immasoft
Senior Member
- Mar 2, 2011
- 188
- 128
Haya basi, tukafika kwenye uwanja wetu, tayari kwa uburuzaji. Na sikatai, kidogo tulitingishika mlipotoka, tukafikiri kwamba labda mna mikakati murua ya kuwaamsha watu, kumbe yaleyale tu, yaleyale. Kutishia maandamano kisha kukaa kimya. Mmmh, kweli mmenifurahisha sana.
Halafu kung'ang'ania tu, kung'ang'ania tu rasimu ya sumu jinsi ilivyo mmetupatia nafasi nyingi bora kabisa. Kwani wale walikuwa miungu? Lazima walisahau mambo mengine, na kubwa kabisa hawakuandika katiba ya nchi isiyo na jina hivyo tumeweza kuahidi kila kitu kwa kila mtu ili kuficha jinsi tulivyoondoa yale ambayo yalitubana, pamoja na suala zito lenyewe la mahusiano ya ndoa.
Ndiyo, wasanii wamelalamika, wape, na wanawake, kabisa wape maana wapiga kura wengi ni wanawake, hata vijana wakorofi, wape, wakulima, wape. Mimi nilikuwa tayari kuwapa hata watoto wa shule za msingi iandikwe kwenye katiba kwamba ni marufuku kuwachapa viboko lakini wenzangu wakanikumbusha kwamba hawana kura. Senene wangekuwa na kura tungeweka kwamba wana haki ya kutoliwa ha ha ha lakini wenye kura si wao, na wa kuliwa wengine wala hawatambui. Na katika ahadi zote hizi, hakuna inayoweza kufuatiliwa kisheria. Na wote ambao wameahidiwa hivyo wanatingisha kiuno na wao. Angalia akina mama wanavyoshangilia.
Sasa tulitegemea na nyinyi mngekuja na mapendekezo mengine ya kuboresha lakini wapi. Rasimu ya sumu ikageuka msahafu kwa hiyo tuliachiwa uwanja kucheza tunavyopenda. Haya mkategemea kwamba tutashindwa kupitisha, mkalainishwa na mkutano mwingine tena na kurudi na furaha kwamba mchakato umeahirishwa. Ama kweli nyinyi hamjui siasa. Baada ya mapatano, uwanja ulikuwa wazi tukamilishe kila kitu bila kipingamizi, na kura zilipotaka kutuvuruga, sisi ndiyo tunaoshika mpini kwa hiyo ikawa rahisi sana na waliotaka kutingisha tumewaondoa.
Ndiyo. Hii ndiyo demokrasia yetu. Na tuna uhakika kwamba tutapitisha rasimu yetu tu. Tunajua mtalalamika tena kidogokidogo, lakini hakuna mpango wa kuzunguka na kutoa elimu ya kweli, hakuna ambaye atakaa chini na kulinganisha rasumu yenu na rasimu yetu, hakuna ambaye atatoa vipeperushi na kuvisambaza nchi nzima, hakuna mwenye ujanja wa kukwepa marungu yetu yote ya dola pamoja na dola zetu za kuhonga. Mtaingia barabarani tena na kupigwa kidogo kisha tutapitisha rasimu tena bila wasiwasi.
Na usije kwangu na machozi ya mamba, ooh demokrasia imebakwa, ooh sisi wateule tumeondoa mambo yote ya kutishia maslahi yetu, oooh sasa unatumika udikteta kulazimisha katiba yetu, oooh mbele ya safari itazaa machafuko. Nani anajali machafuko ya kesho wakati anabugia leo. Nani anataka kujua kuna nini nyuma ya mlima wa pilao mbele yake. Kula na kusaza ndiyo mtindo wa kisasa, ndiyo mtindo wa kisiasa pia.
Najua utachukia sana barua hii Makengeza maana tumewaweza ndiyo maana tuna haki ya kutingisha ------ mbele yenu. Nawaambieni ukweli hata ukiuma namna gani. Na usinisumbue kunilaani na kusema nimesema uongo. Nionyeshe. Nionyeshe kwa mipango yenu madhubuti siyo kelele zenu za juujuu. Vinginevyo, karibuni kwenye katiba mpya ha ha ha ha.
