Ubakaji na mwonekano wake kwa jamii

Ubakaji na mwonekano wake kwa jamii

Bernadetta

Member
Joined
Mar 24, 2013
Posts
7
Reaction score
3
Naomba maoni yenu kuhusu hii hoja. Hivi ni kwanini ubakaji nchini unaonekana kama jambo la aibu kwa mtendewaji? Na kwanini jamii baada ya kuwasaidia hawa waliobakwa wengi hukaa chini na kuwasengenya na kuwaongelea waliobakwa kama vile ni habari za kunywea chai vijiweni? Je jamii yenu imekuwa haina moyo wa utu na huruma kwa hawa waliobakwa au ni kutokuwa na ufahamu wa madhara ya ubakwaji kisakologia? Ni mara nyingi nasikia na kusoma kwenye blogs watu wanasema 'duh huyu demu alibakwa bwana' au 'mtoto wa yule mama kaharibiwa maskini'...nabaki najiuliza jamani hizi ni habari za kutangaza kwa jamii kama gossips au inatakiwa ujiulize nitamsaidiaje huyu binadamu mwenzangu. Nilifurahi sana ile issue ya ubakwaji wa yule mwanafunzi wa chuo wa India ilivyochukuliwa na jamii ile. Watu waliandamana, vyombo vya habari vilipiga kelele mpaka serikali ilichukuwa hatua. Je ni watu wangapi na watoto wa Tanzania wanabakwa kila siku? Je serikali na wewe kama mtanzania unafanya nini? Tusifungie macho jambo hili hata kidoogo :nono: kwani hao wanaobakwa ni mama zetu, dada zetu, marafiki zetu, watoto zetu...usingoje mpaka janga hii lifike kwenye familia yako ndipo uchukue hatua. Usiwe mmoja wa tatizo kwa kugossip tu na kucheka yaliowakumba (eee haeli kabakwa alikuwa anaringa sana huyo) kuwa mmoja wa suluhisho.
 
Mkuu nchi yetu si kwamba ubakaji ndo inafumbia macho tu, yapo mambo mengi mno na cha kushangaza zaidi ni pale mtu anabaka na uthibisho upo ila kutokana na rushwa kushamiri mbakaji anarudi mtaani akitamba kama shujaa flani we unadhani kwa wale wenye nia kama hiyo watabadilika na kuiacha dhamira hiyo? Leo Tz hakuna vita ubakaji unashamiri kiasi hicho je ikitokea (japo siombei kuwa hivyo) tuwe vitani kama Kongo ama nchi zingine itakuwa je? Ilopo ni wananchi kujipanga ktk chaguzi zijazo tujitahidi kuweka madarakani viongozi ambao watatutetea na kuwa na uchungu na moyo wa uzalendo na nchi yetu, hasa wanawake ambao kwa kiasi kikubwa ndio wanaozalilika na ndio wao wanakuwa mstari wa nyuma kujitokeza kupiga kura, ni wakati wao sasa kujifunza kutokana na makosa
 
Back
Top Bottom