Ni kweli Chama changu kinakwepa sana nafasi kama hizi kutoa ufafanuzi muhimu kwa mambo muhimu yanayojiri.huyo Mkonda hana upeo mpana anapwaya sana kwenye hoja za msingi.
Nape hayupo na kama angekuwepo asingethubutu kwenda kushindanisha hoja na Mnyika kwani uwezo wake ni mdogo sana na analitambua hilo. Sasa unategemea ccm wangemtuma nani kuwawakilisha?
Sasahivi wamekaa mbele ya tv zao wanashuhudia kijana wao anavyokukuruka.
Askofu anasema wajifunze kutokumkataa mtu ila wakatae mawazo yake kama hayafai,wanasiasa wa sasa wanakataa watu ndiyo maana wanatafutana kumalizana kisiasa kwa hila.
Mnyika anasema mwaka 2013 wananchi wanatakiwa kurudishiwa nguvu ya kuiwajibisha serikali, utakuwa mwaka wa hoja ngumu za rasilimali za nchi,utakuwa mwaka wa bunge la katiba na utakuwa mwaka wa jamii kupima utendaji wa serikali.Mnyika amehitimisha kwa kusema mwaka 2013 uwe mwaka wa upendo na uwajibikaji.
wasimamizi wa kipindi cha leo,hawakufanya haki ya kutusomea maswali na maoni yetu watazamaji,bado namuuliza mchungaji,atutajie matusi yanayotukanwa viongozi,isije kuwa ukweli kugeuzwa matusi
Kwa upeo na kiwango cha makonda kwenye medani ya siasa kupambanishwa na Mnyika, kajitahidi kwa kiasi chake kuliko wale wanaokimbia mijadala. Tusimwone hajafanya chochote.
wasimamizi wa kipindi cha leo,hawakufanya haki ya kutusomea maswali na maoni yetu watazamaji,bado namuuliza mchungaji,atutajie matusi yanayotukanwa viongozi,isije kuwa ukweli kugeuzwa matusi