Ninauza Daf CF 430 HP toka UK imetoka bandarini juzi, rangi yake ni nyeupe (Pearl white) na ina hali nzuri sana. Bei ni maelewano. Endapo mtu anataka kuiona ipo Temeke Mwisho na kwa mawasiliano zaidi piga 0717 615535 au 0789 100891. Karibuni sana.
Mkuu biashara yako unaruhusu mtu kulipa kidogo kidogo(kwa installment)?
Sijaelewa maana ya 'Tracto', au unamaanisha Tractor?
Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
Mkuu dereva wa lorry policy yangu ya mauzo hairuhusu hilo ndio maana bei zetu kidogo ziko chini. Karibu sana.
Sawa Bobby, weka picha na bei basi tuone kama tutaweza kabla hatujapiga simu au kuchoma mafuta mpaka Temeke.
Mkuu toa specs za gari, engine size, uzito maana ya tani? Jee unalo trailer lake au inabidi nichongeshe. Mwaka wa gari? Niambie matairi yametumika muda gani? maana 50% au 75%.
Good umejibu majibu yangu kama nilivyotaka, next time weka hizo specs mwanzoni. Sasa kingine jee ni kiasi gani linauzwa? Pili jee ni day cab au sleeping cab? Kama ni sleeping cab naamaanisha ina kitanda jee inakuwa ndani ya sheria za Tanroad au naitaji kibali cha kila mwaka cha kuoperate over size trailer.
Sleeper ambazo inabidi uwaone Tanroad ni zile longnose za kimarekani au volvo zile zenye pua. Kwasababu urefu wa tractor na trela kwa pamoja unazidi meters allowed by tanroad. Hizi european trucks(cab over) hazina shida na Tanroad.