Ubongo wenye chuki

krenea

JF-Expert Member
Joined
Apr 3, 2014
Posts
405
Reaction score
160
Wasalaaam,

Ndugu wanajamvi leo tujadili suala hili.

Imekuwa kawaida kwa watanzania wengi kuwa na chuki mioyoni mwao ata kuwa na mtazamo hasi juu ya mafanikio ya maisha yao na ya wengine kwa ujumla.

Utakuta mtu anahold kumbukumbu mbaya au ya kusikitisha ya maisha ya mtu fulani na wakati wote anaileta katika sifa/mafanikio ya mtu husika.sikatazi historia kutajwa ila nazungumza mtu kuileta katika hali ya kubeza na kutaka kufififsha sifa.

Mfano yakitajwa mafanikio ya mtu lazima atokee wa kubeza kwa kutaja historia mbaya/ya kuuzunisha ya mtu huyo mfano " usimuone hivi zamani alikua ana sota mpaka ananiomba nauli" au yule anaye olewa si alikua ana megwa na fulan na bra braaaa nyingiii.
au nilisoma nae akafeli na kwenda kusoma kwingine ili mradi tu ataje kitu negative.au usiwaone hivi mama yao kawasomesha kwa kuuza visheti nk. Au anajidai kashika dini wakati alikua mlemvi.

Ata ukikutana na mtu alokufahamu ukiwa mdogo utakuta anasema we ulikua unalia wewe.au ulikua mwembamba sana au ulikua mtundu ndo umekua mama/baba?

Mara nyingi maneno haya usemwa kwa lengo la kuififisha sifa tajwa ya wakati huo.utasikia alikua anaishi Tandale ooooh alikua kachoka mpaka mtu ana google picha zake za zamani na nia hasa si kingine bali ni kutaka kufifisha sifa.

Maisha yanabadilika na binadamu pia wanabadilika kwanini usifurahi mtu anapopata kufanikiwa? kwani lazima utaje kitu flani katika maisha yake kitakacho shusha hadhi na sifa yake kwa wakati husika.
 
Historia huwa haifutiki ndiyo maana kuna hadi nyumba za makumbusho.
 
this is very true.mkuu binadamu ndo tulivyo
 
Nilishakumbana na kitu cha namna hiyo tena kwenye umati wa watu...sijui story ilianzia wapi sijui ndio chuki zenyewe nilashangaa mtu anawaambia watu huyu kanipa shida sana akiwa mtoto alikuwa anajinyea,mara nilishindwa kumlea mwanangu nikawa namlea yeye daah iliniuma nililia sana, nilijiuliza kwahiyo alinilea ili aje anisimange iliniumiza ukizingatia saizi na mimi nina watoto wangu wawili na nimeolewa, nafikiri wangekuwepo wakati wa mazungumzo hayo hata wao wangejisikia vibaya. nilichojifunza ni chuki kwasababu hataki kukubali ukweli uliopo sasa.
 
Hiyo lazima iwepo wana jf,kwaa ajili ya kujenga watu wengine,mfano,mbona fulani alikuwa kama mimi na amefika hapo? Kwanini nisiweze? Iko hivyo,soma hata vitabu vya dini,
 

kiface--Huyo alikudhalilisha sana aisee na urembo wote huo ulionao tena mbele ya kadamnasi.
 
Historia huwa haifutiki ndiyo maana kuna hadi nyumba za makumbusho.

Sitaki ifutike ila kwanini itumike kama hukumu.Au kama fact ya kumshusha mtu.
 

Pole mwaya imefikia hatua ata ukimuulizia mtu kwa kutaja jina kabla mtoa jibu ajakujibu uta sikia si yule aliyee..........?(kitu kibaya)
 
Hiyo lazima iwepo wana jf,kwaa ajili ya kujenga watu wengine,mfano,mbona fulani alikuwa kama mimi na amefika hapo? Kwanini nisiweze? Iko hivyo,soma hata vitabu vya dini,

Mkuu walio wengi awasemi kwa nia ya kutumia historia kama ushuhuda wengi wanasema mtu anapopata kufanikiwa ili tu mafanikio yake yasipingezwe saaaaana.
 
