ufafanuzi utumishi

ufafanuzi utumishi

Will i.a.m

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2012
Posts
347
Reaction score
49
yeyote mwenye ufafanuzi juu ya majina yalitolewa leo na PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT - PSRS je ni majina ya barua za maombi zilizoandikwa kwa kingereza au ni za kiswahili mssaada tafadhali maana iomeibuka sitofahamu kwa baadhi ya watu amabo wanadhani kua kuna majina mengine yatatangazwa mmoja wapo ni mimi
 
10. Wale ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa
maombi yao hayakufanikiwa na wasisite kuomba tena mara nafasi za kazi
zitakapotangazwa.
 
10. Wale ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa
maombi yao hayakufanikiwa na wasisite kuomba tena mara nafasi za kazi
zitakapotangazwa.
matangazo yalikua mawili la kikengereza na kiswahili so hii ni genaral au ni
specifical
 
Nahisi majina yaliyotoka ndo hayohayo hakuna mengine na mbona maelezo yao yanajitosheleza kwasababu wamesema kwenye hiyo document kwamba ambao hawataona majina yao watambue kuwa maombi yao hayakufanikiwa hivo wajaribu tena wakati mwingine waonapo matangazo.
 
matangazo yalikua mawili la kikengereza na kiswahili so hii ni genaral au ni
specifical

Mkuu labda wadau wengine watakupa ufafanuzi bt me nili2mia lile tangazo la kiingereza na nimeona nafac zote walizotangaza zipo. Cjui kwenye tangazo la kiswahili kama hizo posts zipo au vp.
 
kuna baadhi ya nafasi hawajaita watu kwenye usaili sasa sijui wote walioomba hawakuwa na vigezo au ni kitu gani?
 
binafsi naona nafasi zote zilizoitwa ni tangazo la kiingereza. Nimejaribu kuulizia wadau hakuna anayefahamu! Ila wataitwa wengine!!
 
jaman anaeweza kunihelp kuchek jina la csta yangu anipm coz niko xul bwen so kupata net ishu.hapa na2mia 4n
 
Nahisi majina yaliyotoka ndo hayohayo hakuna mengine na mbona maelezo yao yanajitosheleza kwasababu wamesema kwenye hiyo document kwamba ambao hawataona majina yao watambue kuwa maombi yao hayakufanikiwa hivo wajaribu tena wakati mwingine waonapo matangazo.

Siyo kweli. Asubuhi kulikuwa na document moja tu, lakini muda huu wame upload nyingine kwa wale walioomba Mzumbe University.
Usipotoshe kama huna uhakika!
 
yeyote mwenye ufafanuzi juu ya majina yalitolewa leo na PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT - PSRS je ni majina ya barua za maombi zilizoandikwa kwa kingereza au ni za kiswahili mssaada tafadhali maana iomeibuka sitofahamu kwa baadhi ya watu amabo wanadhani kua kuna majina mengine yatatangazwa mmoja wapo ni mimi