Haya basi, tukafika kwenye uwanja wetu, tayari kwa uburuzaji. Na sikatai, kidogo tulitingishika mlipotoka, tukafikiri kwamba labda mna mikakati murua ya kuwaamsha watu, kumbe yaleyale tu, yaleyale. Kutishia maandamano kisha kukaa kimya. Mmmh, kweli mmenifurahisha sana.
Halafu kung'ang'ania tu, kung'ang'ania tu rasimu ya sumu jinsi ilivyo mmetupatia nafasi nyingi bora kabisa. Kwani wale walikuwa miungu? Lazima walisahau mambo mengine, na kubwa kabisa hawakuandika katiba ya nchi isiyo na jina hivyo tumeweza kuahidi kila kitu kwa kila mtu ili kuficha jinsi tulivyoondoa yale ambayo yalitubana, pamoja na suala zito lenyewe la mahusiano ya ndoa.
Ndiyo, wasanii wamelalamika, wape, na wanawake, kabisa wape maana wapiga kura wengi ni wanawake, hata vijana wakorofi, wape, wakulima, wape. Mimi nilikuwa tayari kuwapa hata watoto wa shule za msingi iandikwe kwenye katiba kwamba ni marufuku kuwachapa viboko lakini wenzangu wakanikumbusha kwamba hawana kura. Senene wangekuwa na kura tungeweka kwamba wana haki ya kutoliwa ha ha ha lakini wenye kura si wao, na wa kuliwa wengine wala hawatambui. Na katika ahadi zote hizi, hakuna inayoweza kufuatiliwa kisheria. Na wote ambao wameahidiwa hivyo wanatingisha kiuno na wao. Angalia akina mama wanavyoshangilia.
Sasa tulitegemea na nyinyi mngekuja na mapendekezo mengine ya kuboresha lakini wapi. Rasimu ya sumu ikageuka msahafu kwa hiyo tuliachiwa uwanja kucheza tunavyopenda. Haya mkategemea kwamba tutashindwa kupitisha, mkalainishwa na mkutano mwingine tena na kurudi na furaha kwamba mchakato umeahirishwa. Ama kweli nyinyi hamjui siasa. Baada ya mapatano, uwanja ulikuwa wazi tukamilishe kila kitu bila kipingamizi, na kura zilipotaka kutuvuruga, sisi ndiyo tunaoshika mpini kwa hiyo ikawa rahisi sana na waliotaka kutingisha tumewaondoa.
Ndiyo. Hii ndiyo demokrasia yetu. Na tuna uhakika kwamba tutapitisha rasimu yetu tu. Tunajua mtalalamika tena kidogokidogo, lakini hakuna mpango wa kuzunguka na kutoa elimu ya kweli, hakuna ambaye atakaa chini na kulinganisha rasumu yenu na rasimu yetu, hakuna ambaye atatoa vipeperushi na kuvisambaza nchi nzima, hakuna mwenye ujanja wa kukwepa marungu yetu yote ya dola pamoja na dola zetu za kuhonga. Mtaingia barabarani tena na kupigwa kidogo kisha tutapitisha rasimu tena bila wasiwasi.
Na usije kwangu na machozi ya mamba, ooh demokrasia imebakwa, ooh sisi wateule tumeondoa mambo yote ya kutishia maslahi yetu, oooh sasa unatumika udikteta kulazimisha katiba yetu, oooh mbele ya safari itazaa machafuko. Nani anajali machafuko ya kesho wakati anabugia leo. Nani anataka kujua kuna nini nyuma ya mlima wa pilao mbele yake. Kula na kusaza ndiyo mtindo wa kisasa, ndiyo mtindo wa kisiasa pia.
Najua utachukia sana barua hii Makengeza maana tumewaweza ndiyo maana tuna haki ya kutingisha ------ mbele yenu. Nawaambieni ukweli hata ukiuma namna gani. Na usinisumbue kunilaani na kusema nimesema uongo. Nionyeshe. Nionyeshe kwa mipango yenu madhubuti siyo kelele zenu za juujuu. Vinginevyo, karibuni kwenye katiba mpya ha ha ha ha.