Hilo limesababisha wabongo kushindwa kujenga makampuni ushirika kwa roho ya kijicho. watu wanaeza kusanyika kucheza upatu,saccos lakini hawawezi kusanyika kuanzisha kiwanda,watalogana. Inaenda mbali ata watumishi wakiona mwingine kapanda watachomekea baya
 
Asante mwaya,ni chuki tu ndio iliotawala kwani hakutegemea kama na mimi ipo siku nitasimama mwenyewe, kwa umri nilionao kuanza kunipaka bila sababu yoyote hata watu tuliokuwa nao walimshangaa( ilikuwa kwenye sherehe flani hivi) sikumjibu kitu kwakweli nilikaa pembeni nikalia mpaka hasira ziliponiisha
 
Sitaki ifutike ila kwanini itumike kama hukumu.Au kama fact ya kumshusha mtu.

Wasiwasi wako tu!

Historia ipo na inatunzwa. Iwe mbaya au nzuri bado ni historia.

Jiamini. Cha muhimu ni ulipoishia siyo ulipoanzia.
 
Wasiwasi wako tu!

Historia ipo na inatunzwa. Iwe mbaya au nzuri bado ni historia.

Jiamini. Cha muhimu ni ulipoishia siyo ulipoanzia.

ni kweli unachosema kuwa historia ipo na inatunzwa kwaajili ya vizazi vijavyo, lakini wengine wanaitumia vibaya kwa mf: mtu anakupa story za baba/mama au mti wako wa karibu sana ambazo hazikusaidii zaidi ya kukuumiza, mf anakwambia mama yako alikuwa malaya sana, inakusaidia nini au utajisikiaje. Historia ipo kwaajili ya kujifunza na kutusaidia lkn si kwaajili ya kumdhalilisha mtu au kumchafua
 
Mashujaa waliowahi kushindwa
 

Attachments

  • 1409293511482.jpg
    160.1 KB · Views: 71
Unajua Billy gâtés alishindwa shule Harvard,einstern alionwa na walimu wake kama mbumbumbu,michael Jordan aliachwa kama asiyeweza basketball shuleni,apple boss alifukuzwa toka kampuni alioanzisha nk
 
Ni kweli na watu wa hivyo ni wa kukaa nao mbali ambao hawaoni mazuri ila mabaya tu na siku zote wanarudisha maendeleo ya watu nyuma
NYONGEZA;
Ni vizuri kwenye maisha yetu tukawa tunafikiri kabla ya kufanya jambo lolote coz mwisho wa siku ulichokifanya tayari ni kumbukumbu tosha hata vijukuu vyako vitakuja kuambiwa flani alikuwa hivi flani alikuwa vile, tujitahidi kutende mema.
 
Mama yangu mzazi alikaa 10 years bila kupata mtoto after ndoa yake na baadae alitupata team.kuna mtu uwa anaisema kila akituona cha ajabu asemi kwa kumtukuza Mungu anasema as if (msijishaue tunajua kupatikana kwenu)
 
Kweli jamani yaani inauma sana. Binadamu wengi hawapendi kuona wenzao wanaendelea. Yaani watu wanafurahi kuona Kila siku mtu ni wakulialia tu, aombeombe kwao, anyenyekee. Lkn inapotokea Yule mtu akafanikiwa chuki inaanza, tena chuki iliyokomaa kama vile mna mda mna ugomvi na huyo mtu. Daa!! Inanishangazaga sana.

Tubadilike na tuchukulie mafanikio ya mtu mwingne kama yako mwenyewe.
 
Mama yangu mzazi alishafariki miaka 18 iliyopita lakini kuna watu wanamzungumzia vibaya mpaka leo,watoto wake tunavyoyasikia tunajisikia uchungu sana, kuna dadaangu siku moja alipika chakula kibichi chaajabu aliambiwa hicho ni kilema kutoka kwa mamaako dadaangu alilia sana, siku nyingine dadaangu huyohuyo sikumbuki sana kosa alilofanya lkn aliambiwa utakuja kufa kama mama yako daah aisee hii dunia ina mengi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…