Tochi za Trafiki barabarani balaa!

Tochi za Trafiki barabarani balaa!

mysee

Member
Joined
Apr 4, 2014
Posts
74
Reaction score
9
Nilidhani utetezi tu wa madereva waliokuwa wanadai wanatozwa faini kwa kosa la mwendo kasi Over 50 Km/hr maeneo yenye tahadhari hii.

Nikaona siku moja katika safari yangu nijionee, nilipo fika Mdaula eneo lenye maelekezo hayo nikapunguza mwendo mara gafla tokea ichakani akajitokeza afande akiwa na tochi kunisimamisha baada ya salamu akaielekeze screen ya tochi 65 Km/Hr akanipotezea muda kwa malumbano.

Ikandoka kufika mizani eneo la Mlandizi nikiwa nawaona askari kwakua hakukua na gari kubwa mbele nikawa naenda 35Km/hr nikasimamishwa tena,kwakua sikua na tatizo lolote nikajua atakagua gari niondoke askari akanionesha tochi tena 65k/hr nilipanic tukaanza debate wakaja wenzake wawili kumsaidia, kilicho nibore kali zao, eti wamechukua leseni yangu,wakataka kuniandikia notification wakati huo wananitishia twende kituoni kwakuwa nimekana speed yangu jumatatu wanipeleke mahakamani.

Ilikuwa Jumamosi, hawa ndio waliniptezea muda zaidi kwakuwa sikuwa na haraka nilitaka nione mwisho wake takuaje nikasubiri sanaaa.
 
Hahahahaaa basi kila Mkoa na speed yake, maana wale wa Chalinze Kuelekea Tanga na kilimanjaro wao wanakuonyesha Speed 55KM/Hr yaani kila anayekamatwa anaonyweshwa speed hio hio walishanikamata mara kibao sana ila kila siku speed ni hio hio najiuliza hivi hizi mashine zao zinafanya kazi kweli au ni geresha? Haiwezekani kila nikikamatwa iwe ni 55 na hata wengine hupewa speed hio hio ya 55 hawa jamaa ni MIJIZI iliyokubuhu. Sijui kwanini hawataki kutoa EFD mashine zitumike maana kinachoendelea pale ni wizi mtupu
 
Back
Top Bottom