Tuijadili kauli hii: "Kuanzia leo namsimamisha kazi kiongozi huyu kwa mamlaka niliyonayo"

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,244
7,966
Wadau hebu tufafanuliane juu ya tafsri ya statement hii! Kikatiba/kisheria unapotaka kumsimamisha kazi unafanyaje? Nini tafsiri ya hili neno mbele ya kadamnasi kabla hata ya uchunguzi?

Ni swali tu maana wengi wetu tunafurahia kusikia flani katumbuliwa mbele ya halaiki.Kumwandikia mtu barua kua unamsimamisha kazi hakutoshi? Maana hata kasi waliyonayo maDC na maRC kutumbua majipu hadharani sio ndgo.
 
Ni uvunjaji wa sheria za utumishi wa umma hata kama mamlaka yakiwa yake nchi hii tunaongozwa kwa sheria na hakuna aliye juu ya sheria.
 
Kuna vitu vingine haya masuala ya sheria yatafuata baadae lkni kitu kimetumbuliwa. Maana hakuna kinachoharibika kwenye hizi nafasi za uteuz. Mshahara wako upo pale pale
 
Wadau hebu tufafanuliane juu ya tafsri ya statement hii! Kikatiba/kisheria unapotaka kumsimamisha kazi unafanyaje? Nini tafsiri ya hili neno mbele ya kadamnasi kabla hata ya uchunguzi?

Ni swali tu maana wengi wetu tunafurahia kusikia flani katumbuliwa mbele ya halaiki.Kumwandikia mtu barua kua unamsimamisha kazi hakutoshi? Maana hata kasi waliyonayo maDC na maRC kutumbua majipu hadharani sio ndgo.
Kosa ni kufukuzwa kazi kabla ya uchunguzi/kujojiwa...otherwise kusimamishwa kazi huitaji prior notice...afterall, unasimishwa ili uchunguzi ufanyike...uelewa wako mdogo kwenye maswala ya sheria
 
Anayetaka Tafsiri ya maneno hayo ktk lugha nadhifu ys kiswahili arudi Darasani akasome Kiswahili au awasiliane na BAKITA.Hawa jamaa huwa wana kipindi REDIO ONE siku ya Jumapili asubuhi akisikilize atenge muda Maswali kama haya hawezi kuwa anauliza humu JF
 
Hakuna mwanasiasa mwenye uwezo wa kumfuta mtumishi wa uma kazi!!

Na kumsimamisha mtu kazi haimaanishi kafutwa kazi.
 
Back
Top Bottom