Waombaji wa nafasi za kazi Serikalini kwa tangazo lililokuwa limetolewa tarehe 26 Machi, 2013 kupitia Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ambalo mwisho wa kutuma maombi ilikuwa terehe 9 Aprili, 2013 wametakiwa kuangalia majina yao katika tovuti ya Sekretarieti ya Ajira kuanzia tarehe 13 Mei mwaka huu ili kujua endapo wamechaguliwakwa ajili ya kufanya usaili wa nafasi walizoomba. Naibu Katibu wa Sekretarieti ya Ajira Bw. Lucas Mrumapili amesema ofisi yake imepokea jumla ya barua za maombi ya kazi 20,763 ambazo mchanganuo wake kwa tangazo la Kiingereza imepokea barua za maombi 6,332 na kwa tangazo la Kiswahili imepokeabarua za maombi 14,431 ambapo Ofisi yake iko katika hatua za mwisho za kukamilisha uchambuzi wa maombi hayo ili kuweza kuendelea na zoezi la usaili. Mrumapili amebainisha kuwa kwa tangazo la Kiingereza lililokuwa na nafasi wazi 185 ni kwa ajili ya Waajiri kutoka katika Taasisi za Umma zifuatazo; Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (NAO), Chuo Kikuu Mzumbe (MU), Chuo cha Serikali za Mitaa (LGTI), Wakala wa Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA), Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI), Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Taasisi ya Chakula na Lishe Tanzania (TFNC), Taasisi ya Utafiti wa Misitu Tanzania (TAFORI), Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori (TAWIRI), Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA), Chuo cha Mafunzo ya Ufundi Arusha (ATC), Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO), Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Amewataja Waajiri kuwa ni pamoja na Chuo cha Utumishi wa Umma (TPSC), Wakala wa Huduma za Ufundi na Umeme (TEMESA), Kituo cha zana za Kilimo na Ufundi Vijijini (CAMARTEC), Chuo cha Maji (WDMI), Chuo cha Mipango Dodoma(IRDP), Chuo cha Takwimu cha Afrika Mashariki (EASTC), Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi (TAFIRI), Taasisi ya Magonjwa ya Mifupa Muhimbili (MOI), Chuo cha Bandari Dar es Salaam (DMI), Wakala wa Mafunzo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Taasisi ya Ustawi wa Jamii (ISW), Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere (MNMA), Wakala wa Serikali Mtandao (eGA), Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB) pamoja na Chuo cha Diplomasia na Uhusiano wa Kimataifa (CFR). Amesema kwa upande wa Tangazo la Kiswahili lilikuwa na nafasi wazi 949 ambapo Waajiri wake ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Katibu Mkuu wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi na Ushirikiano wa Kimataifa, Afisa Mtendaji Mkuu Wakala wa Vipimo, Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Katibu Mkuu Wizara ya Kazi na Ajira, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Chakula na Ushirika, Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda na Biashara. Katibu Mkuu Wizara ya Sayansi na Technolojia, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Katibu Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Makazi, Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Katibu Ofisi ya Rais Maadili, Wengine ni Katibu Tawala wa Mkoa Kagera, Iringa, Ruvuma, Mbeya, Mwanza, Shinyanga, Manyara, Dar es Salaam, Morogoro, Geita, Pwani, Mara, Kilimanjaro, Lindi, Singida, Tabora, Tanga, Katavi na Arusha, Mkurugenzi Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Mkurugenzi Halmashauri Manispaa Iringa, Songea, Shinyanga, Morogoro, Singida, Kigoma/Ujiji na Temeke. Nafasi nyingine ni kwa ajili ya Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya Mufindi, Kyela, Rungwe, Mbeya, Chunya, Biharamulo, Bukoba, Muleba, Namtumbo, Songea, Morogoro, Makete, Mkuranga, Mbinga, Tunduru, Ukerewe, Sengerema, Ilemela, Busega, Maswa, Meatu, Shinyanga, Kishapu, Kilosa, Msalala, Rufiji, Rorya, Ruangwa, Lushoto, Mkinga, Mpanda, Monduli, Ngorongoro,Kigoma, Nachingwea, Rombo, Same, Singida, Urambo, Tabora, Babati, Mbulu, Simanjiro, Kiteto, Handeni, Pangani, Kibondo, Chamwino, Mtwara, Nanyumbu, Mpwapwa, Kongwa naTandahimba. Mkurugenzi Halmashauri ya Mji Njombe, Kibaha, Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) na TEMESA. Aidha, amewataka waombaji na wadau wengine kurejea Matangazo ya nafasi za kazi yaliyokuwa yametolewa tarehe 26 Machi, 2013 ili kujikumbusha kuhusu nafasi husika zilizokuwa zimetangazwa. Alimalizia kwa kusema kuwa waombaji ambao hawataona majina yao pindi majina yatakapotangazwa wajue hawakufanikiwa kutokana na kutokukidhi vigezo vya tangazo kwa nafasi husika walizokuwa wameomba, hivyo wasisite kuomba kwa mara nyingine pindi nafasi hizo zitakapotangazwa tena.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini.
Ofisi ya Rais-Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma. 30 Aprili, 2013. Kwa maelezo zaidi; wasiliana na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
kwa Barua pepe; gcu@ajira.go.tz au Simu; 255-687624975
 
tuli mda unavyozidi kwenda wana update ukiangalia kwa makini asubuhi lilikuwepo moja sasa yako mawili so endelea kusubiri mkuu....
 
Sasa mbona hawaupload hizo document za majina???????? Na matangazo hata mda haujaisha wameyatoa!!!! Hawa vp??????
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom