Tujifunge mkanda dhidi ya nchi za Magharibi


Sidhani kama kuna nchi yoyote ambayo haitakuwa na interests zake akikusaidia
Sio wamarekani tu hata wachina, wajapani, wahindi etc
Usipojisimamia Na kujikwamua mwenyewe basi utabaki kuwa mtumiwaji tu
 
UPEO WAKO NI WA KIPEKEE KABISA KUPATA KUUONA HAPA JF,BRO MAWAZO YAKO YANALENGA BARA ZIMA LA AFRIKA, FIKRA ZAKO HAZINA UBINAFSI HATA KIDOGO..MUNGU IBARIKI AFRIKA....LIKE.

Barikiwa ndugu,Sifa ;heshima na utukufu namwachia Mungu
 
Tunajiibia wenyewe wala tusitafute visingizio
Angalia kama issue Ya IPTL sijui Escrow mara Lugumi
Hao nao ni wametoka the western world???
Yule singasinga katokea wapi?
Lugumi kwao wapi?
Lipumba kwao wapi?

Ukifuatilia kwa ufahamu wenye rutuba hata wizi mkubwa wenye kunyonya mataifa mengi maskini kuna uratibu wa karibu wa mabenki makubwa ya dunia {Magharibi,makampuni makubwa ya dunia {Magharibi},majasusi wa kiuchumi wenye kofia ya uzawa wakisimama kama madalali wakuu..viunganishi...nomino...
Mfano tu :
{Richmond=Dowans=Symbion=?
;{IPTL=Merchar=PAP=SCB [HK}=?
 

Lugumi?
Meremeta?
UDA?
ATCL ?
 
Mwaka huu mtajifunga mpaka nyuzi za viroba.
 

Ukatiri,uonevu,vita,chokochoko,ujambazi wa utajiri wetu kwa jina la demokrasia/misaada/Haki za binadamu haupaswi kutetewa na yeyote mwenye kufahamu gharama ya uhuru wa mataifa yetu...ukombozi mamboleo umewadia ...viongozi legelege wenye kusema ndio kwenye kila linalonenwa na waliokuwa wakoloni wetu sidhani kama wana nafasi..hata viongozi wa vyama wenye kuwanyenyekea waliokuwa wakoloni ili tu wawezeshwe kushika dola hawana tofauti na wakoloni mamboleo husika
 
KULA ULE PEKE YAKO.....MKANDA TUFUNGE SOTE? ULIYE TAFUTA NAE KUNI NDIO UTAKAYE OTA NAE MOTO
 

Naona unamsema mkweree kiaina hapa
 
Ukweli ukizihiri uongo hujitenga mbona hukulisema lile la dhulma lililofanyika kule Zanzibar na kuwanyanganya wazanzibar ushindi Wao wa octobar 25-2015

Siasa ni mchezo ambao wengi wanaoucheza hawajui asili yake,ukweli wake,mbinu zake,siri zake ,miiko yako,tamaduni zake,...waliotuletea inayoitwa demokrasia wenyewe inawasumbua na inawashinda...Yatuppasa kujitambua zaidi,kujitafakari zaidi..
je manufaa ya hizi siasa zetu ni umoja?Mshikamano?Undugu?Maendeleo?Ustawi wa jamii zetu?Kuondoa umaskini?...
Ni nchi gani toka dunia ya tatu imeendelea kwa kinachoitwa demokrasia?..

Ieleweke sipingi haki za kidemokrasia lakini sio demokrasia yenye kulenga kuwafurahisha wanyonyaji,majambazi wa rasilimali zetu...Demokrasia inayofuhaia umaskini endelevu wa washangilia khanga,kofia,chumvi,vijipesa,ubwabwa,viroba wakati wa kampeni.....
 

South Korea and Singapore, used to be third world countries
 
USA hana ubavu tutampiga kama tulivyo mpiga idi amini sisi hutuhitaji upuuzi wake name sisi tutamuekea vikwazo ale majani mwitu
 

we unaona Mugabe kutawala hadi miaka zaidi ya 30 nisawa kisa, Africa. Mseveni kutawala zaidi ya miaka 30 niswa, kisa Africa. Nchi zinaitisha uchaguzi hewa, wanatumia pesa nyingi katika chaguzi, wananchi wakiamua kuweka kiongozi mwingine kupitia sanduku la kura watawala wanabadilisha matokeo, halafu unasema ohhh Afrika, utumwa, ukoloni, hii nishida ya kjitakia. Tenda haki halafu ukiona pamoja na haki kutendeka bado kuna uvunjifu wa amani ndio ulalamike. sasa wewe unakandamiza haki za raia, wakifurukuta na wazungu wakaona kweli kuna tatizo ndio unakumbuka kuwa una uzalendo? Hii haikubaliki. Wee hubiri haki kwanza, halafu fuatia amani halafu ndio utuambie habari ya ukoloni na utumwa!
 
Waambie viongozi wajifunge mkanda, Waambie viongozi watende haki, Waambie viongozi wafuate sheria,

Huu mkanda wetu sisi mbona tulijifunga tangia UHURU!
Ni nan atatufungua? Maana kila baada ya uchaguzi maneno na matendo ni yale yale.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…