UTANIPENDA
Member
- Feb 25, 2012
- 31
- 12
kushindwa kwa CCM Arumeru hakikuwa kipimo cha kuwa CCM wamekuwa dhaifu... na wala kushindwa kwa CHADEMA Kalenga sio kipimo cha udhaifu wa CHADEMA.
CHADEMA ipo na shida kubwa sana ya msingi ya uwezo wa viongozi wa ngazi za chini hasa kwenye kata na wilaya. Kwa siasa za hivi sasa ambapo CCM wanafanya siasa za kila namna huku wakisaidiwa na mfumo huu mbovu ili ashinde kwa kweli kwa aina hii ya viongozi wa ngazi za chini, wananunulika kirahisi, waoga hata wakigombezwa na balozi wa CCM unakuta mwenyekiti wa chadema anafyata mkia, yaani hamna kitu kabisa wanafurahia kuitwa viongozi wa chadema lakini hawafanyi kazi yoyote ya siasa.
Udhaifu huu uliopo kwenye uongozi wa chini unapelekea uongozi wa juu kuelemewa na kuonekana dhaifu.
Kuongoza chama cha siasa ni kazi kubwa sio kama wanaJF tunavyobeza beza kienyeji enyeji. MBowe na sekretariat ya chadema wanajitahidi sana na huu ndio uimara wa chadema, tatizo huko chini hakuna viongozi wenye uwezo, yaani wana shida nyingi sana.
CHADEMA ipo na shida kubwa sana ya msingi ya uwezo wa viongozi wa ngazi za chini hasa kwenye kata na wilaya. Kwa siasa za hivi sasa ambapo CCM wanafanya siasa za kila namna huku wakisaidiwa na mfumo huu mbovu ili ashinde kwa kweli kwa aina hii ya viongozi wa ngazi za chini, wananunulika kirahisi, waoga hata wakigombezwa na balozi wa CCM unakuta mwenyekiti wa chadema anafyata mkia, yaani hamna kitu kabisa wanafurahia kuitwa viongozi wa chadema lakini hawafanyi kazi yoyote ya siasa.
Udhaifu huu uliopo kwenye uongozi wa chini unapelekea uongozi wa juu kuelemewa na kuonekana dhaifu.
Kuongoza chama cha siasa ni kazi kubwa sio kama wanaJF tunavyobeza beza kienyeji enyeji. MBowe na sekretariat ya chadema wanajitahidi sana na huu ndio uimara wa chadema, tatizo huko chini hakuna viongozi wenye uwezo, yaani wana shida nyingi sana.