Tunataka kuona ukomavu wa CCM sasa!

Tunataka kuona ukomavu wa CCM sasa!

Mchokoo

JF-Expert Member
Joined
Jul 28, 2015
Posts
1,188
Reaction score
1,604
Ni nani ambaye hajui kuwa ccm inapita katika bonde la uvuli wa mauti! Naaam, ni mahali hapa ambapo vyama tawala barani africa hufika na kufutika katika ramani za siasa.
Pamoja na kuwa natamani ccm ishindwe kabisa katika uchagizi huu, lakini sipendi taasisi hii kongwe ife kifo cha mende. Ni kwanini nataka ccm itoke magogoni lakini isiondoke Lumumba na dodoma?

Tusijidanganye wenyewe, maana ili tupige hatua za maendeleo tunahitaji chama tawala imara, na upinzani imara pia. Ndio maana kwa upande mmoja nafsi yangu inawapongeza sana mashujaa wanaotoka ccm na kujiunga katika kambi ya ukombozi, ingawa upande mwingine nakuwa na wasiwasi iwapo chama hiki kitasalimika hasa baada ya kushindwa katika uchaguzi unaotukabili.
Pengine unaweza kujiuliza swali, kwanini mambo haya mara nyingi hutokea zaidi afrika na si kwingineko

Tatizo ni kwamba vyama tawala barani havina msamiati wa kushindwa, na kwa hivyo huwa hawajajipanga kwa ajili ya hilo. Sasa basi lile lisilopendwa linapotokea; wanasiasa hao hustushwa mithiri ya mainzi yaondokavyo kwenye mashonde.

CCM mmechafuka, ni kweli, hamtufai sasa. Lakini hali hii haitaendelea siku zote. Mkibadilika ninyi na sisi tutabadikika nakuwahitaji tena. Kubalini kupata uzoefu ambao hamna sasa! Ninamaanisha uzoefu wa upinzani. Chonde chonde jamani, muungwana akivuliwa nguo huchuchumaa.
 
Leo mkuu nilikuwa katika group moja la team makomeo, wakaanza kutuhamasisha kesho kila mtu haende jangwani na rafiki zake at least wa3 na eti na kama Kuna anaekaa kinondoni kutakuwa na mabus ya kwenda jangwani kuanzia saa 5 Nimecheka Sana halafu wanasingiziaga Ni lowasa!! Yaani haya majizi yamekosa mvuto mpaka mnabeba watu kwi, kwi, kwi, kwi ngoja nitume na ujumbe wao hapa chini mkuu
 
Na huku ilala wamesema kesho kuna magari halafu watu watapewa kofia fulana na kila mtu atakula buku 5
 
Wakati Mwingine uwe unaangalia na uhalisia... CCM inatakiwa kuwa kibudu! Tuanze UPYA ... Kitu gani wameweza for 54 years ?.. acheni utani wakuu ...
 
Leo mkuu nilikuwa katika group moja la team makomeo, wakaanza kutuhamasisha kesho kila mtu haende jangwani na rafiki zake at least wa3 na eti na kama Kuna anaekaa kinondoni kutakuwa na mabus ya kwenda jangwani kuanzia saa 5 Nimecheka Sana halafu wanasingiziaga Ni lowasa!! Yaani haya majizi yamekosa mvuto mpaka mnabeba watu kwi, kwi, kwi, kwi ngoja nitume na ujumbe wao hapa chini mkuu

Kaka alafu naona kama ulifungua uzi fulan kuhusiana na hichi ila sijui umetolewa..?
 
Kaka alafu naona kama ulifungua uzi fulan kuhusiana na hichi ila sijui umetolewa..?
yeah wanautoa sijui Ni kwanini!!! Wakati ni kweli, hawa MODS WA jf sijui washanunuliwa na wao!:A S confused:
 
Back
Top Bottom