Ndugu zangu watanzania poleni na hongereni kwa pilika pilika za msimu wa sikukuu!
Nimekuwa na kero ya muda mrefu kuhusu hizi school bus wanazopanda watoto wetu.
Kuna baadhi ya shule ambazo wanafunzi hubebwa kwa bus na hizo bus nyingi hazina hadhi ya kubeba watoto kwasababu ya ubovu na uchakavu.
Tupo kwenye kipindi ambacho watoto wetu wanafungua shule, tuwalinde na kuhakikisha hawapandishwi magari mabovu.