Haya basi, tukafika kwenye uwanja wetu, tayari kwa uburuzaji. Na sikatai, kidogo tulitingishika mlipotoka, tukafikiri kwamba labda mna mikakati murua ya kuwaamsha watu, kumbe yaleyale tu, yaleyale. Kutishia maandamano kisha kukaa kimya. Mmmh, kweli mmenifurahisha sana.
Halafu kung'ang'ania tu, kung'ang'ania tu rasimu ya sumu jinsi ilivyo mmetupatia nafasi nyingi bora kabisa. Kwani wale walikuwa miungu? Lazima walisahau mambo mengine, na kubwa kabisa hawakuandika katiba ya nchi isiyo na jina hivyo tumeweza kuahidi kila kitu kwa kila mtu ili kuficha jinsi tulivyoondoa yale ambayo yalitubana, pamoja na suala zito lenyewe la mahusiano ya ndoa.
Ndiyo, wasanii wamelalamika, wape, na wanawake, kabisa wape maana wapiga kura wengi ni wanawake, hata vijana wakorofi, wape, wakulima, wape. Mimi nilikuwa tayari kuwapa hata watoto wa shule za msingi iandikwe kwenye katiba kwamba ni marufuku kuwachapa viboko lakini wenzangu wakanikumbusha kwamba hawana kura. Senene wangekuwa na kura tungeweka kwamba wana haki ya kutoliwa ha ha ha lakini wenye kura si wao, na wa kuliwa wengine wala hawatambui. Na katika ahadi zote hizi, hakuna inayoweza kufuatiliwa kisheria. Na wote ambao wameahidiwa hivyo wanatingisha kiuno na wao. Angalia akina mama wanavyoshangilia.
Sasa tulitegemea na nyinyi mngekuja na mapendekezo mengine ya kuboresha lakini wapi. Rasimu ya sumu ikageuka msahafu kwa hiyo tuliachiwa uwanja kucheza tunavyopenda. Haya mkategemea kwamba tutashindwa kupitisha, mkalainishwa na mkutano mwingine tena na kurudi na furaha kwamba mchakato umeahirishwa. Ama kweli nyinyi hamjui siasa. Baada ya mapatano, uwanja ulikuwa wazi tukamilishe kila kitu bila kipingamizi, na kura zilipotaka kutuvuruga, sisi ndiyo tunaoshika mpini kwa hiyo ikawa rahisi sana na waliotaka kutingisha tumewaondoa.
Ndiyo. Hii ndiyo demokrasia yetu. Na tuna uhakika kwamba tutapitisha rasimu yetu tu. Tunajua mtalalamika tena kidogokidogo, lakini hakuna mpango wa kuzunguka na kutoa elimu ya kweli, hakuna ambaye atakaa chini na kulinganisha rasumu yenu na rasimu yetu, hakuna ambaye atatoa vipeperushi na kuvisambaza nchi nzima, hakuna mwenye ujanja wa kukwepa marungu yetu yote ya dola pamoja na dola zetu za kuhonga. Mtaingia barabarani tena na kupigwa kidogo kisha tutapitisha rasimu tena bila wasiwasi.
Na usije kwangu na machozi ya mamba, ooh demokrasia imebakwa, ooh sisi wateule tumeondoa mambo yote ya kutishia maslahi yetu, oooh sasa unatumika udikteta kulazimisha katiba yetu, oooh mbele ya safari itazaa machafuko. Nani anajali machafuko ya kesho wakati anabugia leo. Nani anataka kujua kuna nini nyuma ya mlima wa pilao mbele yake. Kula na kusaza ndiyo mtindo wa kisasa, ndiyo mtindo wa kisiasa pia.
