Nashukuru wana jf kwa makaribisho mazuri,
hivi inakuwaje mwanaume anakuwa muongo anakudanganya for two years kwamba hajaoa, then unakuja unagundua kaoa ,ana mke na watoto
Mie nimedanganywa na sasa niko kwenye maumivu makali ili niweze kuendelea na maisha,nilikutana nae chuoni yeye anasoma masomo ya juu zaidi yangu, akasema yuko single na mipango yote ya kuoana tukimaliza chuo alikuwa ananiambia.
Yeye alitangulia kumaliza lakini alikuwa anasafiri anakuja kuniangalia chuoni, baasi nilipomaliza kwa vile tunakaa mikoa tofauti nikaamua kumzukia kwa suprise huko anapoishi, nilienda nilipofika mojakwa moja hadi ofisini, kastuka sana, tukatoka nikajua napelekwa kwake akaishia hotelini, jioni alipokuja ndio akanimwagia hilo shuzi, eti sorry,hivi kweli binadamu wamekuwa na roho mbaya kiasi hiki?nawaasa wasichana wenzangu wawe makini sana na hawa wenzetu kwani sio kila kitu wanachosem ni kweli....sasa nikaamua kukatisha mawasiliano kabisa kwa kipindi kirefu kiasi
juzjuz kaja na mpya kaniomba anioe mke wa pili kwamba hawezi ishi bila mimi, marafiki zangu wanavutana wengine wanasema nikubali na wengine wanasema niendelee na msimamo wangu, je wewe mwana jf mwenzangu unasemaje?????
Ahsante sana kwa kweli huwezi jua ila ukiwa mchunguzi sana unaweza jua mapema, maana kunasimu zingine maybe ningekuwa mpekuzipekuzi ningegundua mapemaWawe makini kivipi Dada angu? Huwezi kumjua mtu Eti pale tu atakapokuja kwa mara ya kwanza, ujue huyu huko hvi au vile. Kinachotakiwa hapa ni wewe kuwa na msimamo wako.sikushaur uje kuw mke wa pili ,achana nae mana bado hajakuletea effect kubwa kam vle Mimba,ambyo inawez kukufany ukakae naye.. Kwa Dunia ya leo wake wawil ni Ugomv ambao hutawez kuhimil kam una moyo mwepes. Ni hayo tu sisy angu na pole sana kwa yaliyokukuta.
Hili nalo neno, maana hizo zamu!Pole dada. Ila la mke wa pili sikushauri. Maana hapa sisi tuko wawili yani husband na wife bado songombingo; sasa nambie muwe na uhusiano wa watu watatu; mume mmoja wake wawili; si kutafuta maradhi huko dada maana hapo ina maana umemuamini mume wako na mke mwenzio.
Baba enock niliamua kum surprise ile ya kimahaba, na nikijua yuko ofisini coz asubuhi na mapema alinipigia kwa landline kwa hiyo nisingewaza namfumania ofisini, pia ilikuwa ya kimahaba bila kuwaza lolote, swali kwako, kwa nini unafikiri alinidanganya? alidhani akisema ameoa ningemkataa au ni kitu gani alikuwa anawaza, kwa maoni yako tuNadhani hadi kufikia hatua ya "kumzukia kwa surprise" tayari ulikuwa na wasiwasi fulani kuhusu huyo kijana?
Ungefuata "dhamira" yako usingelizwa, lakini maisha ndivyo yalivyo, wanawake ni wa kudanganywa mara zote!
<br /><font size="3"><span style="font-family: franklin gothic medium">Pole kwa mkasa uliokukumba...endelea na maisha na fungua moyo wako ipo siku utapata wa kwako peke yako.<br />
Vijana single tupo wa kumwaga,ushindwe kuchagua tu.</span></font>
<br />1.Tatizo wasichana tunajenga mazingira ya kudanganywa tangu awali. Mwanaume ukimdanganya jambo moja na akagundua umemdanganya ujue wewe utadanganywa matano.<br />
2. Wasichana wamekuwa wepesi sana kuwaamini hawa wanaume hivyo kuwahi kuanzisha mahusiano nao kabla hawajawaelewa.<br />
3. Wanashindwa kutofautisha wanapopendwa kikweli na wanapotumiwa.<br />
4. Wasichana wengi ni kama wanalazimisha penzi, yaani unaona kabisa mtu hakupendi ila kwa sababu moyo wako upo pale unaona hakuna mwingine.<br />
Yaani mimi mtu akinidanganya siku hiyo najua kama ananidanganya. Ndani ya wiki tu nitajua hadi marital status yake labda kama sihitaji kumjua.
Pole kwa mkasa uliokukumba...endelea na maisha na fungua moyo wako ipo siku utapata wa kwako peke yako.
Vijana single tupo wa kumwaga,ushindwe kuchagua tu.