Tupinge dhuruma

Tupinge dhuruma

Sikasyakamo

Member
Joined
Aug 1, 2015
Posts
36
Reaction score
9
Tupinge dhuruma, huu ni ubinafsi kwa wabunge wetu
IMG-20181118-WA0007.jpeg
 
Sijui hili ni kabila gani linaendelea kutuharibia lugha yetu adhimu.

Sio dhuruma ni dhuluma mkuu.
 
Sijui hili ni kabila gani linaendelea kutuharibia lugha yetu adhimu.

Sio dhuruma ni dhuluma mkuu.
Ni wakati wa kuungana na kuwa wamoja seriously na si kukosoa lugha. Hili ni jambo la msingi sana ambalo linakwenda kuwaumiza watumishi na wafanyakazi wa nchi hii. Mfanyakazi umekatwa kodi miaka 35 halafu na hiki kidogo walinachodai wanakuwekea wanakupokonya kwa kutunga sheria hizi kandamizi Umeweka hela yako miaka yote 35 labda ukitegemea utapata na interest siku ya kuipata badala yake unaporwa hata kile kidogo. Wanaoumia zaidi sana ni watumishi waaminifu ambao hawakututa wakati wa utumishi wao kwani kipato cha mtumishi wa nchi yetu hakitoshi hata kula mlo wa heshima.
Ni kweli kwamba hawa wabunge wetu hawana msaada kwetu na tusiposimama na kujitetea wenyewe hakika yajayo yatatuumiza zaidi. Tuungane tuseme hapana yatosha, kila mahali mfanyakazi wa Tanzania alipo aseme neno na kutenda kwenye uchaguzi ujao.
Wamekataa kututetea nasi tuwakatae kwenye sanduku la kura kwani hata wakiiba kura lakini hukumu itabaki mioyoni mwao kuwa tuliwakataa na wanatutawala kwa mabavu.
 
kama ukisikia dhuluma ni hii ya wastaafu kupunjwa hela zao eti wataathirika mitaani wakipewa zote. Na eti wanawahi kuishiwa na kubaki wakiishi maisha ya chini. Kwanza ifahamike kiwa hii serikali haitaki kuwajali watumishi wake. Tangu mwaka 2015 ni watumishi wachache sana wamepandishwa vyeo na nyongeza ya mishahara hakuna. Kwahiyo mtumishi kama walivyo watu wengine inabidi achukue mikopo na kuishi kwa kipato cha chini sana. Hapa analazimika kupunguza baadhi ya matumizi zikiwema huduma za lishe bora. Baada ya kustaafu inabidi apumzike na kuanza kula matunda ya kazi yake
Cha ajabu anapokumbana na mafao yasiyoridhisha ndoto yake lazima afya yake itayumba. Hii 35% ni hela ndogo sana isiyotosheleza chochote kwa mstaafu. Ni iweje serikali iwe na maamuzi mabaya namna hii. Kuna nini nyuma ya pazia? Je nini utetezi wa vyama vya wafanyakazi juu ya hili. Ni kwa nini hatuwasikia wabunge wakitetea jambo hili. Ni vipi huyu mstaafu na yeye akaanzisha miradi yake na kujihesabu kuwa muwekezaji au hata kuanzisha mradi wa kilimo. Hivi ni kwa nini rais adilitolee maamuzi kama alivyofanya kwenye bei ya klrosho. Au huyu mstaafu anafanyiwa hivi kwa sababu halindi kura na pengine idadi yao ni ndogo.
Tufike sehemu tusianze kuchezeana kwenye mapato. Mfano kwa mtu uliyetumika serikalini kwa miaka 40 na kuwa na akiba ya milioni 100 halafu unakuja kuambulia milioni 35. Hii naona si sawa, fedha zinapungua thamani mfano leo thamani ya dola haitolingana na thamani ya dola miaka 12 ijayo. Na lek hii nikichukua milioni 100 zangu nikatengeneza miradi, baada ya kipindi nitakuwa mbali sana. Jamani hawa wabunge wametutia umasikini bila sababu. Hivi juhudi zipi za serikali ambazo zinawatoa wabunge upinzani kwenda kuziunga kama hali ndiyo hii. Iweje mtu mkamilifu aende kuunga juhudi kuwatia wenzake umasikini. Hela za mbunge miaka 5 haiguswi na wanapata zaidi ya milioni 200. Sisi wastaafu tunapewa chini ya mia. Naomba rais Maghfuli alione hili
 
1.Kwanini wafanyakazi wa uma wa Tanzania wanafanywa wa watumwa ndani ya nchi yao?
2.Kwanini watu wachache wanajilimbikizia keki ya taifa taifa na wengine kupunjwa?
3.tutaendelea kuishi hivi mpaka lini mbona wenzetu kenya wameweza sisi tunashindwa nini?
Haya maswali hua hayaanishi mimi ni mmoja kati ya captive workers wa nchi hii kwa mwendo huu natamani hii serikali isipate hata kura moja kutoka kwa watumishi wa umma kwa sababu kinacho endelea sasa hivi hakionyeshi kama tupo kwenye right track jana nilkua na kunywa chai na mkate leo na kunywa chai na kiporo jana nilikua sijuihata kushona viatu lakini leo nimekua nimekua kama fundi jana nilikua na save 5000 leo sina cha kusave kila ninachkipata
Kina yeyuka kutokana na mfumuko wa bei je hii ndio amani? Je haya ndio maendeleo? Je maendeleo ni kurudi nyuma?
 
Naunga mkono hoja lakini tatizo serikali hii inavyopenda ubabe sijui kama hatutaletewa geshi la banaichi
 
Tanzania wafanyakazi hamfiki hata milioni moja, so someni namba kwani nyie mliplay a big part kutuletea jiwe
 
Back
Top Bottom