Najua utachukia sana barua hii Makengeza maana tumewaweza ndiyo maana tuna haki ya kutingisha ------ mbele yenu. Nawaambieni ukweli hata ukiuma namna gani. Na usinisumbue kunilaani na kusema nimesema uongo. Nionyeshe. Nionyeshe kwa mipango yenu madhubuti siyo kelele zenu za juujuu. Vinginevyo, karibuni kwenye katiba mpya ha ha ha ha.
Halafu kung'ang'ania tu, kung'ang'ania tu rasimu ya sumu jinsi ilivyo mmetupatia nafasi nyingi bora kabisa. Kwani wale walikuwa miungu? Lazima walisahau mambo mengine, na kubwa kabisa hawakuandika katiba ya nchi isiyo na jina hivyo tumeweza kuahidi kila kitu kwa kila mtu ili kuficha jinsi tulivyoondoa yale ambayo yalitubana, pamoja na suala zito lenyewe la mahusiano ya ndoa.
Ndiyo, wasanii wamelalamika, wape, na wanawake, kabisa wape maana wapiga kura wengi ni wanawake, hata vijana wakorofi, wape, wakulima, wape. Mimi nilikuwa tayari kuwapa hata watoto wa shule za msingi iandikwe kwenye katiba kwamba ni marufuku kuwachapa viboko lakini wenzangu wakanikumbusha kwamba hawana kura. Senene wangekuwa na kura tungeweka kwamba wana haki ya kutoliwa ha ha ha lakini wenye kura si wao, na wa kuliwa wengine wala hawatambui. Na katika ahadi zote hizi, hakuna inayoweza kufuatiliwa kisheria. Na wote ambao wameahidiwa hivyo wanatingisha kiuno na wao. Angalia akina mama wanavyoshangilia.
Sasa tulitegemea na nyinyi mngekuja na mapendekezo mengine ya kuboresha lakini wapi. Rasimu ya sumu ikageuka msahafu kwa hiyo tuliachiwa uwanja kucheza tunavyopenda. Haya mkategemea kwamba tutashindwa kupitisha, mkalainishwa na mkutano mwingine tena na kurudi na furaha kwamba mchakato umeahirishwa. Ama kweli nyinyi hamjui siasa. Baada ya mapatano, uwanja ulikuwa wazi tukamilishe kila kitu bila kipingamizi, na kura zilipotaka kutuvuruga, sisi ndiyo tunaoshika mpini kwa hiyo ikawa rahisi sana na waliotaka kutingisha tumewaondoa.
Ndiyo. Hii ndiyo demokrasia yetu. Na tuna uhakika kwamba tutapitisha rasimu yetu tu. Tunajua mtalalamika tena kidogokidogo, lakini hakuna mpango wa kuzunguka na kutoa elimu ya kweli, hakuna ambaye atakaa chini na kulinganisha rasumu yenu na rasimu yetu, hakuna ambaye atatoa vipeperushi na kuvisambaza nchi nzima, hakuna mwenye ujanja wa kukwepa marungu yetu yote ya dola pamoja na dola zetu za kuhonga. Mtaingia barabarani tena na kupigwa kidogo kisha tutapitisha rasimu tena bila wasiwasi.
Na usije kwangu na machozi ya mamba, ooh demokrasia imebakwa, ooh sisi wateule tumeondoa mambo yote ya kutishia maslahi yetu, oooh sasa unatumika udikteta kulazimisha katiba yetu, oooh mbele ya safari itazaa machafuko. Nani anajali machafuko ya kesho wakati anabugia leo. Nani anataka kujua kuna nini nyuma ya mlima wa pilao mbele yake. Kula na kusaza ndiyo mtindo wa kisasa, ndiyo mtindo wa kisiasa pia.
Najua utachukia sana barua hii Makengeza maana tumewaweza ndiyo maana tuna haki ya kutingisha ------ mbele yenu. Nawaambieni ukweli hata ukiuma namna gani. Na usinisumbue kunilaani na kusema nimesema uongo. Nionyeshe. Nionyeshe kwa mipango yenu madhubuti siyo kelele zenu za juujuu. Vinginevyo, karibuni kwenye katiba mpya ha ha ha ha.
