Tulivyokuwa tukiiba almasi mgodi wa Mwadui na wenzetu kuuawa

Sisi ndio tulikuwa tunaishi pale kabla kachuchuru hajahamia.
Kabla ya mwl Kachuchuru ile nyumba aliishi mzee Gordon labda utakua we ni mtoto wake... watu mwadui sio tumeishi tu bali tumezaliwa na kukulia pale... kiboko ya wabeshi alikua marehemu mzee Kirahi Oguma alikua polisi chini ya kamanda mzee Mbelwa, enzi hizo Mwadui kweli mwadui miaka ya 80 kurudi nyuma.
 
Dah, pole sana mkuu kwa msoto wa maisha, ama kwa hakika story yako imenivutia sana, imenipa somo kubwa sana la kujifunza japo ni story inayotisha inatia huruma na pia inasisimua kwa kuwa in true story, pole sana mkuu.
 
Du yaani una nikumbusha mwadui ni sehemu niliyokulia kwa kweli maisha ya mgodini miaka hiyi ya 80 ni Kama vile uko ulaya kumbe nyie ndio mlikuwa wezi du poleni Mara mlijigeuza fisi
Aaaa nyie watoto wa mgodini mlikuwa mnakula raha sana;na mlijisahau mkadhani mtaishi mle milele.Duka kubwa unakutana na nyama za kutoka Daily Farm na mikate,maziwa ya token mlangoni,ukitembelea recreation club ndio balaa...hizi mambo ndio zilitupa hasira sana tuliokaa kandokando ya mgodi mpaka tukawa tunavamia kuiba.

Utakuwa mtoto wa Boidi ya Juu au ya Chini?Au Alamasi Road?
 
Kulikuwa na kikosi hatari sana cha mbwa na farasi,na walikuwa wakifanyia mazoezi kule Line Polisi kama unaelekea kijiji cha Utemini,kweli Mwadui ilikuwa kama Ulaya.

Maziwa kedekede,nyama za kutosha na mabasi ya kuzunguka ndani ya mgodi,toka Kampaundi mpaka Alamasi Road.Kuna boss alikuwa anaitwa Mipawa,huyu aliunda kikosi hatari sana cha mbwa na farasi;walitusumbua sana hasa njia yetu ya kupitia Songwa,Bwawani mpaka Mgodini.

Mkuu ww wa TS,Mwaseco au Agriculture?Umenikumbusha mbali,team ya mpira na marefa kina Mzee Mshangama sisi tukija kushangaa mpira kupitia geti kubwa kwa ruhusa maalumu,halafu jioni tunarudi kama wabeshi.Kweli maisha ni safari ndefu
 
Longo
 
Charles Kihiyo mgosi
 
Hatari sana...babu yangu mzee Mipawa siku hizi ni diwani wa kata ya SayuSayu-Maswa.
 
Mwadui boidi ya huu na nimezaliwa hapo na kusoma hapo
Basi wewe mkuu mbaswike utakuwa ulisoma ama Mwadui A au Mwadui B.Kwa mwalimu Nyabi,Ntantulu,Masunga na Miss Lewis....Nyie watoto wa mwadui mlikuwa mnatukebehi sana wabeshi nyie...
 
Mkuu,Barafu nmekupa salute..umeuza ile chumvi ya NYALAJA!!?
Mkuu Ntaluke.N. salute pia kwako,maana unapita mulemule nilimopite.Nisipouza chumvi ya Nyalaja sasa ntakuwaje mbeshi??Yaani unataja misamiati hatari sana ya miaka hiyoooo....Umenikumbusha mbali sana mpaka nakumbuka jamaa zangu waliotangulia mbele za haki...Asante sana mkuu
 
Hatari sana...babu yangu mzee Mipawa siku hizi ni diwani wa kata ya SayuSayu-Maswa.
Mkuu huyu alikuwa Meneja,alitusumbua sana kwa kuunda Kikosi cha mbwa na Farasi waliokuwa wanapata mafunzo toka Nje ya nchi.Baada ya Ubaguzi wa rangi kuisha,wale mbwa wakawa wanaletwa toka South Africa,ile "specie" ya mbwa waliokuwa wanatumika kuuwa watu weusi wakati wa maandamano ya ubaguzi wa rangi S.Africa.

Wale mbwa ndio waliletwa wakiwa na mafunzo makari sana na walikuwa mbwa katiri sana sana.Jamaa zetu wengi walikufa kwa kuumwa na wale mbwa.Ninamkumbuka huyo Meneja akiitwa Sylivester Mipawa.Kumbe sasa ni diwani?Duuuh.... kituli one mpe salamu anko wako mzee wa benzi
 
maskini mwadui kwisha habari yake imebaki story,wapi swai mikate,wapi hiporaiti moshi,wapi dkt tosiri,wapi chekingo na kabondo mapilot wetu enzi hzo,wapi mwalimu mutembei na mwalimu musa wa ts,wapi mwalimu gontako na mwalimu kachuchuru wa mwadui sec,wapi mwalimu kasoyaga wa mwadui mashariki,wapi mzee ngoromole,mzee ndaki konda wa mabasi ya mwadui,wapi idara ya shamba,wapi dairy farm,wapi golf,wapi ujamaa c,wapi posta na simu,daaah kweli mwadui ilikuwa nzuri sana,mzee wetu muhali,mzee wetu bugome,mzee kimolo,mzee kailembo dj mwakapesa,mzee hincha
 
Mwadui miaka ya 80 ilikua tayari chali ishachoka sana ...mwadui 80 rudi nyuma ndio ilikua little London in Africa..ndege twice a week to Nairobi.. 80 ilikua ishachoka sana.
Picha ya mwadui wakuu ,natamani kufika huko niojionee
 
Mzee Hiporaiti moshi yupo Dar anakula shushu taratibu
 
Umesahau Mashine Kubwa na duka kubwa!!Songwa Club na Twiga Hostel,Team ya Mwadui na kina Mshangama.

Sema watoto wa Mwadui mlikuwa na dharau sana kama mnaishi Ulaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…