Tunapohitaji msaada na njia tunazotumia

Tunapohitaji msaada na njia tunazotumia

2v1

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2024
Posts
253
Reaction score
384
Siku mbili tatu nimekuwa nikichati na chatgpt na nimekuwa nikimuuliza maswali, kuhusu maelezo mafupi ya muziki wa juice wrld na kupelekea kujikuta nikimuuliza na maisha yake juice world.

Kiujumla moja ya mambo ambayo nimeyaona na ningependa tujuzane leo ni:

Kutozingatia watu wanapohitaji msaada.

Mf juice world katika wimbo wake wishing well alisema
"Ring-ring, phone call from depression
You used my past and my memories as a weapon
On the other line, I talk to addiction, huh
Speaking of the devil, all the drugs, I miss them
This can't be real, is it fiction?
Somethin' feels broke, need to fix it
I cry out for help, do they listen?
I'ma be alone until it's f
inished"

yaani

"Ring-ring, simu kutoka kwa huzuni
Umetumia maisha yangu ya nyuma na kumbukumbu kama silaha
Kwa upande wa pili, nazungumza na uraibu, huh
Nikimzungumzia shetani, madawa yote, nawakumbuka
Hii haiwezi kuwa kweli, ni hadithi?
Kuna kitu kimevunjika, kinahitaji kutengenezwa
Nalia kuomba msaada, je, wanasikiliza?
Nitakuwa peke yangu hadi yote yaishe."

Tujitahidi kuwa nao karibu, mtu yoyote anapoonesha anahitaji masaada. Tusiwaache watu hawa peke yao kwa sababu hatujui mwisho wake utakuaje.

Kupambana na huzuni na maumivu ya kihisia.

Kila mtu ananjia zake za kupambana na huzuni na maumivu ya kihisia, juice wrld alitumia madawa ya kulevya kama njia ya kutuliza hisia hizo ingawa alijua njia hiyo ilimletea madhara zaidi.

Mimi binafsi napenda kukaa peke yangu na kufikiria njia la kulitatua na huwa napenda kula vizuri nikiwa na stress zangu, je! wewe hutumia njia gani? ni hayo tu.
 
Napenda kusikiliza mziki na kwenda kupiga tizi kabla ya kurudi na kukuta suala limeisha automatic.
 
  • Thanks
Reactions: 2v1
Nikiwa na stress, hata sijui...just anything can soothe my broken soul, msosi, muziki/gospel, a beautiful lady...just anything.
 
  • Thanks
Reactions: 2v1
PORN.



Just kidding. Movie na series zinakupeleka ulimwengu tofauti kabisa.
 
  • Thanks
Reactions: 2v1
Back
Top Bottom