sirluta
JF-Expert Member
- Nov 28, 2012
- 6,325
- 2,491
Wasalaam wanabodi,
Awali ya yote kama tujuavyo kuna msemo unasema kila kitu kina pande mbili yaani (+ve) na (-ve), hivyo hata Udikteta kuna Udikteta +ve na Udikteta -ve.
Tujadiliane Udikteta +ve katika mahusiano ambao lengo lake ni kuimarisha mahusiano. Je ni kweli unaimarisha ama unabomoa?
Chukulia mfano umeoa (ke) ambaye utambana na kumfuatilia kila hatua anayotoka, lakini pia chukulia umeoa (ke) lakini unamwacha free bila kumfuatilia chochote, anarudi muda anaotaka, kwako kila kitu sawa ilimradi unampa uhuru wote na unamtrust kwa kila afanyalo na kila anapokwenda.
Japo wanasema "Bwana asipolinda nyumba, alindae akesha bure", lakini too much freedom inaweza kuleta madhara makubwa kwani kuna wasichana ambao walilelewa kidikteta na wazazi wao ndo wakatulia kwa wazazi, sasa unapomwoa ukimpa uhuru ndipo uhuru huo unaweza ukatumika vibaya na ukaleta madhara baadae kwakuwa hajauzoea.
Lakini pia kuna wasichana walizoea kuishi kwa uhuru wakiwa kwa wazazi wao, ila akiingia kwenye ndoa anakumbana na dikteta ambaye hata kama unaenda kununua vocha lazima upangiwe muda wa kwenda na kurudi.
Tudadavue : udikteta unaimarisha mahusiano ama unayaharibu? Karibuni.
Awali ya yote kama tujuavyo kuna msemo unasema kila kitu kina pande mbili yaani (+ve) na (-ve), hivyo hata Udikteta kuna Udikteta +ve na Udikteta -ve.
Tujadiliane Udikteta +ve katika mahusiano ambao lengo lake ni kuimarisha mahusiano. Je ni kweli unaimarisha ama unabomoa?
Chukulia mfano umeoa (ke) ambaye utambana na kumfuatilia kila hatua anayotoka, lakini pia chukulia umeoa (ke) lakini unamwacha free bila kumfuatilia chochote, anarudi muda anaotaka, kwako kila kitu sawa ilimradi unampa uhuru wote na unamtrust kwa kila afanyalo na kila anapokwenda.
Japo wanasema "Bwana asipolinda nyumba, alindae akesha bure", lakini too much freedom inaweza kuleta madhara makubwa kwani kuna wasichana ambao walilelewa kidikteta na wazazi wao ndo wakatulia kwa wazazi, sasa unapomwoa ukimpa uhuru ndipo uhuru huo unaweza ukatumika vibaya na ukaleta madhara baadae kwakuwa hajauzoea.
Lakini pia kuna wasichana walizoea kuishi kwa uhuru wakiwa kwa wazazi wao, ila akiingia kwenye ndoa anakumbana na dikteta ambaye hata kama unaenda kununua vocha lazima upangiwe muda wa kwenda na kurudi.
Tudadavue : udikteta unaimarisha mahusiano ama unayaharibu? Karibuni.