Haya basi, tukafika kwenye uwanja wetu, tayari kwa uburuzaji. Na sikatai, kidogo tulitingishika mlipotoka, tukafikiri kwamba labda mna mikakati murua ya kuwaamsha watu, kumbe yaleyale tu, yaleyale. Kutishia maandamano kisha kukaa kimya. Mmmh, kweli mmenifurahisha sana.
Halafu kung'ang'ania tu, kung'ang'ania tu rasimu ya sumu jinsi ilivyo mmetupatia nafasi nyingi bora kabisa. Kwani wale walikuwa miungu? Lazima walisahau mambo mengine, na kubwa kabisa hawakuandika katiba ya nchi isiyo na jina hivyo tumeweza kuahidi kila kitu kwa kila mtu ili kuficha jinsi tulivyoondoa yale ambayo yalitubana, pamoja na suala zito lenyewe la mahusiano ya ndoa.
Ndiyo, wasanii wamelalamika, wape, na wanawake, kabisa wape maana wapiga kura wengi ni wanawake, hata vijana wakorofi, wape, wakulima, wape. Mimi nilikuwa tayari kuwapa hata watoto wa shule za msingi iandikwe kwenye katiba kwamba ni marufuku kuwachapa viboko lakini wenzangu wakanikumbusha kwamba hawana kura. Senene wangekuwa na kura tungeweka kwamba wana haki ya kutoliwa ha ha ha lakini wenye kura si wao, na wa kuliwa wengine wala hawatambui. Na katika ahadi zote hizi, hakuna inayoweza kufuatiliwa kisheria. Na wote ambao wameahidiwa hivyo wanatingisha kiuno na wao. Angalia akina mama wanavyoshangilia.
Sasa tulitegemea na nyinyi mngekuja na mapendekezo mengine ya kuboresha lakini wapi. Rasimu ya sumu ikageuka msahafu kwa hiyo tuliachiwa uwanja kucheza tunavyopenda. Haya mkategemea kwamba tutashindwa kupitisha, mkalainishwa na mkutano mwingine tena na kurudi na furaha kwamba mchakato umeahirishwa. Ama kweli nyinyi hamjui siasa. Baada ya mapatano, uwanja ulikuwa wazi tukamilishe kila kitu bila kipingamizi, na kura zilipotaka kutuvuruga, sisi ndiyo tunaoshika mpini kwa hiyo ikawa rahisi sana na waliotaka kutingisha tumewaondoa.
Ndiyo. Hii ndiyo demokrasia yetu. Na tuna uhakika kwamba tutapitisha rasimu yetu tu. Tunajua mtalalamika tena kidogokidogo, lakini hakuna mpango wa kuzunguka na kutoa elimu ya kweli, hakuna ambaye atakaa chini na kulinganisha rasumu yenu na rasimu yetu, hakuna ambaye atatoa vipeperushi na kuvisambaza nchi nzima, hakuna mwenye ujanja wa kukwepa marungu yetu yote ya dola pamoja na dola zetu za kuhonga. Mtaingia barabarani tena na kupigwa kidogo kisha tutapitisha rasimu tena bila wasiwasi.
Na usije kwangu na machozi ya mamba, ooh demokrasia imebakwa, ooh sisi wateule tumeondoa mambo yote ya kutishia maslahi yetu, oooh sasa unatumika udikteta kulazimisha katiba yetu, oooh mbele ya safari itazaa machafuko. Nani anajali machafuko ya kesho wakati anabugia leo. Nani anataka kujua kuna nini nyuma ya mlima wa pilao mbele yake. Kula na kusaza ndiyo mtindo wa kisasa, ndiyo mtindo wa kisiasa pia.
Najua utachukia sana barua hii Makengeza maana tumewaweza ndiyo maana tuna haki ya kutingisha ------ mbele yenu. Nawaambieni ukweli hata ukiuma namna gani. Na usinisumbue kunilaani na kusema nimesema uongo. Nionyeshe. Nionyeshe kwa mipango yenu madhubuti siyo kelele zenu za juujuu. Vinginevyo, karibuni kwenye katiba mpya ha ha ha ha.
