Jumuiya ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDASA) imesikitishwa sana na tabia za baadhi ya Watumishi wa Serikali wanaochelewesha kwa visingizio visivyoeleweka malipo kuhusu stahiki mbalimbali za WanaUDASA
Kwa miaka 3 sasa Wanataaluma wanaostahili kulipwa posho ya nyumba ya kuishi (kwa mujibu wa standing orders for the public service 2009, section L, L.34 hadi L36 na Section M)
Kwa UDSM pekee Wanataaluma wanaidai Serikali kiasi cha za Kitanzania Bilioni 6, 272,357,696.00 ambalo ni deni la kuanzia Januari 2014 hadi Septemba 2018
Deni hili linaendelea kuongezeka kila mwezi ilhali hakuna maji ya kueleweka kutoka kwa wahusika
Wanataaluma wa UDSM wanaidai Serikali kiasi cha zaidi ya Shilingi Bilioni 5 kama malipo ya nyongeza ya mishahara (arrears). Baada ya malalamiko Juni mwaka jana WanaUDASA 102 walilipwa lakini 1060 hawakulipwa
"Zoezi hilo la ulipwaji lilikuwa na viashiria kama vya kutaka kuwaziba midomo baadhi ya wanajumuiya"
Kwa miaka mitatu Wanataaluma wanaokidhi vigezo hawapandishwi madaraja na waliopandishwa baada ya kuongeza elimu hawaongezewi mishahara
Pia kuna wana watumishi walioajiriwa 2017 hawakulip wa mishahara kwa muda wa miezi 5 na hadi sasa hawajalipwa
Hivyo UDASA tunashauri yafuatayo.
Serikali ilipe mara 1 malipo yote ifukapo Februari 2019.
Serikali ianzishe utaratibu wa kuambatanisha malipo ya posho ya nyumba kwa wanaostahili pamoja na mishahara yao
Ofisi ya Utumishi wa Umma iwapandishe mara moja Wanataaluma vyeto vipya na ianze kuwalipa mishahara inayoendana na vyeo hivyo
Kinyume na hapo Serikali itakuwa imetangaza mgogoro na Wanataaluma. Mgogoro huu utatulazinisha WanaUDASA kuondoa nguvu yetu kwenye majukumu yetu
Dkt. George Leonard Kahangwa
Mwenyekiti wa UDASA