Tutarajie mabadiliko makubwa kama haya ..

Tutor B

JF-Expert Member
Jun 11, 2011
9,025
6,554
Kutozwa kodi kwa yafuatazo:-
1. Pesa za michango ya harusi
2. Pesa za kuendesha misiba.
3. Michango ya Happy birteh day
4. Michango ya Send off / Engagement party
5. Mkikutwa zaidi ya watu sita mnakula lager ... lipa kodi

Yote haya yanaweza tokea kwa sababu nchi yetu haina mkakati wa kimaandishi wa kuiendesha na kuifikisha kunakotakiwa. Kila anayepata nafasi anaanzisha mambo yake - na pindi akimaliza muda wake ; yote yanasaaulika kana kwamba hayakuwa na maana yoyote.
Ya mwalimu tuyahache japo yapo mengi ... (mazuri na mabaya)
Ruksa kweli ilikuwa ruksa hadi kuambiwa kwamba anayetaka kula chura RUKSA.

Mbinafsishaji ... jamani hata nyumba ambayo siku zote inapanda thamani nayo ilibinafsishwa?

Kilimo kwanza ... mashamba ya kumilikiwa na taifa yako wapi kwa kampeini ya kilimo kwanza?

Sasa Tanzania ya viwanda yaja ... naogopa kusema mengi kwa kuwa hata mwaka mmoja bado .. ila Mwanzo wa ngoma ni lele..
 
Back
Top Bottom