Haya basi, tukafika kwenye uwanja wetu, tayari kwa uburuzaji. Na sikatai, kidogo tulitingishika mlipotoka, tukafikiri kwamba labda mna mikakati murua ya kuwaamsha watu, kumbe yaleyale tu, yaleyale. Kutishia maandamano kisha kukaa kimya. Mmmh, kweli mmenifurahisha sana.
Halafu kung'ang'ania tu, kung'ang'ania tu rasimu ya sumu jinsi ilivyo mmetupatia nafasi nyingi bora kabisa. Kwani wale walikuwa miungu? Lazima walisahau mambo mengine, na kubwa kabisa hawakuandika katiba ya nchi isiyo na jina hivyo tumeweza kuahidi kila kitu kwa kila mtu ili kuficha jinsi tulivyoondoa yale ambayo yalitubana, pamoja na suala zito lenyewe la mahusiano ya ndoa.
Ndiyo, wasanii wamelalamika, wape, na wanawake, kabisa wape maana wapiga kura wengi ni wanawake, hata vijana wakorofi, wape, wakulima, wape. Mimi nilikuwa tayari kuwapa hata watoto wa shule za msingi iandikwe kwenye katiba kwamba ni marufuku kuwachapa viboko lakini wenzangu wakanikumbusha kwamba hawana kura. Senene wangekuwa na kura tungeweka kwamba wana haki ya kutoliwa ha ha ha lakini wenye kura si wao, na wa kuliwa wengine wala hawatambui. Na katika ahadi zote hizi, hakuna inayoweza kufuatiliwa kisheria. Na wote ambao wameahidiwa hivyo wanatingisha kiuno na wao. Angalia akina mama wanavyoshangilia.
Sasa tulitegemea na nyinyi mngekuja na mapendekezo mengine ya kuboresha lakini wapi. Rasimu ya sumu ikageuka msahafu kwa hiyo tuliachiwa uwanja kucheza tunavyopenda. Haya mkategemea kwamba tutashindwa kupitisha, mkalainishwa na mkutano mwingine tena na kurudi na furaha kwamba mchakato umeahirishwa. Ama kweli nyinyi hamjui siasa. Baada ya mapatano, uwanja ulikuwa wazi tukamilishe kila kitu bila kipingamizi, na kura zilipotaka kutuvuruga, sisi ndiyo tunaoshika mpini kwa hiyo ikawa rahisi sana na waliotaka kutingisha tumewaondoa.
Ndiyo. Hii ndiyo demokrasia yetu. Na tuna uhakika kwamba tutapitisha rasimu yetu tu. Tunajua mtalalamika tena kidogokidogo, lakini hakuna mpango wa kuzunguka na kutoa elimu ya kweli, hakuna ambaye atakaa chini na kulinganisha rasumu yenu na rasimu yetu, hakuna ambaye atatoa vipeperushi na kuvisambaza nchi nzima, hakuna mwenye ujanja wa kukwepa marungu yetu yote ya dola pamoja na dola zetu za kuhonga. Mtaingia barabarani tena na kupigwa kidogo kisha tutapitisha rasimu tena bila wasiwasi.
Na usije kwangu na machozi ya mamba, ooh demokrasia imebakwa, ooh sisi wateule tumeondoa mambo yote ya kutishia maslahi yetu, oooh sasa unatumika udikteta kulazimisha katiba yetu, oooh mbele ya safari itazaa machafuko. Nani anajali machafuko ya kesho wakati anabugia leo. Nani anataka kujua kuna nini nyuma ya mlima wa pilao mbele yake. Kula na kusaza ndiyo mtindo wa kisasa, ndiyo mtindo wa kisiasa pia.
Najua utachukia sana barua hii Makengeza maana tumewaweza ndiyo maana tuna haki ya kutingisha ------ mbele yenu. Nawaambieni ukweli hata ukiuma namna gani. Na usinisumbue kunilaani na kusema nimesema uongo. Nionyeshe. Nionyeshe kwa mipango yenu madhubuti siyo kelele zenu za juujuu. Vinginevyo, karibuni kwenye katiba mpya ha ha ha ha.