Afadhali ufisadi wa kuiba fedha (nasema kwa namna ya kifisadi) kuliko wa 'SUTI' jamani! Hivi nchi hii ni kama sote tumerogwa! Viongozi wetu wamekuwa vipofu, viziwi na wenye kiburi cha madaraka kuliko hata mobutu! Halafu mijadala kama hiyo mama makinda haitaki maana amewekwa hapo kwa maslahi ya chama siyo ya taifa. KAGODA, MEREMETA, RICHMOND, KASHFA YA RADA, MENO YA TEMBO, MIKATABA MIBOVU, AJIRA ZA UPENDELEO KWENYE TAASISI NYETI,......Haya! kifo Daudi Balali ndiyo funga kazi! CCM kiboko kwa uhalifu. Lakini hadi lini? Pale mtz atakapoacha kusikiliza ujinga wa mtu kama Mwigulu ambaye kazi kubwa siyo kujenga hoja bali kununua na kurubuni wanachama wa chama cha cdm wakati hao wanajiunga kwa hiari baada ya kuona kazi nzuri ya chama husika. BADO KITAMBO KIDOGO MABADILIKO YA KWELI YATATOKEA na ccm watashangaa kuona waliyemuita msaliti anaingia ikulu, kama wanabisha wakamuulize Dr salmin Amour a.k.a KOMANDOO dhidi ya kina maalim na kundi lake. Ukweli ni kwamba huwezi kuzuia mabadiliko wakati unapokuwa umetimia. PEOPLEEEEES...aluta continua