Tume ya ajira mzigo kwa serikali:

Tume ya ajira mzigo kwa serikali:

Kimboko

Member
Joined
Nov 16, 2010
Posts
56
Reaction score
7
Ndugu zangu salaam,

Kwanza nitoe pole kwa sisi wote tulioomba kazi kupitia matangazo ya tume ya ajira tangu mwaka jana mwanzoni.

Ni jambo la kushanga sana kwa taasisi hii ya ajira vitengo vyote kutangaza kazi halafu wasiweke wazi ni namna gani wanapata hao wafanyakazi.

Kwani wanaitaje wasailiwa kwenye usaili jamani??

Kama kuna mlioitwa ebu nipeni namna ya wanaovyoita. Najua wanatangaza kwenye tovuti yao lakini ni wangapi mlioakwisha wahi kuitwa ata kwenda kuhudhuria hizo saili!!

Habari nilizozipata ni kwamba, tume hii iliundwa kwa maslahi ya wachache ya kwamba wangekuwa wanalipwa hela na wale wanaotaka wafanyakazi ili kutangaza hizo kazi, kutangaza kuitwa kwenye usaili na hatimaye kuajiri; je mchakato huu utaenda kihalali kweli ndugu zanguni??

Sasa kilichofichuka ni kwamba hizo taasisi hazina hela za kuwapa tume ya ajira kwa sababu hawana budget kwa ajili ya fungu hilo.

Hebu jiulizeni jamani, utoe hela mfuko huu uweke mfuko wa pili au unatoa hela mfuko wa kulia unaweka mfuko wa kushoto hii inaleta maantiki kweli!!!

Sasa habari zakuaminika ni kwamba hawapati hela kama wlivyptarajia na ndo maana hawaiti watu kwenye usaili kwa sababu hawawezi kukaa bure kusaili watu bila mshiko, wamekalia kufikiri posho tu siyo maslahi ya taifa, sasa taasisi zilizotaka wafanyakazi hawajapata na taifa linazidi kwenda mrama kwa kukosa wafanyakazi mahiri kama sisi tulioko nyumbani tunalea watoto bila ajira.

Hebu naomba mnipe ushauri au muwape ushauri Serikali yetu kwamba tunakokwenda utakuta taasisi moja ina kabila moja kuanzia mhudumu hadi mkurugenzi kama Luhanjo alivyofanya TANAPA na TASAF. Kaweka wakurugenzi wa kwao we unategemea kupata ajira hapo kweli.

Tuangalie sana ndugu zanguni ukabila unaletwa na hawa wajamaa waliokaa kwnye viti huko juu, ukienda tasaf sasa hivi utakuta madriver wa darasa la saba ukiuliza ni ndugu wa fulani na yule ni ndugu wa yule ilimradi wawekane wale wenyewe ata kama mtu hana sifa.

Niishie hapa nanyi mchangie jamani hali ni mbaya.
 
Kwani Tanzania tuna ukabila si kila mtu anatambulika kama Mtanzania na sio Mbena kama Luhanjo na ndugu zake
 
Mbona watu kibao tu wameshaitwa. Mimi binafsi nimeitwa mara tatu kwenye usaili bila kuwa na uhusiano na mtu yeyote wala kujuana..
Wewe umefanya utafiti gani kusupport hayo unayosema?
 
Jamani tuwe na Subira, maana hata kama tukiitwa wote bado hawataweza kutuajiri wote. Ingekua vizuri kama ungefanya utafiti ili kubaini kwa nini haukuchaguliwa nadhani jibu lingekusaidia sana. Hii hali kukatishana tamaa sio nzuri maana wapo wengi wamepata na wala hawakua na watu waliwashika mkono.
 
Unataka kusaidiwa nn? Mbona usaili ushafanyika siku nyingi sana, na kuna waliokwishaitwa makazini? Unaishi sayari gani ndg?
 
Ndugu zangu salaam,

Kwanza nitoe pole kwa sisi wote tulioomba kazi kupitia matangazo ya tume ya ajira tangu mwaka jana mwanzoni.

Ni jambo la kushanga sana kwa taasisi hii ya ajira vitengo vyote kutangaza kazi halafu wasiweke wazi ni namna gani wanapata hao wafanyakazi.

