwani alikuwa almost kachanganyikiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…