Tuambieni mabaya yake!

Tuambieni mabaya yake!

Mandevis

Member
Joined
Sep 1, 2015
Posts
70
Reaction score
29
Nimekuwa msomaji ktk JF kwa muda mrefu sana. Na hii ni kati ya posts zangu za mwanzo kabisa. Ombi langu kwa wasomaji wa JF ni moja:- Kwa kuwa CCM wanamzungumzia sana mgombea urais kupitia UKAWA yaani Mh. Lowasa hasa kwa mabaya yake, basi na wanaomuunga mkono Lowasa nao waongee mambo mabaya ya Mh. Magufuli tuyasikie.

Nimeandika hivi kwa sababu kubwa mbili:- kwanza, naona wapinzani wanatumia nguvu nyingi kumchafua Rais Kikwete na familia yake ambaye amebakiza mwezi mmoja amalize kazi yake, pia wanapoteza mda mwingi kumponda Dr Slaa ambaye si mgombea urais, mambo ambayo kwangu naona hayana faida na ni kupoteza muda wao bure!

Sababu nyingine ni, mnatunyima wananchi haki ya kujua mabaya ya Magufuli maana yale mnayotuambia ya kuuza nyumba inaelekea sio yake bali la baraza zima akiwemo Lowasa na Waziri mkuu ​Sumae pia.

Wana UKAWA tajeni ubaya wa Magufuli tusikie maana kwa kuacha kuyataja mnatufanya tuamini kuwa Dr Magufuli ndiye anayefaa kuwa rais wetu wa awamu ya tano!
 
Kwani tatizo la lowassa kama lowassa ni nini? Ile Richmond haikuwa ya lowassa pekee kama ilivyo kwa magufuli ya kuuza nyumba za serikali na kujimilikishia zingine.

Hilo la kujilimbikizia Mali sio hoja, niambie ni kiongozi gani hakujilimbikizia Mali????

La msingi wagombea wshindane kwa sera na utendaji.
 
Binafsi nampenda Magufuli kwa jambo moja tu, kuchukua maamuzi na kusimamia maamuzi yake tatizo langu lipo kwa chama chake.

Kwa upande mwingine hayo ya kuuza nyumba za serikali siwezi kuyaongelea sana , ila kwa hili la kujenga barabara chini ya kiwango ntamlaumu, tumetumia gharama kubwa kwa kupata barabara chini ya kiwango ambazo muda sio mrefu tutarudi kulekule tulikotoka. Hayo ya hasara za kuchelewa kuwalipa wakandarasi na hasara za fidia ya meli ya wavuvi nayo sitii neno sana.

Kinachonifanya nisimpe kura yangu ni kimoja tu, chama chake ndio kimeingia mikataba mibovu na kuendelea kuisababishia nchi umasikini licha ya kua na rasilimali nyingi. Anavyo ahidi kwamba ataleta mabadiliko, atarudi tena kwa watu hao avunje mikataba iliyoingiwa na chama chake kinachoiongoza serikali ambayo yeye ndio atakua rais endapo atachaguliwa?
 
Mkuu japo kuwa umejiaunga September mwaka huu na hii ni pots yako ya tano lakini umenena..Waseme
 
Back
Top Bottom