Kwani wanaitaje wasailiwa kwenye usaili jamani??

Kama kuna mlioitwa ebu nipeni namna ya wanaovyoita. Najua wanatangaza kwenye tovuti yao lakini ni wangapi mlioakwisha wahi kuitwa ata kwenda kuhudhuria hizo saili!!

Habari nilizozipata ni kwamba, tume hii iliundwa kwa maslahi ya wachache ya kwamba wangekuwa wanalipwa hela na wale wanaotaka wafanyakazi ili kutangaza hizo kazi, kutangaza kuitwa kwenye usaili na hatimaye kuajiri; je mchakato huu utaenda kihalali kweli ndugu zanguni??

Sasa kilichofichuka ni kwamba hizo taasisi hazina hela za kuwapa tume ya ajira kwa sababu hawana budget kwa ajili ya fungu hilo.

Hebu jiulizeni jamani, utoe hela mfuko huu uweke mfuko wa pili au unatoa hela mfuko wa kulia unaweka mfuko wa kushoto hii inaleta maantiki kweli!!!

Sasa habari zakuaminika ni kwamba hawapati hela kama wlivyptarajia na ndo maana hawaiti watu kwenye usaili kwa sababu hawawezi kukaa bure kusaili watu bila mshiko, wamekalia kufikiri posho tu siyo maslahi ya taifa, sasa taasisi zilizotaka wafanyakazi hawajapata na taifa linazidi kwenda mrama kwa kukosa wafanyakazi mahiri kama sisi tulioko nyumbani tunalea watoto bila ajira.

Hebu naomba mnipe ushauri au muwape ushauri Serikali yetu kwamba tunakokwenda utakuta taasisi moja ina kabila moja kuanzia mhudumu hadi mkurugenzi kama Luhanjo alivyofanya TANAPA na TASAF. Kaweka wakurugenzi wa kwao we unategemea kupata ajira hapo kweli.

Tuangalie sana ndugu zanguni ukabila unaletwa na hawa wajamaa waliokaa kwnye viti huko juu, ukienda tasaf sasa hivi utakuta madriver wa darasa la saba ukiuliza ni ndugu wa fulani na yule ni ndugu wa yule ilimradi wawekane wale wenyewe ata kama mtu hana sifa.

Niishie hapa nanyi mchangie jamani hali ni mbaya.

Madai yako ni ya kukurupuka...Watu tumeitwa, tumeajiriwa, watu wenye sifa wote wameajiriwa...Inaelekea wewe huna taarifa. Pitia kila mara kwenye tovuti ya sekretarieti (Kama unapitia tovuti ya Tume ya ajira unachemka).
Kuhusu kupewa hela na Taasisi zinazohitaji watu pia ni uzushi uliopitiliza....Sekretarieti ya Ajira ina bajeti yake kupitia Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi...Kuhusu TANAPA na TASAF huu ni uzushi pia, hizi ni miongoni mwa Taasisi ambazo haziajiri kupitia sekretarieti sasa uhusiano hapoi upoje? Acha malalamiko kijana, subiri nafasi yako ambayo una fit omba kwa kujiamini, fuatilia matatngazo ya kuitwa Interview ukiitwa jiamini utapata tu. Watanzania haka ka tabia ka kutanguliza malalamiko sijui tutakaacha lini?.......na mwisho acha kupanda basi la ukabila
 
kama ungelikuwa umefanya utafiti vizuri usingeacha kutaja wachagga na wahaya. Hawa ndo wanaongoza wengine cha mtoto. Siku hizi nimesikia hata kina mwanakampwala na wale wa turiripereke kituoni wanakuja juu.
 
hawa tume ya ajira hawako fair,kama wanabase kwenye GPA,hivi hawa wenye lower second na pass wao wanastahili kufanya kazi sekta ipi?manake wanarecruit based on GPA,sasa wenye lower performance hawastahiii government,binafsi ni mhanga hata ktk interview hawaniit,Je tanzania sasa 2naweigh GPA ndo kigezo!
 
mimi mwenyewe niliitwa mwaka 2010 kwenye interview ya Computer Analyst II. nikafanya vizuri na sasa nipo hapa Hazina nakula shavu la serikali.
 
Back
Top Bottom